< Ndu Manzaniba 24 >
1 Niwa ivi ton aka hia, ninkon Prist Ananiyas, ni bi chiche, mba indji wu to tre ri, ni nde Tatulus, ba hi niki. Indji biyi ba nji kpe wa ba vu Bulus ni latre ye ni shishi gomna.
Baada ya siku tano, kuhani mkuu Anania akashuka akiwa amefuatana na baadhi ya wazee pamoja na mwanasheria mmoja aitwaye Tertulo, nao wakaleta mashtaka yao dhidi ya Paulo mbele ya mtawala.
2 Niwa Bulus a lu kri ni shishi gomna, Tatulus a lu si nhau nda tre ni gomna ndi, “Nitume ki he ni kikle sisron, mba to ko shishi me ani nji mla ti ndindi ni ye ni gbungblu mbu.
Paulo alipoitwa aingie ndani, Tertulo akaanza kutoa mashtaka akisema, “Mtukufu Feliksi, kwa muda mrefu tumefurahia amani na matengenezo mengi mazuri yamefanywa kwa ajili ya watu hawa kwa sababu ya upeo wako wa kuona mambo ya mbele.
3 Nitu ki, ni shuni ngyiri ki kpa wawu kpiwa wuti, kikle wa a bizan wawu, Felix.
Wakati wote na kila mahali, kwa namna yoyote, mtukufu sana Feliksi, tumeyapokea mambo haya yote kwa shukrani nyingi.
4 Nitu du mina ziu son gbame na, mi bre lo sron me ni du wo me wu nton fiime.
Lakini nisije nikakuchosha zaidi, ningekuomba kwa hisani yako utusikilize kwa kifupi.
5 Kiye to ndi indji yi he to nhran mba wa ani du Yahudawa wawuu kagon gbungblu meme duba ni lukri nitu bi koshishi mba. Ahi ninkon wu biwa ba rjuki nkan nda yo kpamba ndi Nazarin.
“Tumemwona mtu huyu kuwa ni msumbufu, anayechochea ghasia miongoni mwa Wayahudi duniani pote. Yeye ndiye kiongozi wa dhehebu la Wanazarayo,
6 A ta son kpa hekalia ti rji, kima a duta vuu lo zi. / Nha vunvu bi sen bari ba kanha ndi, / Kita son ki gaatre nituma hu kpewa du mbu hla'a /
na hata amejaribu kulinajisi Hekalu, hivyo tukamkamata; [tukataka kumhukumu kufuatana na sheria zetu.
7 Nha bisen bari ba he ni nklan 7 mba mumla wu nklan 8, / 7 I Lysias, Ofisa, a ye ban u ni gbengble rju ni wo mbu, 8 nda yobi nha wu a duba ye ni wu. /
Lakini jemadari Lisia alitujia na nguvu nyingi, akamwondoa mikononi mwetu,
8 Niwa wuta mye Bulus nitu tutre biyi, wu mla to kime nitu kpi biyi wa ki si nhanwu a.
akiwaamuru washtaki wake waje mbele yako: ili] kwa kumchunguza wewe mwenyewe unaweza kujua kutoka kwake mambo yote tunayomshtaki kwayo.”
9 Yahudawa ba ngame ba zontu ni nhaw, ndani kpanyime ndi kpewa ba nhanu nituma ba njanji.
Pia wale Wayahudi wakaunga mkono wakithibitisha kuwa mashtaka yote haya ni kweli.
10 I niwa gomna a tini wo du Bulus tre, Bulus a saa ndi, “Mi mla to ndi wu zi gaatre ni meme mbu wu se gbugbuwu, nitu ki mi ngyiri niwa mi ngla tumu niwu.
Mtawala Feliksi alipompungia Paulo mkono ili ajitetee, yeye akajibu, “Najua kwamba wewe umekuwa hakimu katika taifa hili kwa miaka mingi, hivyo natoa utetezi wangu kwa furaha.
11 Wu to kime ndi ana zan vi wlon don ha na rji niwa mi hon hi bre mba nzu Irji hon ni Urushelima.
Unaweza kuhakikisha kwa urahisi kuwa hazijapita zaidi ya siku kumi na mbili tangu nilipopanda kwenda Yerusalemu kuabudu.
12 Niwa ba to me nimi hekali, mina sen nyu ni ndrjo na ndina kpa jbu ndji tsitu na, sinagog mba koka ni mi gbua na.
Hawa wanaonishtaki hawakunikuta nikibishana na mtu yeyote Hekaluni au kuchochea umati wa watu katika sinagogi au mahali pengine popote mjini.
13 Bana mla tsro ndi ahi njanji kpe wa ba nhan me zizan nituma na.
Wala hawawezi kabisa kukuthibitishia mashtaka haya wanayonishtaki kwayo.
14 I me bwu nhran niwu ndi, nitu nkon wabayo ndi bi rhuki nkan, ni nkon kima yi mi hu Irji wu ba titi mbu, mi kpanyime ni kpi wawu ni kpi wa a kri tsra ni du mba wa ba anabawa ba nhaa.
