< 4 Царе 13 >

1 В двадесет и третата година на Юдовия цар Иоас, Охозиевия син, се възцари Иохаз, Ииуевият син, над Израиля в Самария, и царува седемнадесет години.
Katika mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wa Yoashi mwana wa Ahazia mfalme wa Yuda, Yehoahazi mwana wa Yehu alianza kutawala Israeli katika Samaria, naye akatawala miaka kumi na saba.
2 Той върши зло пред Господа, като последва греховете на Еровоама, Наватовия син, с които направи Израиля да греши; не се остави от тях.
Akafanya maovu machoni pa Bwana kwa kufuata dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, na wala hakuziacha.
3 Затова гневът на Господа пламна против Израиля, и Той постоянно ги предаваше в ръката на сирийския цар Езалия, и в ръката на Венадада, Азаиловия син.
Kwa hiyo hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Israeli na kwa muda mrefu akawaweka chini ya utawala wa Hazaeli mfalme wa Aramu, na Ben-Hadadi mwanawe.
4 Тогава Иоахаз се помоли Господу; и Господ го послуша, защото видя притеснението на Израиля, как сирийският цар ги притесняваше.
Ndipo Yehoahazi akamsihi Bwana rehema, naye Bwana akamsikiliza, kwa maana aliona jinsi mfalme wa Aramu alivyokuwa akiwatesa Israeli vikali.
5 (И Господ даде избевител на Израиля, така щото се отърваха изпод ръката на сирийците, та израилтяните живееха в жилищата си, както по-напред;
Bwana akamtoa mwokozi kwa ajili ya Israeli, nao wakaokoka kutoka kwenye mamlaka ya Aramu. Hivyo Waisraeli wakaishi katika nyumba zao wenyewe kama ilivyokuwa hapo awali.
6 обаче не се оставиха от греховете на дома на Еровоама, с които направи Израиля да греши, а в тях ходиха; и ашерата още стоеше в Самария).
Lakini hawakuziacha dhambi za nyumba ya Yeroboamu, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda, bali wakaendelea kuzitenda. Nguzo ya Ashera pia iliendelea kusimama katika Samaria.
7 Защото сирийският цар не беше оставил на Иоахаза от людете повече от петдесет конници, десет колесници и десек хиляди пешаци; защото сирийският цар беше ги погубил и беше ги направил като стъпкана пръст.
Hapakubaki kitu chochote katika jeshi la Yehoahazi isipokuwa wapanda farasi hamsini, magari kumi ya vita na askari wa miguu elfu kumi, kwa kuwa mfalme wa Aramu alikuwa amewaangamiza hao wengine na kuwafanya kama mavumbi wakati wa kupura nafaka.
8 А останалите дела на Иоахава, и всичко що извърши и юначествата му, не са ли написани в Книгата на летописите на Израилевите царе?
Matukio mengine ya utawala wa Yehoahazi yote aliyoyafanya na mafanikio yake, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
9 И Иоахаз заспа с бящите си, и погребаха го в Самария; а вместо него се възцари син му Иоас.
Yehoahazi akalala pamoja na baba zake, akazikwa huko Samaria. Naye Yehoashi mwanawe akawa mfalme baada yake.
10 В тридесет и седмата година на Юдовия цар Иоас, се възцари Иоас, Иоахазовият син, над Израиля в Самария, и царува шестнадесет години.
Katika mwaka wa thelathini na saba wa utawala wa Yoashi mfalme wa Yuda, Yehoashi mwana wa Yehoahazi alianza kutawala Israeli huko Samaria, naye akatawala miaka kumi na sita.
11 Той върши зло пред Господа; не остави ни от един от греховете на Еровоама, Наватовия син, с които направи Израиля да греши, а в тях ходи.
Alifanya maovu machoni pa Bwana, na hakuacha dhambi yoyote kati ya zile za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, bali aliendelea kuzitenda.
12 А останалите дела на Иоаса, и всичко що извърши и юначеството, с което воюва против Юдовия цар Амасия, не са ли написани в Книгата на летописите на Израилевите царе?
Na kwa matukio mengine ya utawala wa Yehoashi, yote aliyoyafanya na mafanikio yake, pamoja na vita yake dhidi ya Amazia mfalme wa Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
13 И Иоас заспа с бащите си; а на престола му седна Еровоам. А Иоас биде погребан в Самария с Израилевите цари.
Yehoashi akalala pamoja na baba zake, akazikwa Samaria pamoja na wafalme wa Israeli. Yeroboamu akawa mfalme baada yake.
14 В това време Елисей се разболя от болестта, от която умря. И Израилевитят цар слезе при нето та плака над него, като рече: Татко мой! татко мой! колесница Израилева и конница негова!
