< लूका 14 >
1 फिरी यीशु सब्ते दे रोजे फरीसियां दे सरदारां चे कुसकी दे घरे रोटी खाणां खाणे तांई गिया: कने सै यीशु जो ढंगे ने ताका दे थे की कोई गलती तोपी सकन।
Ikawa siku moja Yesu alipokuwa amekwenda kula chakula kwa mmoja wa viongozi wa Mafarisayo siku ya Sabato, watu walikuwa wakimchunguza kwa bidii.
2 ओथु इक माणु था, जिसदे हथ कने पैर सूजी गियो थे।
Papo hapo mbele yake palikuwa na mtu mmoja mwenye ugonjwa wa kuvimba mwili.
3 इसा गल्ला पर यीशुऐ व्यवस्था जो सिखाणे बालयां कने फरीसियों ने बोलया, “क्या सब्ते दे रोजे लोकां जो ठीक करणे दी अनुमति व्यवस्था च है, की नी है?”
Yesu akawauliza wale Mafarisayo na walimu wa sheria, “Je, ni halali kuponya watu siku ya Sabato au la?”
4 पर सै चुपचाप ही रे। तालू यीशुऐ उस पर हथ रखीकरी ठीक किता, कने जाणा दिता।
Wakakaa kimya. Hivyo Yesu akamshika yule mgonjwa mkono na kumponya, akamruhusu aende zake.
5 कने उना जो बोलया, “मन्नी लिया कि तुसां चे कुसकी दा जागत या दांद सब्ते दे रोजे खुऐ च पेई जा कने उसयो उस रोजे झट बाहर ना कडे?”
Kisha akawauliza, “Kama mmoja wenu angekuwa na mtoto au ngʼombe wake aliyetumbukia katika kisima siku ya Sabato, je, hamtamvuta mara moja na kumtoa?”
6 सै इना गल्लां दा कोई भी जबाब नी देई सके।
Nao hawakuwa na la kusema.
7 तालू उनी दिखया, की सदयो लोक कियां सै जगा चुणी लेंदे जिथू सबते खास लोक बोंदे न, तां यीशुऐ उना जो इक कहाणी सुणाई करी उना ने बोलया,
Alipoona jinsi wageni walivyokuwa wanachagua mahali pa heshima wakati wa kula, akawaambia mfano huu:
8 जालू कोई तिजो बियाये दिया धामा च सदगा, तां तुसां उना खास आसना च मत बोंदा, कुथकी इयां ना हो की उनी तिजो ला भी बड़े खास बंदे जो न्युंद्र दितियो हो।
“Mtu akikualika arusini, usikae mahali pa mgeni wa heshima kwa kuwa inawezekana amealikwa mtu mheshimiwa kuliko wewe.
9 कने जिनी तिजो कने उसयो दोनो जो न्युंद्र दितियो है, सै आई करी तिजो ने बोले, की इसयो जगा दे, तालू तिजो शरमिंदा होईकरी सारयां ला पिच्छे बालिया जगा च बोणा पोऐ।
Kama mkifanya hivyo yule aliyewaalika ninyi wawili atakuja na kukuambia, ‘Mpishe huyu mtu kiti chako.’ Ndipo kwa aibu utalazimika kukaa katika nafasi ya chini kabisa.
10 पर जालू तिजो सदगे, तां सारयां ला पिच्छे बालिया जगा जाई करी बेई जा, की जालू सै, जिनी तिजो सदया हे सै ओऐ, कने तिजो ने बोले की हे मित्र, अग्गे जाई करी खास बाली जगा च बैठ; तालू तेरे सोगी बोंणे बालयां दे सामणे तेरी बड़ाई होंणी।
Badala yake, unapoalikwa, chagua nafasi ya chini, ili yule mwenyeji wako atakapokuona atakuja na kukuambia, ‘Rafiki yangu, nenda kwenye nafasi iliyo bora zaidi.’ Kwa jinsi hii utakuwa umepewa heshima mbele ya wageni wenzako wote.
11 “क्योंकि जड़ा कोई अपणे आपे जो बडा महान बणांगा, उसयो छोटा किता जाणा; कने जड़ा कोई अपणे आपे जो छोटा बणांगा, सै सबते महान कितया जाणा।”
Kwa maana kila mtu ajikwezaye atashushwa, naye ajishushaye atakwezwa.”
