< 1 Летописи 7 >

1 А Исахарови синове бяха: Тола, Фуа, Ясув и Симрон, четирима;
Isiakari alikuwa na wana wanne Tola, Pua, Yashubi, na Shimironi.
2 а Толови синове: Озий, Рафаия, Ериил, Ямай, Евсам и Самуил, началници на бащиния им Толов дом, силни и храбри в поколенията им; в дните на Давида, числото им бе двадесет и две хиляди и шестстотин;
Wana wa Tola walikuwa Uzi, Refaia, Yerie, Yamai, Ibisami, Shemueli. Walikua vichwa katika nyumba za baba yao, toka uzao wa Tola na waliorodheshwa kama mashujaa hodari miongoni mwa kizazi chao. Katika siku za Daudi walikua na idadi ya 22, 600.
3 а Озиеви синове: Езраия; и Езраиеви синове; Михаил, Авдия, Иоил и Есия, петима, всички началници.
Mwana wa Uzi alikua Izrahia. Mwana wake alikua Michaeli, Obadia, Yoeli, na Ishia, wote watano walikua viongozi wa ukoo
4 И с тях, според поколенията им, според бащините им домове, имаше полкове войска за бой, тридесет и шест хиляди души; защото имаха много жени и синове.
Pamoja nao walikua na jeshi la watu elfu thelathini na sita kwa mapambano, Kwa mujibu wa orodha zilizomilikiwa na koo za mababu zao, kwa kuwa walikuwa na wake wengi pamoja na wana.
5 А братята им, между всичките Исахарови семейства, силни и храбри, всичките преброени според родословията си, бяха осемдесет и седем хиляди души.
Kaka zao, kabila la Isakari, walikua na wanaume wa vita themanini na saba, kwa mujibu wa orodha zilizomilikiwa na koo za mababu zao.
6 Вениаминови синове: Вела, Вехер и Едиил, трима;
Wana watatu wa Benjamini walikuwa Bela, Beka, na Yediaeli.
7 а Велови синове: Есвон, Озий, Озиил, Еримот и Ирий, петима, началници на бащини домове, силни и храбри, които се преброиха според родословията си; и бяха двадесет и две хиляди и тридесет и четири души;
Wana watano wa Bela walikuwa Ezibono, Uzi, Uzieli, Yerimoti, na Iri. Walikua ni wanajeshi na waanzilishi wa koo. Watu wao walikuwa na idadi ya wanaume wa vita 22, 034, kwa mujibu wa orodha zilizomilikiwa na koo za mababu zao.
8 а Вехерови синове: Земира, Иоас, Илиезер, Елиоинай, Амрий, Еримот, Авия, Анатот и Аламет; всички тия бяха Вехерови синове.
Wana wa Beka walikuwa Zemira, Yoashi, Elieza, Elionai, Omri, Yeremoti, Abiya, Anatoti, na Alemeti. Wote hawa walikuwa wana wake.
9 А броят на родословието им, според поколенията им, бе двадесет хиляди и двеста началници на бащините из домове, силни и храбри.
Orodha ya koo zao ilikua na idadi ya 20, 200 viongozi wa familia na wanaume wa vita.
10 А Едиилов син бе Валаан; а Валаанови синове: Еус, Вениамин, Аод, Ханаана, Зитан, Тарсис и Ахисаар;
Mwana wa Yediaeli alikuwa Bilhani. Wana wa Bilhani walikuwa Yeushi, Benjamini, Ehudi, Kenaana, Zetani, Tarishishi, na Ahishahari.
11 всички тия Едиилови потомци, началници на бащини домове, силни и храбри, бяха седемнадесет хиляди и двеста души, които можеха да излизат на война.
Wote hawa waikuwa wana wa Yediaeli. Waliorodheshwa katika ukoo orodha ilikuwa 17, 200 viongozi na wanaume wa vita imara kwa kazi ya jeshi.
12 А Суфим и Уфим бяха Ирови синове; а Ахиров
(Shupimu na Hupimu walikuwa wana wa Iri, na Hushimu alikuwa mwana wa Aheri.)
13 Нефталимови синове; Ясиил, Гуний, Есер и Селум внуци на Вала.
Wana wa Naftali walikuwa Yazieli, Guni, Yezeri, na Shalumu. Hawa walikuwa wajukuu wa Bilhahi.
14 Манасиеви синове: Асриил, когото му роди жена му; (а наложницата му сирианката роди Махира Галаадовия баща;
Manasse alikua na mtoto wa kiume aliitwa Asrieli, Ambaye suria wake wa Kiaramia alimzalia. Pia alimzaa na Makiri, baba wa Gileadi.
15 а Махир взе за жена сестрата на Уфама и Суфама, и името на сестра им бе Мааха); а името на втория бе Салпаад; и Салпаад роди дъщеря.
Makiri alimchukua mke wake kutoka Hupite na Shupite. Jina la dada yake lilikuwa Maaka. Mwingine wa uzao wa Manasse alikuwa Zalofehadi, ambaye alikuwa na mabinti pekee.
16 А Махировата жена Мааха роди син и нарече го Фарес; а името на брат му бе Сарес, а името на брата му бе Сарес, е синовете му: Улам и Раким;
Maaka mke wa Makiri, alimzaa mwana na alimuita Pereshi. Kaka yake aliitwa Shereshi, na wana wake walikuwa Ulamu na Rakemu.
17 и Уламов син бе Ведан. Тия бяха синовете на Галаада, син на Махира, Манасиевия син.
Mwana wa Ulami alikuwa Bedani. Hawa walikuwa uzao wa Gileadi mwana wa Makiri mwana wa Manase.
18 А сестра му Амолехет роди Исуда, Авиезера и Маала.
