< Yak'ob 3 >
1 Ti eshuwotso! noo danifuwotsi wottsuwots iki bogts angsho node'k'etwok'o itdantsotse ititse ayuwots danifuwotsi wotk'ayine.
Ndugu zangu, siyo wengi wenu mnapaswa kuwa walimu, mkijua kwamba tutapokea hukumu kubwa zaidi.
2 No noúnets aayote nosheeliri, b́ noon keew keewon darrawo bí bí ats jamo kordek' falituwo ik jag bí atse daatseraw ashe.
Kwa kuwa wote tunakosea katika njia nyingi. Kama yeyote huwa hajikwai katika maneno yake, huyo ni mtu mkamilifu, aweza kudhibiti mwili wake wote pia.
3 Farsho noosh bí azazetwok'o b́ nonots lugamo nogedeti, mank'oon bíats jamó no shuntsok jiishituwone.
Sasa kama tunaweka lijamu za farasi katika vinywa vyao wanatutii, na tunaweza kuigeuza miili yao yote.
4 Markabo awuk'o een b́ wotiyaloru jong angon b́ jookewor, markab jokirwo bir múk'naún b́ shuntso maants b́ jiishiti.
Tambua pia kwamba meli, ingawa ni kubwa na husukumwa na upepo mkali, zinaongozwa kwa usukani mdogo sana kwenda popote anakotaka nahodha.
5 Mank'owere alberu muk'na'a atsi kayu wotefetsat een een keewwotsn bit'iri, een gemo b́mis'fo taw muk'na'úne.
Vivyo hivyo, ulimi ni kiungo kidogo cha mwili, lakini hujisifia makuu sana. Angalia msitu mkubwa unavyoweza kuwashwa kwa cheche ndogo ya moto!
6 Alberunu tawok'oyiye. Alberu noatsi kaywotsitse daatseru gond datsuniye. Ats jamats aldetstsonat noats jamo bi awaashiti. Gahanemitse keshiru tawok'o nobee jamo bmitsiri. (Geenna )
Ulimi pia ni moto, ni ulimwengu wa uovu, umewekwa miongoni mwa viungo vya mwili wetu, ambao hunajisi mwili wote na huiweka juu ya moto njia ya maisha, na wenyewe kuchomwa moto wa kuzimu. (Geenna )
7 Datsatsi s'otswotsnat kafuwots, datsatse getseyirwotsnat aats k'arotse sha'iru azeets jamwots ashon sezewo falitune, andoor sezeerne.
Kila aina ya mnyama wa polini, ndege, kitambaacho na kiumbe cha baharini kinadhibitiwa na wanadamu.
8 Wotowa bako albero sezo falituwo konuwor aaliye, úd'it marziyo bín s'eentsonat kashdek'o biitse deshaw gond keewniye.
lakini hakuna mwanadamu hata mmoja ambaye anaweza kudhibiti ulimi; ni uovu usiotulia, umejaa sumu ya kufisha.
9 Bín no nihi Ik'o noúdiri, mank'owere bín Ik'i aron azeets ashuwotsi noc'ashiri.
Kwa ulimi twamtukuza Bwana na Baba yetu, na kwa huo twawalaani watu ambao wameumbwa kwa mfano wa Mungu.
10 Noon ikotse údonat c'ashon keshirune, tieshuwotso! han b́ woto geyiratse.
Katika kinywa hichohicho husema maneno ya baraka na laana. Ndugu zangu mambo haya hayapaswi kuwa.
11 Aats t'up' ikotse úshosh wotit shaaw aatsonat s'aam aatson t'up'osh falituwa?
Je, kisima kimoja huweza kutoa maji matamu na machungu?
12 Ti eshuwotso! belesi mito woyira eteets mit shúwo shuwosh falatse. Wee woyini bos'o Belesi shuwo shuwosh falatse? Mank'o s'aam aatsotse shaaw aatso keyatse.
Ndugu zangu, Je, mti wa mtini unaweza kuzaa matunda ya mzeituni, au mzabibu unazaa matunda ya mtini? Wala chemchemi ya maji chumvi haitoi maji yasio na chumvi.
13 It dagotsere dan teleefonat t'iwints detsts asho kone? Dani teleefonat b́tooko dashan detson b́fiintsfino b́sheng beyon kitsuwe.
Ni nani miongoni mwenu aliye na hekima na ufahamu? Hebu mtu huyo na aoneshe maisha mema katika kazi zake kwa unyenyekevu utokanao na hekima.
14 Wotowabako s'aamts okooronat b́ took shuno it nibots fa'e wotiyal it'k'ayere, arikeewatsowere kootk'ayere.
Lakini kama mnao wivu mkali na nia ya ubinafsi mioyoni mwenu, msijivune na kusema uongo mkiupinga ukweli.
15 Dani teleefan b́ daatseti, datsuwatse meetsatse, Dablosokna bako Ik'onaaliye.
Hii siyo hekima ile ishukayo kutoka juu, lakini badala yake ni ya kidunia, si ya kiroho, na ni ya kipepo.
16 Okooronat took shunon bobeyokoke dimbironat gond fin jamwots beetune.
Kwa kuwa palipo na wivu na ubinafsi upo, kuna vurugu na kila matendo maovu
17 Wotowaere Ik'oke daatset dani teleefo shin shino s'ayine, manats dabrnuwere jeenon s'eents, doo, maneyo, mhretiyo, sheeng shuwo bín s'eentso, bogabogshoonat gitalberetsi woto biitse deshawoniye.
Lakini hekima itokayo juu, kwanza ni safi, kisha kupenda amani, upole na ukarimu, yenye kujaa rehema na matunda mema, bila kupendelea watu fulani, na kweli.
18 Jeen be shunts ashuwots jeeno shoohr kááwi shuwo kakuwitune.
Na tunda la haki hupandwa katika amani kwa wale ambao wanatenda mambo ya amani.