< Ndu Manzaniba 6 >
1 Zizan ni vi biyi, wa mir ko bi hua, ba si ye ni bran Yahuda wa bi wo helenanci bi nji yiye nitu bi Ibrini yawaba, ahdi bana mla niya mmba be k'po ni zo wa ba yi bawu chachuna.
Basi ikawa katika siku hizo, wakati idadi ya wanafunzi ilipokuwa ikiongezeka sana, palitokea manungʼuniko kati ya Wayahudi wa Kiyunani, dhidi ya Waebrania kwa sababu wajane wao walisahaulika katika mgawanyo wa chakula wa kila siku.
2 don ha'a ba yo kpaa mir ko ba nda tre ndi “Ana bi du ta ka tsro lan tre Irjhi chuwo ni k'ma ki ta ga biri na.
Wale mitume kumi na wawili wakakusanya wanafunzi wote pamoja wakasema, “Haitakuwa vyema sisi kuacha huduma ya neno la Mungu ili kuhudumu mezani.
3 Nitu kima, bika chu, ndi tamgban ni mimbi, indhi wa ndi ba kpanyme ni ba u ba he ni rhuhu mba mre wuto ndindi, ni chuba yo ni ndu yi.
Kwa hiyo ndugu, chagueni watu saba miongoni mwenu, watu wenye sifa njema, waliojawa na Roho Mtakatifu na hekima, ambao tunaweza kuwakabidhi kazi hii,
4 Anita um mbu, ki kri nitu bre mba ndu tsro lan tre Irjhi.
nasi tutatumia muda wetu kuomba na huduma ya neno.”
5 I tre mba a bi wo ni kpaandhi ba wawu. Niki ba chu Istifanus, ndhi wa a shu ni suron gbangban ni nkon Rjhi, mba ni Ruhu Tsatra, u Filibus, Prochorus, Nicanor, Timon, Pamenas, mba Nicolaus ndhi wu Antioch, wa a kpanyme n'dani hu Rjhi bibi wu Yahudawaba.
Yale waliyosema yakawapendeza watu wote, nao wakamchagua Stefano (mtu aliyejawa na imani na Roho Mtakatifu) pamoja na Filipo, Prokoro, Nikanori, Timoni, Parmena na Nikolao, mwongofu kutoka Antiokia.
6 Bi wa ba kpanyme niwu'a ba nji ndhi biyi ye ni shishi ba manzaniba, u ba bre Rjhi nibawu nda sa wo ni tu mba.
Wakawaleta watu hawa mbele ya mitume, nao wakawaombea na kuwawekea mikono juu yao.
7 Niki u tre Rjhi a si bwu kagon U mir ko ni Urishilima ba si bran kpukpome. U Prist gbugbuu ba kpa trea nda hu ni gbengble suron.
Neno la Mungu likazidi kuenea. Idadi ya wanafunzi ikazidi kuongezeka sana katika Yerusalemu hata makuhani wengi wakaitii ile imani.
8 Zizan, Istifanus wa alheni mba gbengble ahe wu suron a si ti kikle kpi ni shishi ndhi ba.
Stefano, akiwa amejaa neema na nguvu za Mungu, alifanya ishara na miujiza mikubwa miongoni mwa watu.
9 Ama Ndhi bari ba rhuki rhi ni haikali'a wa ba yo ndi Haikali wu bi wa ba chubachuwo, rhi ni Cyrenians mba Alexandrians, ni basi rhi ni Cilicia mba Asia. Ndhi biyi ba si a sen nyk ni Istifanus
Hata hivyo, ukainuka upinzani wa watu wa Sinagogi la Watu Huru (kama lilivyokuwa linaitwa), la Wayahudi wa Kirene na wa Iskanderia, na wengine kutoka Kilikia na Asia. Watu hawa wakaanza kupingana na Stefano.
10 Ama bana to kri nda ti kpe zan iri hikima mba iri ruhu wa Istifanus tre'a na. Mle ba lunde le nyu bari ni du ba tre ndi.
Lakini hawakuweza kushindana na hekima yake wala huyo Roho ambaye alisema kwake.
11 ki wo Istifanus a sia tre lan wu mmre Musa mba Rjhi”.
Ndipo kwa siri wakawashawishi watu fulani waseme, “Tumemsikia Stefano akisema maneno ya kufuru dhidi ya Mose na dhidi ya Mungu.”
12 Ba chon ndhiba, ni datibe, bahabi nha (Scribes) mle ba wa Istifanus hi nda jiwu ye ni bi niko ni tra sonmba.
Wakawachochea watu, wazee na walimu wa Sheria, nao wakamkamata Stefano wakamfikisha mbele ya baraza.
13 Ba nji bi che du ba lha ndi ba wa to ni shishinda wa ni tonmba kpiwa ba bla sa niwu'a. Ba tre ndi iguyi na donme ni tre lan meme nitu tsatsra bubuyi mba doka Rjhi na.
Wakaweka mashahidi wa uongo ambao walishuhudia wakisema, “Mtu huyu kamwe haachi kusema dhidi ya mahali hapa patakatifu na dhidi ya Sheria.
14 Nikima, ki wo-u a tre ndi Yesu wu Na'zarat yi, ani zi bubuyi, nda k'ma njo Musa wa a yo nda ka nuta duta ki hu'a sran.
Kwa maana tumemsikia akisema kwamba Yesu wa Nazareti atapaharibu mahali patakatifu na kubadili desturi zote tulizopewa na Mose.”
15 Ko nha wa a son ni tra son bi ninko a sru shishi ni wu nda to shishima a k'ma rhu wu malaika.
Watu wote waliokuwa wameketi katika baraza wakimkazia macho Stefano, wakaona uso wake unangʼaa kama uso wa malaika.