< Filimo 1 >

1 Pol, indji u tie ndu Kristi Yesu, ba-mba vayi ma Timoti hi ni Filimon, ikpan mbu ni ikpan tie ndu mbu,
Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu, na ndugu Timotheo kwa Filemoni, mpendwa rafiki yetu na mtenda kazi pamoja nasi,
2 nda hi ni Afia vayi mbu vrenwa, nda hi ni Akipus ikpan u taku mbu, nda hi ni Chochi wa bi rii ni koh mbi.
na kwa Afia dada yetu, na kwa Arkipas askari mwenzetu, na kwa kanisa lile linalokutana nyumbani kwako.
3 Dun Aliheri he ni yi ni sie rji ni Irji, Itti mbu ni Bachi Yesu Kristi.
Neema iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
4 Mi zie bre Irji mu. Mi yo yi ni mi bre mu chachu.
Wakati wote namshukuru Mungu. Ninakutaja katika maombi yangu.
5 Mi woh ye nitu son mba yo'shi ni Irji wa bi he niwu nimi Bachi Yesu mba ni wawu bi hu Irji.
Nimesikia upendo na imani uliyonayo katika Bwana Yesu na kwa ajili ya waumini wote.
6 Mi bre nitu zohn tu-mbi u yo'shi nitu Irji dun vu-kri nitu toh ba kpie bi ndindima wa ahe ni mbu nimi Kristi.
Ninaomba kwamba ushirika wa imani yenu iwe na ufanisi katika ujuzi wa kila jambo jema lililoko kati yetu katika Kristo.
7 U mi ngyri banbran ni vu-suron nitu son kpa mbi, nitu suron bi wa ba hu Irji ba he ngelelen me ni tie me, vayi.
Kwa kuwa nimekuwa na furaha na faraja kwa sababu ya upendo wako, kwa sababu mioyo ya waumini imekuwa ikitulizwa nawe, ndugu.
8 Nika, mi he ni gbengblen suron nimi Kristi wa mi ndi dun wu tie kpe wa-abi dun tie,
Kwa hiyo, ingawa nina ujasiri wote katika Kristo kukuamuru wewe kufanya kile unachoweza kufanya,
9 u mi k'ma bre-wu nitu son u Irji - Ime, Pol, chiche ndji, u zizan mi ndji na ba tro me ni Kristi Yesu.
lakini kwa sababu ya upendo, badala yake nakusihi - mimi, Paulo niliye mzee, na sasa ni mfungwa kwa ajili ya Kristo Yesu.
10 Mi miye u, ivre mu Onisimu, ime mi tima ni brusuna.
Ninakusihi kuhusu mwanangu Onesmo, niliyemzaa katika vifungo vyangu.
11 Ana kpa tie meme niwu, ama zizan ahi vren ndindima niwu u ni me ngame.
Kwa kuwa mwanzoni hakukufaa, lakini sasa anakufaa wewe na mimi.
12 Mi tru'u dun kma ye niwu, a vren u suron mu.
Nimemtuma- yeye ambaye ni wa moyo wangu hasa - kurudi kwako.
13 Mi na son ndi mini kawu zi ni me, don dun tie nimu ndu u'mbi, ka mi ri he ni loh nitu itre Irji.
Nataraji angeendelea kubaki pamoja nami, ili anitumikie badala yako, wakati niwako kifungoni kwa ajili ya injili.
14 Mina son ndi mi tie-kpe hama ni kpa nyime me na. Mina son ndi dun tie ume wa ndi a bi'a dun he nitu gbigbi na u ka he ndi wu tie rji nimi suron ndindima.
Lakini sikutaka kufanya jambo lolote bila ruhusa yako. Nilifanya hivi ili kwamba jambo lolote zuri lisifanyike kwa sababu nilikulazimisha, bali kwa sababu ulipenda mwenyewe kulitenda.
15 U a rjuto ahi nitu wayi mba ba chu-u rju rji niwu ni vi tsaa ntoh, nitu ani la kma ye nda he niwu ni wawu ntoh. (aiōnios g166)
Labda ni sababu alitengwa nawe kwa muda, ilikuwa hivyo ili uwe pamoja naye milele. (aiōnios g166)
16 Ana la tie grahn ngana, ani tie bi zan tie u grahn, immri vayi bi son suron mu. Ahi ndji ndindima nda ri nimi suron mu zan, u gra ma niyi ngame, nimi ikpa yi ni nimi Bachi.
Ili kwamba asiwe tena mtumwa, bali bora zaidi ya mtumwa, kama ndugu mpendwa, hasa kwangu, na zaidi sana kwako, katika mwili na katika Bwana.
17 U toh bi kpa me nji na ikpan tie ndu niyi, kpa-u ngame na wa bi kpa me.
Na hivyo kama wanichukulia mimi mshirika, mpokee kama ambavyo ungenipokea mimi.
18 To a tie-kpe wa isuron mbi na banwu na u nda kpa ihla ni yi, ko ani hi nge a kpa, bla yo ni tu mu.
Lakini kama amekukosea jambo lolote, au unamdai kitu chochote, kidai hicho kutoka kwangu.
19 Ime Pol, mi nha ni'wwo mu: mi hahn yi. Ana ndi bi kma tie ihla ni'wwo mu na.
Mimi Paulo, ninaandika kwa mkono wangu mwenyewe: mimi nitakulipa. Sisemi kwako kwamba nakudai maisha yako hasa.
20 Eih, vayi, tie nimu wayi nimi Bachi; kpa suron mu ku-si nimi Kristi.
Naam ndugu, acha nipate furaha ya Bwana toka kwako: uburudishe moyo wangu katika Kristo.
21 Gbengble suron nitu wo-ttre mbi, misi nha ye niyi. Mi toh ndi bi tie bran zan ikpe wa mi meyi me.
Nikiwa na imani kuhusu utii wako, nakuandikia nikijua kwamba utafanya hata zaidi ya vile ninavyokuomba.
22 Nimi ntoh ki, bika mlah mitra u bitsri tie ni mi, don mi si yo'shi ndi nitu ibre mbi, ba nji me kma ye ni yi.
Wakati huo huo andaa chumba cha wageni kwa ajili yangu, kwa kuwa ninatumaini kupitia maombi yako nitakutembelea hivi karibuni.
23 Epafras, ikpan mu u tie ndu nimi Kristi Yesu, a-ndi dun mi chi yi.
Epafra, mfungwa mwenzangu katika Kristo Yesu anakusalimu,
24 U Markus, Aristachus, Demas, u mba Luka, ba kpukpan tie ndu mu.
na kama afanyavyo Marko, Aristarko, Dema, Luka, watendakazi pamoja nami.
25 Dun Liheri u Bachi Mbu Yesu Kristi hu ni suron mbi. Amin
Neema ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na roho yako. Amina.

< Filimo 1 >