12 तालू यीशुऐ अपणे न्युंद्र देणेबाले फरीसियो जो भी बोलया, “जालू तू दिने दा या राती दा खाणां खांगा, तां अपणे दोस्तां या भाईयां या रिश्तेदारां या अमीर पड़ोसियां जो मत सददा, की इयां ना हो, की सै भी तिजो सदन, कने जड़ा तू खाणा खुआया उदा बदला होई जाऐ।”
Kisha Yesu akamwambia yule aliyewaalika, “Uandaapo karamu ya chakula cha mchana au cha jioni, usialike rafiki zako au ndugu zako au jamaa zako au majirani zako walio matajiri tu. Ukifanya hivyo, wao nao wanaweza kukualika kwao, nawe ukawa umelipwa kile ulichofanya na kupata thawabu yako.
13 “पर जालू तू रोटी खाऐ, तां गरीबां जो, लंगड़यां जो कने अन्नयां जो सदी लियां।
Bali ufanyapo karamu, waalike maskini, vilema na vipofu,
14 तालू तू धन्य होणा, क्योंकि उना बाल तिजो देंणे तांई कुछ नी है, पर जालू धर्मी लोकां दे फिरी जिन्दा होई जाणा तालू परमेश्वरे तुहांजो इदा इनाम देणा।”
nawe utabarikiwa kwa sababu hawa hawana uwezo wa kukulipa. Mungu atakulipa wakati wa ufufuo wa wenye haki.”
15 उदे सोगी रोटी खाणे बालयां चे इकी ऐ गल्लां सुणिकरी उसयो बोलया, “धन्य है सै, जड़ा परमेश्वरे दे राज्य दिया धाम च शामिल होंगा।”
Mmoja wa wale waliokuwa pamoja naye mezani aliposikia hivi akamwambia Yesu, “Amebarikiwa mtu yule atakayekula katika karamu ya Ufalme wa Mungu!”
16 उनी उसयो बोलया, कुनकी माणुऐ बड़ी बडी धाम दिती कने मतयां जो सदया।
Yesu akamjibu, “Mtu mmoja alikuwa anaandaa karamu kubwa, akaalika watu wengi.
17 जालू खाणां तैयार होई गिया, तां उनी अपणे नोकरे जो भेजया कि जिना जो नियुंद्र दितियो उना लोकां जो बोली ओआ, की ओआ, खाणां तैयार है।
Wakati wa karamu ulipofika, akamtuma mtumishi wake akawaambie wale walioalikwa, ‘Karibuni, kila kitu ki tayari sasa.’
18 पर सै सारे दे सारे माफी मंगणा लग्गे, पेहले माणुऐ उसला बोलया, मैं खेतर खरीदया है कने जरूरी है की मैं उसयो दिखें; मैं तिजो ने बिनती करदा है, की मिंजो माफ करी दे।
“Lakini wote, kila mmoja, wakaanza kutoa udhuru: Wa kwanza akasema, ‘Nimenunua shamba, lazima niende kuliona. Tafadhali niwie radhi.’
19 दूऐ माणुऐ बोलया, मैं पंज जोड़ी दांद खरिदयो न, कने उना जो परखणा जाणा है; मैं तिजो ने बिनती करदा है की मिंजो माफ करी दे।
“Mwingine akasema, ‘Ndipo tu nimenunua jozi tano za ngʼombe wa kulimia, nami ninakwenda kuwajaribu, tafadhali niwie radhi.’
20 इकी होरनी बोलया, की मैं बियाह कितया है, इस तांई मैं नी आई सकदा है।
Naye mwingine akasema, ‘Nimeoa mke, kwa hiyo siwezi kuja.’
21 उनी सेवके आई करी अपणे मालिके ने ऐ गल्ल सुणाई। तालू घरे दे मालिके गुस्से च आई करी बोलया, शेहरे दे बजारां कने गलियां च जाई करी झट कंगालां, टुंडे, लंगड़यां कने अन्नयां जो ऐथू लेई ओआ।
“Yule mtumishi akarudi, akampa bwana wake taarifa. Ndipo yule mwenye nyumba akakasirika, akamwagiza yule mtumishi wake, akisema, ‘Nenda upesi kwenye mitaa na vichochoro vya mjini uwalete maskini, vilema, vipofu na viwete.’
22 सेवके फिरी बोलया, हे मालिक, जियां तू बोलया था, तियां ही कितया है; फिरी भी जगा है।
“Yule mtumishi akamwambia, ‘Bwana, yale uliyoniagiza nimefanya, lakini bado ipo nafasi.’
23 “मालिके सेवके ने बोलया, सड़कां कने बागां च जाई करी लोकां जो मजबूर करी के लेई आऐ ताकि मेरा घर भरुई जा।
“Ndipo yule bwana akamwambia mtumishi wake, ‘Nenda kwenye barabara na vijia vilivyoko nje ya mji na uwalazimishe watu waingie ili nyumba yangu ipate kujaa.