Dada wa Gileadi Hamoleketi alimzaa Ishihodi, Abi Ezeri, na Mahila.
19 А Семидови синове бяха Ахиан, Тихем, Ликхий и Аниам.
Wana wa Shemida walikuwa Ahiana, Shekemu, Liki, na Aniamu.
20 А Ефремови синове: Сутала; негов син, Веред; негов син, Тахат; негов син, Елеада; негов син, Тахат;
Uzao wa Efraimu ulikuwa kama ifuatavyo: Efraimu mwana wa Shutela. Shutela mwana wa Beredi. Beredi mwana wa Tahati.
21 негов син, Завад; негов син, Сутала; и Езер и Елеад; а гетските мъже, ги убиха защото бяха слезли да отнемат добитъка им.
Tahati mwana wa Eleada. Eleada mwana wa Shutela. (Eza na Eleadi waliuawa na wanaume wa Gati, wenyeji wa nchi, walipoenda kuiba mifugo yao.
22 А баща им Ефрем жали много дни; и братята му дойдоха да го утешат.
Efraimu baba yao aliomboleza kwa siku nyingi, na kaka zake walikuja kumfariji.
23 Сетне влезе при жена си, която зачна и роди син; и нарече го Верия, по причина на нещастието, което се бе случило в дома му;
Alilala na mkewe. Akapata mimba akamzaa mwana. Efraimu akamuita Beria, kwa sababu maafa yalishakuja nyumbani mwake.
24 (а дъщеря му бе Сеера, която съгради долния и горния Веторон и Узен-сеера);
Binti yake alikuwa Sheera, ambaye alijenga miji juu na chini Beth Horon na Uzzen Sheerah.)
25 и негов син бе Рефа; негови синове, Ресеф и Тела; негов син, Тахан;
Mwana wake alikuwa Rafa. Mwana wa Rafa alikuwa Reshefi. Mwana wa Reshafi alikuwa Tela. Mwana wa Tela alikuwa Tahani.
26 негов син, Ладан; негов син, Амиуд; негов син, Елисама;
Mwana wa Tahani alikuwa Ladani. Mwana wa Ladani alikuwa Amihudi. Mwana wa Amihudi alikuwa Elishama.
27 негов син, Нави; и негов син, Исус.
Mwana wa Elishama alikuwa Nuni. Mwana wa Nuni alikuwa Joshua.
28 А притежанията им и жилищата им бяха Ветил със селата му, и към изток Нааран и към запад Гезер със селата му, и Сихем със селата му, до Газа със селата му;
Mali zao na makazi yao yalikuwa Betheli na yalizungukwa na vijiji. Waliongeza upande wa mashariki hadi Naarani na upande wa magharibi hadi Gezeri na vijiji vyake, na Shekemu na vijiji vyake hadi Aya na vijiji vyake.
29 а, в пределите на Манасиевите потомци, Ветсан със селата му, Таанах със селата му, Магедон със селата му, и Дор със селата му. В тях се заселиха потомците на Иосифа Израилевия син.
Katika mipaka pamoja na Manasse kulikuwa na Beti shani na vijiji vyake, Taanaki na vijiji vyake, Megido na vijiji vyake, na Dori na vijiji vyake. Katika huu mji waliishi uzao wa Josefu mwana wa Israeli.
30 Асирови синове: Емна, Есуа, Есуий и Верия, тяхна сестра Сера;
Wana wa Asha walikuwa Imna, Ishiva, Ishivi, na Beria. Sera alikuwa dada yao.
31 а Вериеви синове бяха: Хевер и Малхиил, който е баща на Вирзавит.
Wana wa Beria walikuwa Heberi na Malchieli, Ambaye alikuwa baba wa Birzaiti.
32 А Хевер роди Яфлета, Сомира и Хотама, и тяхна сестра Суя;
Wana wa Heberi walikuwa Yafeti, Shomer, na Hotamu. dada yao alikuwa Shua.
33 а Яфлетови синове бяха: Фасах, Вимал и Асуат; тия са Яфлетови синове;
Wana wa Yafeti walikuwa Pasach, Bimhali, na Ashivati. hawa walikuwa watoto wa yafeti.
34 а Семирови
shoma, kaka wa Yafeti alikuwa na wana hawa: Roga, Yehuba, Aram.
35 а синовете на брата му Елам: Софа, Емна, Селис и Амал;
Kaka yake Shema, Helemu, alikuwa na wana hawa: Zofa, Imna, Sheleshi na Amali.
36 Софови синове бяха: Суа, Арнефер, Согал, Верий, Емра,
Wana wa Zofa walikuwa Sua, Harinefa, Shua, Beri, IMra,
37 Восор, Од, Сама, Силса, Итран и Веера.
Beza, Hodi, Shamma, Shilsha, Ithrani, na Beera.
38 А Етерови синове бяха: Ефоний, Фасфа и Ара.
Wana wa Yeta walikuwa Jefune, Pispa, na Ara.
39 А Улови синове: Арах, Аниил и Рисия.
Wana wa Ulla walikwa Ara, Hannieli, na Rizia.
40 Всички тия бяха Асирови потомци, началници на бащини домове, отборни, силни и храбри, главни първенци. И броят им, според родословието им, за военна служба, възлизаше на двадесет и шест хиляди мъже.
Hawa wote walikuwa uzao wa Asha. Walikua mababu wa ukoo, viongozi wa familia, wananume wa kipekee, wanaume wa vita, na machifu kati ya viongozi. Kulikuwa na wanaume elfu ishirini na sita walioorodheshwa waliokuwa imara kwa kazi ya jeshi, kwa mujibu wa idadi iliyo orodheshwa.

< 1 Летописи 7 >