< Titus 2 >

1 I wu u ka hla njaaji ilan.
Inakupasa kufundisha itikadi sahihi.
2 Gbi bi ciche lila du mba hi he vutu bey vu sunro be toh jaji ni mi kpakyeme ni itere u Irji.
Wafundishe wazee kuwa na kiasi, wastahivu, wenye busara na wanyofu katika imani, upendo na saburi.
3 Na ki imba be niko be ka vutu bi bana be tere totona du bana so ima u tehuwa na.
Vivyo hivyo, wafundishe wanawake wazee kuwa na mwenendo wa utakatifu, wala wasiwe wasingiziaji au walevi, bali wafundishe yale yaliyo mema,
4 Du ba tsoro imba be tsitsama itere sunko wa balilo.
ili waweze kuwafundisha wanawake vijana kuwa na kiasi, wawapende waume zao na kuwapenda watoto wao,
5 Du mba hi be mlaya mba komba bata tee naki itere Irji a ni bi kerekereme.
wawe waaminifu, watakatifu, wakitunza vyema nyumba zao, wema, watiifu kwa waume zao, ili mtu yeyote asije akalikufuru neno la Mungu.
6 Na ki u ka hla imirize du mba hey be sisuron.
Vivyo hivyo, himiza vijana wawe na kiasi.
7 Ko ni konrime u ka zeren dedeme.
Katika kila jambo uwe kielelezo kwa kutenda mema. Katika mafundisho yako uonyeshe uadilifu, utaratibu,
8 Hla tere be dedema. bewa bana toh itere Irji na Ishan ka temba.
na usemi sahihi usio na lawama, ili wanaokupinga watahayari, wakose neno lolote baya la kusema juu yetu.
9 I miri ko mba wo tere ni tei komba ni mi kogeh mba na sunyu ni mbana.
Wafundishe watumwa kuwatii mabwana zao katika kila jambo, wakijitahidi kuwapendeza wala wasijibizane nao,
10 Du ba na tee yibi na. Mba ka ji kpakyeme U Irji gbahgbah me.
wala wasiwaibie, bali waonyeshe kuwa wanaweza kuaminika kabisa, ili kwa kila namna wayafanye mafundisho ya Mungu Mwokozi wetu yawe ya kuvutia.
11 U imiri Irji ba toh didima wawumba.
Kwa maana neema ya Mungu ambayo inawaokoa wanadamu wote imefunuliwa.
12 Ani hla du keh ka memetee u gbu gblu tagah. (aiōn g165)
Nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia, ili tupate kuishi maisha ya kiasi, ya haki na ya utaua katika ulimwengu huu wa sasa, (aiōn g165)
13 Keh ta zere di ta gbey tee lulu ni ze sunro u ye ivere Irji tee bu.
huku tukilitazamia tumaini lenye baraka na ufunuo wa utukufu wa Mungu wetu Mkuu, aliye Mwokozi wetu Yesu Kristo.
14 Yesu a kpa hla tere u bu ni gbu gblu da ikheu ubu wawu. na ki khi ka hu hla terema.
Ndiye alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe kutoka uovu wote na kujisafishia watu kuwa mali yake Mwenyewe, yaani, wale walio na juhudi katika kutenda mema.
15 U ka tere ni gbe gble de tshoro ba jaji ndah na kpa u tsirina.
Basi wewe fundisha mambo haya. Onya na kukaripia kwa mamlaka yote. Mtu yeyote asikudharau.

< Titus 2 >