< 4 Царе 16 >
1 В седемнадесетата година на Факея, Ромеловия син, се възцари Ахаз, син на Юдовия цар Иотам.
Katika mwaka wa kumi na saba wa utawala wa Peka mwana wa Remalia, Ahazi mwana wa Yothamu mfalme wa Yuda alianza kutawala.
2 Ахаз бе двадесет години на възраст, когато се възцари, и царува шестнадесет години в Ерусалим; но не върши това, което бе право пред Господа своя Бог, както баща му Давид,
Ahazi alikuwa na miaka ishirini alipoanza kutawala, akatawala huko Yerusalemu kwa miaka kumi na sita. Tofauti na Daudi baba yake, hakufanya yaliyo mema machoni pa Bwana, Mungu wake.
3 но ходи в пътя на Израилевите царе, и даже преведе сина си през огъня според мерзостите на народите, които Господ изпъди пред израилтяните.
Akaenenda katika njia za wafalme wa Israeli, na hata akamtoa mwanawe kafara katika moto, akifuata njia za machukizo za mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele ya Waisraeli.
4 Той жертвуваше и кадеше по високите места, и по върховете и под всяко зелено дърво.
Akatoa kafara na kufukiza uvumba katika mahali pa juu pa kuabudia miungu, juu ya vilima, na chini ya kila mti uliotanda.
5 Тогава сирийският цар Расин и Израилевият цар Факей, Ромелиевият син, дойдоха в Ерусалим да воюват, и обсадихаАхаза, но не можаха да му надвият.
Kisha Resini mfalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli wakaondoka kwenda kupigana dhidi ya Yerusalemu na kumzunguka Ahazi kwa jeshi, lakini hawakuweza kumshinda.
6 В онова време сирийският цар Расин възвърна Елат под Сирия, и изпъди юдеите из Елат; асирийците дойдоха в Елат та живееха там, гдето са и до днес.
Wakati ule, Resini mfalme wa Aramu akaurudisha Elathi kwa Aramu kwa kuwafukuza watu wa Yuda. Kisha Waedomu wakahamia Elathi, nao wanaishi huko mpaka leo.
7 Затова Ахаз прати човеци до асирийския цар Теглат-фаласар да кажат: Аз съм твой слуга и твой син; възлез да ме избавиш от ръката на сирийския цар и от ръката на на Израилевия цар, който се подигна против мене.
Ahazi akatuma wajumbe kumwambia Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru kwamba, “Mimi ni mtumishi na mtumwa wako. Njoo na uniokoe kutoka mkononi mwa mfalme wa Aramu na wa mfalme wa Israeli, ambao wananishambulia.”
8 А Ахаз взе среброто и златото, което се набери в Господния дом и д съкровищницата на царската къща, та ги проти подарък на асирийския цар.
Naye Ahazi akachukua fedha na dhahabu zilizopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina ya jumba la mfalme, na kuzituma kama zawadi kwa mfalme wa Ashuru.
9 И асирийския цар го послуша и възлезе против Дамаск та го превзе, и тведе жителите му в Кир, а Расина уби.
Mfalme wa Ashuru akamwitikia kwa kushambulia Dameski na kuiteka. Akawahamishia wenyeji wake huko Kiri, na kumuua Resini.
10 А когато цар Ахаз отиде в Дамаск да посрещне асирийския цар Теглат-феласар, видя жертвеника в Дамаск; и цар Ахаз изпрати на свещеника Урия образа на жертвеника, и рисунка на него, точно според направата му.
Kisha Mfalme Ahazi akaenda Dameski kukutana na Tiglath-Pileseri wa Ashuru. Akaona madhabahu huko Dameski, naye akamtumia Uria kuhani mchoro wa hayo madhabahu, pamoja na maelezo ya mpango kamili wa ujenzi wake.
11 И свещеник Урия направи жертвеник точно според това, което цар Ахаз прати от Дамаск; така го направи свещеник Урия догде се върна цар Ахаз от Дамаск.
