< Filimo 1 >

1 Pol, indji u tie ndu Kristi Yesu, ba-mba vayi ma Timoti hi ni Filimon, ikpan mbu ni ikpan tie ndu mbu,
Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu, pamoja na Timotheo ndugu yetu: Kwa Filemoni rafiki yetu mpendwa na mtendakazi mwenzetu,
2 nda hi ni Afia vayi mbu vrenwa, nda hi ni Akipus ikpan u taku mbu, nda hi ni Chochi wa bi rii ni koh mbi.
kwa dada yetu mpendwa Afia, kwa Arkipo askari mwenzetu na kwa kanisa lile likutanalo nyumbani mwako:
3 Dun Aliheri he ni yi ni sie rji ni Irji, Itti mbu ni Bachi Yesu Kristi.
Neema iwe nanyi na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.
4 Mi zie bre Irji mu. Mi yo yi ni mi bre mu chachu.
Siku zote ninamshukuru Mungu ninapokukumbuka katika maombi yangu,
5 Mi woh ye nitu son mba yo'shi ni Irji wa bi he niwu nimi Bachi Yesu mba ni wawu bi hu Irji.
kwa sababu ninasikia juu ya imani yako katika Bwana Yesu na upendo wako kwa watakatifu wote.
6 Mi bre nitu zohn tu-mbi u yo'shi nitu Irji dun vu-kri nitu toh ba kpie bi ndindima wa ahe ni mbu nimi Kristi.
Naomba utiwe nguvu katika kuishuhudia imani yako, ili upate kuwa na ufahamu mkamilifu juu ya kila kitu chema tulicho nacho ndani ya Kristo.
7 U mi ngyri banbran ni vu-suron nitu son kpa mbi, nitu suron bi wa ba hu Irji ba he ngelelen me ni tie me, vayi.
Upendo wako umenifurahisha mno na kunitia moyo, kwa sababu wewe ndugu, umeiburudisha mioyo ya watakatifu.
8 Nika, mi he ni gbengblen suron nimi Kristi wa mi ndi dun wu tie kpe wa-abi dun tie,
Hata hivyo, ingawa katika Kristo ningeweza kuwa na ujasiri na kukuagiza yale yakupasayo kutenda,
9 u mi k'ma bre-wu nitu son u Irji - Ime, Pol, chiche ndji, u zizan mi ndji na ba tro me ni Kristi Yesu.
lakini ninakuomba kwa upendo, mimi Paulo, mzee na pia sasa nikiwa mfungwa wa Kristo Yesu,
10 Mi miye u, ivre mu Onisimu, ime mi tima ni brusuna.
nakuomba kwa ajili ya mwanangu Onesimo, aliyefanyika mwanangu nilipokuwa kwenye minyororo.
11 Ana kpa tie meme niwu, ama zizan ahi vren ndindima niwu u ni me ngame.
Mwanzoni alikuwa hakufai, lakini sasa anakufaa sana wewe na mimi pia.
12 Mi tru'u dun kma ye niwu, a vren u suron mu.
Namtuma kwako, yeye aliye moyo wangu hasa.
13 Mi na son ndi mini kawu zi ni me, don dun tie nimu ndu u'mbi, ka mi ri he ni loh nitu itre Irji.
Ningependa nikae naye ili ashike nafasi yako ya kunisaidia wakati huu nikiwa kifungoni kwa ajili ya Injili.
14 Mina son ndi mi tie-kpe hama ni kpa nyime me na. Mina son ndi dun tie ume wa ndi a bi'a dun he nitu gbigbi na u ka he ndi wu tie rji nimi suron ndindima.
Lakini sikutaka kufanya lolote bila idhini yako, ili wema wowote uufanyao usiwe wa lazima, bali wa hiari.
15 U a rjuto ahi nitu wayi mba ba chu-u rju rji niwu ni vi tsaa ntoh, nitu ani la kma ye nda he niwu ni wawu ntoh. (aiōnios g166)
Huenda sababu ya yeye kutengwa nawe kwa kitambo kidogo ni ili uwe naye daima. (aiōnios g166)
16 Ana la tie grahn ngana, ani tie bi zan tie u grahn, immri vayi bi son suron mu. Ahi ndji ndindima nda ri nimi suron mu zan, u gra ma niyi ngame, nimi ikpa yi ni nimi Bachi.
Si kama mtumwa, bali bora kuliko mtumwa, kama ndugu mpendwa. Yeye ni mpendwa sana kwangu na hata kwako zaidi, yeye kama mwanadamu na kama ndugu katika Bwana.
17 U toh bi kpa me nji na ikpan tie ndu niyi, kpa-u ngame na wa bi kpa me.
Hivyo kama unanihesabu mimi kuwa mshirika wako, mkaribishe kama vile ungenikaribisha mimi mwenyewe.
18 To a tie-kpe wa isuron mbi na banwu na u nda kpa ihla ni yi, ko ani hi nge a kpa, bla yo ni tu mu.
Kama amekukosea lolote au kama unamdai chochote, nidai mimi.
19 Ime Pol, mi nha ni'wwo mu: mi hahn yi. Ana ndi bi kma tie ihla ni'wwo mu na.
Ni mimi Paulo, ninayeandika waraka huu kwa mkono wangu mwenyewe. Nitakulipa. Sitaji kwamba nakudai hata nafsi yako.
20 Eih, vayi, tie nimu wayi nimi Bachi; kpa suron mu ku-si nimi Kristi.
Ndugu yangu, natamani nipate faida kwako katika Bwana, uuburudishe moyo wangu katika Kristo.
21 Gbengble suron nitu wo-ttre mbi, misi nha ye niyi. Mi toh ndi bi tie bran zan ikpe wa mi meyi me.
Nikiwa na hakika ya utii wako, nakuandikia, nikijua kwamba utafanya hata zaidi ya yale ninayokuomba.
22 Nimi ntoh ki, bika mlah mitra u bitsri tie ni mi, don mi si yo'shi ndi nitu ibre mbi, ba nji me kma ye ni yi.
Jambo moja zaidi: Niandalie chumba cha wageni, kwa kuwa nataraji kurudishwa kwenu kama jibu la maombi yenu.
23 Epafras, ikpan mu u tie ndu nimi Kristi Yesu, a-ndi dun mi chi yi.
Epafra, aliye mfungwa mwenzangu katika Kristo Yesu, anakusalimu.
24 U Markus, Aristachus, Demas, u mba Luka, ba kpukpan tie ndu mu.
Vivyo hivyo Marko, Aristarko, Dema na Luka, watendakazi wenzangu wanakusalimu.
25 Dun Liheri u Bachi Mbu Yesu Kristi hu ni suron mbi. Amin
Neema ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na roho zenu. Amen.

< Filimo 1 >