< Ndu Manzaniba 24 >

1 Niwa ivi ton aka hia, ninkon Prist Ananiyas, ni bi chiche, mba indji wu to tre ri, ni nde Tatulus, ba hi niki. Indji biyi ba nji kpe wa ba vu Bulus ni latre ye ni shishi gomna.
Baada ya siku tano, Anania kuhani mkuu, baadhi ya wazee na msemaji mmoja aitwaye Tertulo, wakaenda pale. Watu hawa wameleta mashtaka dhidi ya Paulo kwa gavana.
2 Niwa Bulus a lu kri ni shishi gomna, Tatulus a lu si nhau nda tre ni gomna ndi, “Nitume ki he ni kikle sisron, mba to ko shishi me ani nji mla ti ndindi ni ye ni gbungblu mbu.
Paulo alipo simama mbele ya gavana, Tertulo akaanza kumshitaki na kusema kwa gavana, “kwa sababu yako tuna amani kuu; na kwa maono yako yanaleta mageuzi mazuri katika taifa letu;
3 Nitu ki, ni shuni ngyiri ki kpa wawu kpiwa wuti, kikle wa a bizan wawu, Felix.
basi kwa shukurani yote tunapokea kila kitu ukifanyacho, Wasalam mheshimiwa Feliki.
4 Nitu du mina ziu son gbame na, mi bre lo sron me ni du wo me wu nton fiime.
Lakini nisikuchoshe zaidi, nakusihi unisikilize maneno machache kwa fadhili zako.
5 Kiye to ndi indji yi he to nhran mba wa ani du Yahudawa wawuu kagon gbungblu meme duba ni lukri nitu bi koshishi mba. Ahi ninkon wu biwa ba rjuki nkan nda yo kpamba ndi Nazarin.
Kwa maana tumempata mtu huyu mkorofi, na anasababisha Wayahudi wote kuasi duniani. Tena ni kiongozi wa madhehebu ya Wanazorayo. (Zingatia: Sehemu ya maneno ya mstari huu 24: 6
6 A ta son kpa hekalia ti rji, kima a duta vuu lo zi. / Nha vunvu bi sen bari ba kanha ndi, / Kita son ki gaatre nituma hu kpewa du mbu hla'a /
Na tena alijaribu kulitia hekalu unajisi hivyo tukamkamata., haumo kwenye nakala bora za kale). (Zingatia: Mstari huu
7 Nha bisen bari ba he ni nklan 7 mba mumla wu nklan 8, / 7 I Lysias, Ofisa, a ye ban u ni gbengble rju ni wo mbu, 8 nda yobi nha wu a duba ye ni wu. /
Lisiasi, afisa, alikuja na akamchukua kwa nguvu mikononi mwetu., haumo kwenye nakala bora za maandiko ya kale).
8 Niwa wuta mye Bulus nitu tutre biyi, wu mla to kime nitu kpi biyi wa ki si nhanwu a.
Ukimwuliza Paulo kuhusu mambo haya, hata utaweza kujifunza ni kitu gani tumemshtakia.”
9 Yahudawa ba ngame ba zontu ni nhaw, ndani kpanyime ndi kpewa ba nhanu nituma ba njanji.
Wayahudi nao wakamshtaki Paulo, wakisema kwamba haya mambo yalikuwa kweli.
10 I niwa gomna a tini wo du Bulus tre, Bulus a saa ndi, “Mi mla to ndi wu zi gaatre ni meme mbu wu se gbugbuwu, nitu ki mi ngyiri niwa mi ngla tumu niwu.
Liwali alipompungia mkono ili Paulo aongee, Paulo alijibu, “Ninajua ya kwamba kwa miaka mingi umekua mwamuzi wa taifa hili, na nina furaha kujieleza mwenyewe kwako.
11 Wu to kime ndi ana zan vi wlon don ha na rji niwa mi hon hi bre mba nzu Irji hon ni Urushelima.
Waweza kuhakikisha kuwa hazijapita siku zaidi ya kumi na mbili tangu nilipopanda kwenda kuabudu Yerusalemu.
12 Niwa ba to me nimi hekali, mina sen nyu ni ndrjo na ndina kpa jbu ndji tsitu na, sinagog mba koka ni mi gbua na.
Na waliponikuta katika hekalu, sikubishana na mtu yeyote, na sikufanya fujo katika mkutano, wala katika masinagogi wala ndani ya mji;
13 Bana mla tsro ndi ahi njanji kpe wa ba nhan me zizan nituma na.
na wala hawawezi kuhakikisha kwako mashitaka wanayoyashitaki dhidi yangu.
14 I me bwu nhran niwu ndi, nitu nkon wabayo ndi bi rhuki nkan, ni nkon kima yi mi hu Irji wu ba titi mbu, mi kpanyime ni kpi wawu ni kpi wa a kri tsra ni du mba wa ba anabawa ba nhaa.