Kwa hiyo Uria kuhani akajenga madhabahu kulingana na mipango yote ambayo Mfalme Ahazi alikuwa ameituma kutoka Dameski, na akamaliza ujenzi kabla ya Mfalme Ahazi kurudi.
12 И когато се върна царят от Дамаск, видя жертвеника; и царят се приближи при жертвеника та направи принос върху него.
Mfalme aliporudi kutoka Dameski na kuona hayo madhabahu, akayasogelea na kutoa sadaka juu yake.
13 И върху тоя жертвеник изгори всеизгарянето си и хлебния си принос, и изля възлиянието си, и поръси кръвта на примирителните си приноси.
Akatoa sadaka yake ya kuteketezwa na sadaka ya nafaka, akamimina sadaka ya kinywaji na kunyunyizia damu ya sadaka zake za amani juu ya hayo madhabahu.
14 А медният олтар, който бе пред Господа, премести от лицето на дома, от мястото му между жертвеника и Господния дом, и го постави на северната страна от жертвеника.
Mfalme Ahazi akayaondoa madhabahu ya zamani ya shaba kutoka hapo mbele ya Hekalu la Bwana, yaliyokuwa yamesimama kati ya ingilio la Hekalu na hayo madhabahu mapya, naye akayaweka upande wa kaskazini mwa hayo madhabahu mapya.
15 И цар Ахаз заповяда на свещеника Урия, казвайки: На великия жертвеник принасяй утрешното всеизгаряне, вечерния хлебен принос, царското всеизгаряне и хлебен принос, с всеизгарянето принасяно от всичките люде на земята и хлебния им принос и възлиянията им, и ръси върху него всичката кръв на всеизгарянето и всичката кръв на жертвата; а медният олтар ще служи за мене за да се допитвам до Господа.
Ndipo Mfalme Ahazi akatoa amri zifuatazo kwa Uria kuhani: “Juu ya hayo madhabahu kubwa mapya, toa sadaka ya asubuhi ya kuteketezwa na sadaka ya jioni ya nafaka, sadaka ya mfalme ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya nafaka, sadaka ya kuteketezwa ya watu wote wa nchi, pamoja na sadaka yao ya nafaka na sadaka yao ya kinywaji. Unyunyize juu ya hayo madhabahu damu yote ya sadaka za kuteketezwa na dhabihu. Lakini mimi nitatumia hayo madhabahu ya zamani ya shaba kwa ajili ya kutafuta uongozi.”
16 И свещеник Урия стори така, точно според както му заповяда цар Ахаз.
Naye Uria kuhani akafanya kama Mfalme Ahazi alivyoagiza.
17 А цар Ахаз отсече страничните плочи на подножията, и дигна от там умивалника; и свали морето от медните волове, които бяха под него, та го тури на каменен под.
Mfalme Ahazi akaondoa mbao za pembeni na kuondoa masinia kwenye vile vishikilio vilivyohamishika. Akaondoa ile Bahari kutoka kwenye mafahali wa shaba walioishikilia, na kuiweka kwenye kitako cha jiwe.
18 И покрития път за съботата, който бяха построили в къщата, и външния вход за царя, премести в Господния дом, поради асирийския цар.
Kwa heshima ya mfalme wa Ashuru, akaliondoa pia pazia la Sabato lililokuwa limewekwa ndani ya Hekalu, na akaondoa ile njia ya kifalme ya kuingia kwenye Hekalu la Bwana.
19 А останалите дела, които извърши Ахаз, не са ли написани в Книгата на летописите на Юдовите царе?
Matukio mengine ya utawala wa Ahazi na yale aliyoyafanya, je hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
20 И Ахаз заспа с бащите си, в Давидовия град; а вместо него се възцари син му Езекия.
Ahazi akalala na baba zake, naye akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Naye Hezekia mwanawe akawa mfalme baada yake.