24 क्योंकि मैं तुसां ने बोलदा है, की पेहले सदयो होए लोकां चे कोई भी मेरिया रोटिया जो नी चखगा।”
Kwa maana nawaambia, hakuna hata mmoja wa wale walioalikwa atakayeionja karamu yangu.’”
25 कने जालू मती भीड़ यीशुऐ सोगी चलियो थी, तां उनी पिच्छे मुड़ी करी उसला बोलया।
Umati mkubwa wa watu ulikuwa ukisafiri pamoja na Yesu, naye akageuka, akawaambia,
26 “जड़े लोक मेरे बाल ओंदे न, सै तालू दीकर मेरे चेले नी बणी सकदे, जालू दिकर अपणे माता-पिता कने घरे बाली कने बच्चे कने भाई बेंहण कने अपणे आपे ला जादा प्यारा मिंजो ने नी करदे।”
“Mtu yeyote anayekuja kwangu hawezi kuwa mwanafunzi wangu kama hatanipenda mimi zaidi ya baba yake na mama yake, mke wake na watoto wake, ndugu zake na dada zake, naam, hata maisha yake mwenyewe.
27 जड़ा मेरिया बजा ला दुख सेहन कने मरणे तांई तैयार नही है, सै भी मेरा चेला बणने दे लायक नही है।
Yeyote asiyeuchukua msalaba wake na kunifuata hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
28 “अगर तुसां चे कोई इक बड़ा बड्डा घर बणाणा चांदा हो, तां उनी सबते पेहले बेईकरी इसा गल्ला दा हिसाब लाणा की इसयो बणाणे च कितणा खर्चा ओणा, कने दिखणा की इसयो पूरा करणे तांई पूरा पैसा है की नी।”
“Ni nani miongoni mwenu ambaye kama anataka kujenga nyumba, hakai kwanza chini na kufanya makisio ya gharama aone kama ana fedha za kutosha kukamilisha?
29 अगर उनी इयां नी किता, तां उनी जालू नियां पाई करी घरे जो पूरा तैयार नी करी सकणा, तां सारे दिखणे बाले ऐ बोलिकरी उदा मजाक उड़ाणा,
La sivyo, akiisha kuweka msingi, naye akiwa hana uwezo wa kuikamilisha, wote waionao wataanza kumdhihaki,
30 की इनी माणुऐ घर बणाणा तां शुरू किता, पर पूरा बणाई नी सकया?
wakisema, ‘Mtu huyu alianza kujenga lakini hakuweza kukamilisha.’
31 “अगर इक राजा दस हजार माणुआं जो लेईकरी दुऐ राजे ने लड़ना चलया हो, जड़ा बी हजार माणुआं जो लेईकरी उस पर हमला करणा ओआ दा हो, तां सबते पेहले बेईकरी इसा गल्ला पर बिचार करे की जड़ा बी हजार लेईकरी मिंजो ने लड़ना ओआ दा है, क्या मैं उदा सामणा करी सकदा है की नी?”
“Au ni mfalme gani atokaye kwenda kupigana vita na mfalme mwingine, ambaye hakai chini kwanza na kufikiri iwapo akiwa na jeshi la watu 10,000 ataweza kupigana na yule anayekuja na jeshi la watu 20,000?
32 नितां उदे दूर रेंदे ही, उसला संधी करणे दे बारे च गल्ल बात करणे तांई सै दूतां जो भेजे।
Kama hawezi, basi wakati yule mwingine akiwa bado yuko mbali, yeye hutuma ujumbe wa watu na kuomba masharti ya amani.
33 इयां ही तुसां चे जड़ा कोई अपणा सब कुछ छडी दे, सै ही मेरा चेला होई सकदा है।
Vivyo hivyo, yeyote miongoni mwenu ambaye hawezi kuacha vyote alivyo navyo, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
34 लूँण तां खरा होंदा है, पर अगर उदा स्वाद बिगड़ी जा, तां उदा स्वाद कियां नमकीन करणा?
“Chumvi ni nzuri, lakini chumvi ikiwa imepoteza ladha yake, itafanywaje ili iweze kukolea tena?
35 “सै तां ना जमिना दे ना तां खादी दे कम्मे ओंदा है: उसयो तां लोक बाहर फेंकी दिन्दे न। जिस बाल सुणने तांई कन्न न सै ध्यान लाईकरी गल्ला जो सुणे, कने इसा गल्ला जो समझी ले।”
Haifai ardhi wala kwa lundo la mbolea, bali hutupwa nje. “Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”