< 1 Царе 27 >
1 Тогава Давид каза в сърцето си: Най-сетне ще загина един ден от Сауловата ръка: няма по-добро за мене отколкото да избягам по-скоро във филистимската земя; тогава Саул ще се отчая и няма вече да ме търси по всичките предели на Израиля; така ще се отърва от ръката му.
Daudi akasema moyoni mwake, “Katika mojawapo ya siku hizi nitaangamizwa kwa mkono wa Sauli. Jambo lililo bora ni kutorokea kwenye nchi ya Wafilisti. Hivyo Sauli atakata tamaa ya kunisaka popote katika Israeli, nami nitakuwa nimeponyoka mkononi mwake.”
2 Затова, Давид стана с шестте стотин мъже, които бяха с него и отиде при гетския цар Анхуса Маоховия син.
Hivyo Daudi akaondoka na hao watu mia sita waliokuwa pamoja naye na kwenda kwa Akishi mwana wa Maoki mfalme wa Gathi.
3 И Давид остана да живее при Анхуса в Гет, той и мъжете му, всеки със семейството си, и Давид с двете си жени, езраелката Ахиноам, и кармилката Авигея, Наваловата жена.
Daudi na watu wake wakakaa huko Gathi pamoja na Akishi. Kila mtu alikuwa pamoja na jamaa yake, naye Daudi pamoja na wakeze wawili: yaani Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili wa Karmeli, mjane wa Nabali.
4 И когато известиха на Саула, че Давид побягнал в Гет, той не го потърси вече.
Sauli alipokuwa ameambiwa kwamba Daudi alikuwa amekimbilia Gathi, hakuendelea kumsaka tena.
5 И Давид каза на Анхуса: Ако съм придобил сега твоето благоволение, нека ми се даде място в някой от полските градове, да живея там: защо да живее слугата ти при тебе в царския град?
Ndipo Daudi akamwambia Akishi, “Kama nimepata kibali machoni pako, unipe sehemu katika mojawapo ya miji katika nchi nikae huko. Kwa nini mtumwa wako akae pamoja nawe katika mji huu wa kifalme?”
6 И в същия ден Анхус му даде Сиклаг; затова, Сиклаг принадлежи на Юдовите царе и до днес.
Hivyo siku hiyo Akishi akampa Daudi mji wa Siklagi, nao Siklagi umekuwa mali ya wafalme wa Yuda tangu wakati huo.
7 А времето, което Давид прекара в земята на филистимците бе една година и четири месеца.
Daudi akaishi katika nchi ya Wafilisti muda wa mwaka mmoja na miezi minne.
8 И Давид и мъжете му възлязоха та нападнаха гесурийците, гезерейците и амаличаните (защото те бяха жителите на земята от старо време), до Сур и дори до Египетската земя.
Basi Daudi na watu wake wakapanda na kuwashambulia Wageshuri, Wagirizi na Waamaleki. (Tangu zamani haya mataifa yalikuwa yameishi kwenye eneo lililotanda kuanzia Telemu katika njia iteremkayo Shuri hadi kufikia nchi ya Misri.)
9 Давид опустошаваше земята, и не оставаше жив ни мъж, ни жена; и грабеше овци, говеда, осли, камили и дрехи; и като се връщаше, дохождаше при Анхуса.
Kila mara Daudi aliposhambulia eneo, hakubakiza hai mwanaume wala mwanamke, lakini alichukua kondoo na ngʼombe, punda na ngamia, na nguo. Kisha akarudi kwa Akishi.
10 И Анхус казваше на Давида: Где нападнахте днес? А Давид казваше: Южната част на Юда, и южната земя на ерамеилците и южната земя на кенейците.
Akishi alipomuuliza, “Je leo umeshambulia wapi?” Daudi humjibu, “Dhidi ya Negebu ya Yuda,” au wakati mwingine husema, “Dhidi ya Negebu ya Yerameeli,” au “Dhidi ya Negebu ya Wakeni.”
11 Давид не оставаше жив ни мъж ни жена, които да бъдат доведени в Гет, понеже си думаше: Да не би да долагат против нас, казвайки: Така направи Давид, и такъв е бил обичаят му през цялото време откак е живял във филистимската земя.
Daudi hakumwacha hai mwanaume au mwanamke ili apate kuletwa Gathi, kwa maana Daudi aliwaza, “Wanaweza kujulisha habari zetu na kusema, ‘Hivi ndivyo alivyofanya Daudi.’” Hii ndiyo ilikuwa desturi yake wakati wote aliishi katika nchi ya Wafilisti.
12 И Анхус вярваше на Давида и си казваше: Той е направил себе си съвсем омразен на людете си Израиля; затова ще ми бъде слуга за винаги.
Akishi akamsadiki Daudi na kuwaza moyoni mwake, akasema, “Daudi amekuwa kitu cha kuchukiza kabisa kwa watu wake, Waisraeli, hivi kwamba atakuwa mtumishi wangu milele.”