Ila nakiri hili kwako, ya kwamba kwa njia ile ambayo wanaiita dhehebu, kwa njia iyo hiyo ninamtumikia Mungu wa baba zetu. Mimi ni mwaminifu kwa yote yaliyoko kwenye sheria na maandiko ya manabii.
15 Mi he ni yo sron riri ni Rji to indji biyi, ndi tashme he, ni bi kri nkon ndindi mba ni bi meme sron.
Nina ujasiri ule ule kwa Mungu ambao hata hao nao wanaungojea, kuja kwa ufufuo wa wafu, kwa wote wenye haki na wasio na haki pia;
16 Niki mi nwo nyu ni na he ni meme mren ni shishi Irji mba Indji na.
na kwa hili, ninafanya kazi ili niwe na dhamira isiyo na hatia mbele za Mungu na mbele ya watu kupitia mambo yote.
17 Zizan, niwa se gbugbuwu ba ka hi, mi ye nu zaka mba ton ni meme mu.
Sasa Baada ya miaka mingi nimekuja kuleta msaada kwa taifa langu na zawadi ya fedha.
18 Niwa mi ti toki, Yahudawa bari, wa ba rhini Asiya, ba ye tome ni bubu ti gan wu ngla ni mi hekali, ana ni jbu indji ko ka ni mi kpagro wu tsitu na.
Nilipofanya hivi, Wayahudi fulani wa Asia wakanikuta ndani ya sherehe ya utakaso ndani ya hekalu, bila kundi la watu wala ghasia.
19 Ani na zan du indji biyi duba he ni shishi me zizan nda nha me, bati na he ni kperi.
Watu hawa ambao imewapasa kuwapo mbele yako sasa hivi na waseme kile walichonacho juu yangu kama wana neno lo lote.
20 Kaandi, du indji biyi me du ba hla kpe meme wa ba ye to nime, niwa mi kri ni shishi son bi ninkon Yahudawa,
Au watu hawa wenyewe na waseme ni kosa gani waliloliona kwangu niliposimama mbele za baraza la kiyahudi;
21 hama nitu kpe ririyi, wa mi kpagro hla niwa mi kri nimi mba, “A he nitu tashme rjini kwu wa mi kri ni tsra nituki ni shishime luwa.”
isipokuwa kwa ajili ya kitu kimoja nilichokisema kwa sauti niliposimama katikati yao, ' ni kwa sababu ya ufufuo wa wafu ninyi mnanihukumu.”'
22 Niki Felix, waana to bi nitu nkon'a, a nzu wo trea hi ko shishi. A tre ndi, “Lysias Komanda, anita grji ye rjini Urushelima, mi ya tre me toh.”
Feliki alikuwa ametaarifiwa vizuri kuhusu njia, na akauahirisha mkutano. Akasema, “Lisia jemedari atakapokuja chini kutoka Yerusalemu nitatoa maamuzi dhidi ya mashitaka yenu.”
23 Niki a mmha sojoi (Centurion) ndi duba nji Bulus hi ri zi, nda duuta fon fu ngyngyu, nda na nzu kpukpan ma du ba ye zoo ni kpi wa ani son na.
Ndipo akamwamuru akida amlinde Paulo, ila awe na nafasi na hata asiwepo mtu wakuwakataza marafiki zake wasimsaidie wala wasimtembelee.
24 Hu gon vi bari, Felix a kma ye mba iwama Drusilla, wa ana bi Yahudawa, nda ton ba ka yo Bulus, i ba wo rhinuwu nitu kri gbangban sron ni Kristi Yesu.
Baada ya siku kadhaa, Feliki akarudi na Drusila mkewe aliyekuwa Myahudi, akatuma kumwita Paulo na akasikiliza toka kwake habari za imani ndani ya Kristo Yesu.
25 I niwa Bulus shlesiya niwu nitu Krista tsra, mla kpa nji, mba gaatre wu ye, Felix a ku ti sissri nda tre ndi, “Hi kpame zizan, Mita he ni nton ni ko shishi mi ton ba hi yowu.”
Ila Paulo alipokuwa akijadiliana naye kuhusu haki, kuwa na kiasi na hukumu itakayokuja, Feliki akapata hofu akajibu, “nenda mbali kwa sasa, ila nikipata muda tena, nitakuita.”
26 Ni nton kima me ata yo sron ka Bulus ni nu nklen, niki a ta gbla you nda ye tre niwu.
Muda uo huo, alitegemea kwamba Paulo atampa fedha kwa hiyo alimwita mara nyingi akaongea naye.
27 Niwa ise ha baka hi, Porcius Festus a hon ni ruron gomna hugon Felix, i Felix a ta son kpa ya nyime ni Yahudawa ba, niki a don Bulus ni lo.
Ila miaka miwili ilipopita, Porkio Festo akawa Liwali baada ya Feliki, ila Feliki alitaka kujipendekeza kwa Wayahudi, hivyo akamwacha Paulo chini ya uangalizi.

< Ndu Manzaniba 24 >