Wakati huu, Elisha alikuwa anaumwa na ugonjwa ambao baadaye ulimuua. Yehoashi mfalme wa Israeli akashuka kwenda kumwona na kumlilia. Akalia, “Baba yangu! Baba yangu! Magari ya vita ya Israeli na wapanda farasi wake!”
15 А Елисей му каза: Вземи лък и стрели. И той си взе лък и стрели.
Elisha akasema, “Leta upinde na baadhi ya mishale,” naye mfalme akafanya hivyo.
16 Тогава рече на Израилевия цар: Тури ръката си на лъка. И като тури ръката си, Елисей положи ръцете си върху ръцете на царя и рече:
Elisha akamwambia mfalme wa Israeli, “Shika upinde mikononi mwako.” Alipokwisha kuichukua, Elisha akaweka mikono yake juu ya mikono ya mfalme.
17 Отвори источния прозорец. И той го отвори. И рече Елисей: Стреляй. И той устрели. И рече: Стрелата на Господното спасение! да! стрелата на избавлението то сирийците! защото ще поразиш сирийците в Афек докле ги довършиш.
Elisha akasema, “Fungua dirisha la mashariki,” naye akalifungua. Elisha akasema, “Piga mshale!” Naye akapiga mshale. Elisha akasema, “Mshale wa ushindi wa Bwana, mshale wa ushindi juu ya Aramu! Utawaangamiza Waaramu kabisa huko Afeki.”
18 Рече още: Вземи стрелите. И той ги взе. Тогава рече на израилевия цар: Удряй на земята. И той удари три пъти, и престана.
Kisha akasema, “Chukua mishale,” naye mfalme akaichukua. Elisha akamwambia, “Piga ardhi kwa hiyo mishale.” Akaipiga mara tatu, halafu akaacha.
19 А Божият човек се разсърди на него, и рече: Трябваше да удариш пет или шест пъти; тогава щеше да удариш сирийците докле ги довършиш; но сега само три пъти ще поразиш сирийците.
Mtu wa Mungu akamkasirikia na akasema, “Ungepiga chini mara tano au sita, ndipo ungeishinda Aramu na kuiangamiza kabisa. Lakini sasa utaishinda mara tatu tu.”
20 И Елисей умря, и погребаха го. А в следната година някой моавски чети опустошаваха земята.
Elisha akafa, nao wakamzika. Vikosi vya Wamoabu vilikuwa vinashambulia nchi kwa vita kila mwaka wakati wa vuli.
21 И неколцина израилтяни като погребваха един човек, ето, видяха чета: затова хвърлиха човека в гроба на Елисея. А щом стигна човекът та досегна Елисеевите кости, оживя и се изправи на краката си.
Ikawa Waisraeli fulani walipokuwa wanamzika mtu, ghafula wakaona kikosi cha washambuliaji, basi wakaitupa ile maiti ya yule mtu ndani ya kaburi la Elisha. Wakati ile maiti ilipogusa mifupa ya Elisha, yule mtu akafufuka na kusimama kwa miguu yake.
22 И сирийският цар Азаил притесняваше Израиля през всичките дни на Иоахаза.
Hazaeli mfalme wa Aramu aliwatesa Israeli wakati wote wa utawala wa Yehoahazi.
23 Но Господ им показа милост, пожали ги и ги прегледа заради завета Си с Авраама, Исаака и Якова; и отказа да ги изтреби, и не ги отхвърли още от присъствието Си;
Lakini Bwana akawarehemu na akawahurumia, akaonyesha kujishughulisha nao kwa sababu ya Agano lake na Abrahamu, Isaki na Yakobo. Hadi leo, hajawaangamiza wala kuwafukuza mbele zake.
24 защото, като умря сирийският цар Азаил, и вместо него се възцари син му Венадад.
Hazaeli mfalme wa Shamu akafa, naye Ben-Hadadi mwanawe akawa mfalme baada yake.
25 Иоас, Иоахазовият син, взе обратно от ръката на Венадада, Азаиловия син, градовете, които Азаил беше отнел от ръката на баща му Иоахаза във война. Три пъти го порази Иоас, и взе обратно Израилевите градове.
Kisha Yehoashi mwana wa Yehoahazi akateka tena kutoka kwa Ben-Hadadi mwana wa Hazaeli ile miji aliyokuwa ameitwaa kwa vita kutoka kwa baba yake Yehoahazi. Yehoashi alimshinda mara tatu, hivyo akaweza kuiteka tena ile miji ya Waisraeli.

< 4 Царе 13 >