Lakini, ninakubali kwamba mimi namwabudu Mungu wa baba zetu, mfuasi wa Njia, ile ambayo wao wanaiita dhehebu. Ninaamini kila kitu kinachokubaliana na Sheria na kile kilichoandikwa katika Manabii,
15 Mi he ni yo sron riri ni Rji to indji biyi, ndi tashme he, ni bi kri nkon ndindi mba ni bi meme sron.
nami ninalo tumaini kwa Mungu, ambalo hata wao wenyewe wanalikubali kwamba kutakuwa na ufufuo wa wafu, kwa wenye haki na wasio na haki.
16 Niki mi nwo nyu ni na he ni meme mren ni shishi Irji mba Indji na.
Kwa hiyo ninajitahidi siku zote kuwa na dhamiri safi mbele za Mungu na mbele za wanadamu.
17 Zizan, niwa se gbugbuwu ba ka hi, mi ye nu zaka mba ton ni meme mu.
“Basi, baada ya kutokuwepo kwa miaka mingi nilikuja Yerusalemu ili kuwaletea watu wangu msaada kwa ajili ya maskini na kutoa dhabihu.
18 Niwa mi ti toki, Yahudawa bari, wa ba rhini Asiya, ba ye tome ni bubu ti gan wu ngla ni mi hekali, ana ni jbu indji ko ka ni mi kpagro wu tsitu na.
Nilikuwa nimeshatakaswa kwa taratibu za kiibada waliponikuta Hekaluni nikifanya mambo haya. Hapakuwa na umati wa watu, pamoja nami wala aliyehusika kwenye fujo yoyote.
19 Ani na zan du indji biyi duba he ni shishi me zizan nda nha me, bati na he ni kperi.
Lakini kulikuwa na baadhi ya Wayahudi kutoka Asia, ambao wangelazimika wawepo hapa mbele yako ili watoe mashtaka kama wanalo jambo lolote dhidi yangu.
20 Kaandi, du indji biyi me du ba hla kpe meme wa ba ye to nime, niwa mi kri ni shishi son bi ninkon Yahudawa,
Au, watu hawa walioko hapa waseme ni uhalifu gani walioniona nao waliponisimamisha mbele ya baraza,
21 hama nitu kpe ririyi, wa mi kpagro hla niwa mi kri nimi mba, “A he nitu tashme rjini kwu wa mi kri ni tsra nituki ni shishime luwa.”
isipokuwa ni kuhusu jambo hili moja nililopiga kelele mbele yao kwamba, ‘Mimi nashtakiwa mbele yenu leo kwa sababu ya ufufuo wa wafu.’”
22 Niki Felix, waana to bi nitu nkon'a, a nzu wo trea hi ko shishi. A tre ndi, “Lysias Komanda, anita grji ye rjini Urushelima, mi ya tre me toh.”
Basi Feliksi ambaye alikuwa anafahamu vizuri habari za Njia ile, akaahirisha shauri lile kwa maelezo yake akisema, “Wakati jemadari Lisia atakapoteremka huku, nitaamua shauri lako.”
23 Niki a mmha sojoi (Centurion) ndi duba nji Bulus hi ri zi, nda duuta fon fu ngyngyu, nda na nzu kpukpan ma du ba ye zoo ni kpi wa ani son na.
Ndipo akaamuru kiongozi wa askari amweke chini ya ulinzi lakini ampe uhuru na kuwaruhusu rafiki zake wamhudumie.
24 Hu gon vi bari, Felix a kma ye mba iwama Drusilla, wa ana bi Yahudawa, nda ton ba ka yo Bulus, i ba wo rhinuwu nitu kri gbangban sron ni Kristi Yesu.
Baada ya siku kadhaa, Feliksi alikuja pamoja na Drusila mkewe, ambaye alikuwa Myahudi. Alituma aitiwe Paulo, naye akamsikiliza alipokuwa akinena juu ya imani katika Kristo Yesu.
25 I niwa Bulus shlesiya niwu nitu Krista tsra, mla kpa nji, mba gaatre wu ye, Felix a ku ti sissri nda tre ndi, “Hi kpame zizan, Mita he ni nton ni ko shishi mi ton ba hi yowu.”
Naye Paulo alipokuwa akinena juu ya haki, kuwa na kiasi na juu ya hukumu ijayo, Feliksi aliingiwa na hofu na kusema, “Hiyo yatosha sasa! Waweza kuondoka. Nitakapokuwa na wasaa nitakuita.”
26 Ni nton kima me ata yo sron ka Bulus ni nu nklen, niki a ta gbla you nda ye tre niwu.
Wakati huo Feliksi alitazamia kwamba Paulo angempa rushwa. Hivyo akawa anamwita mara kwa mara na kuzungumza naye.
27 Niwa ise ha baka hi, Porcius Festus a hon ni ruron gomna hugon Felix, i Felix a ta son kpa ya nyime ni Yahudawa ba, niki a don Bulus ni lo.
Baada ya miaka miwili kupita, Porkio Festo akaingia kwenye utawala mahali pa Feliksi, lakini kwa kuwa Feliksi alitaka kuwapendeza Wayahudi, akamwacha Paulo gerezani.