< Gesami Hea:su 69 >

1 Gode! Na gaga: ma! Hano da heda: le, na galogoalisi dagoi.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi.” Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, niokoe, kwa maana maji yamenifika shingoni.
2 Na da fafu lugudu amoga magufasa. Amogai da osobo ga: nasi da hame gala. Na da hano lugudu amoga gala. Hano gafului da na fabeba: le, na da gela sa: imu gadenei ba: sa.
Ninazama kwenye vilindi vya matope, pasipo mahali pa kukanyaga, Nimefika kwenye maji makuu, mafuriko yamenigharikisha.
3 Na da fidima: ne ha: giwane wele sia: nanebeba: le, gufia: i galebe. Na da: gisu da sesa. Na da Dia fidisu ba: musa: hogolalebeba: le, na si da seselei galebe.
Nimechoka kwa kuomba msaada, koo langu limekauka. Macho yangu yanafifia, nikimtafuta Mungu wangu.
4 Dunu amo da nama bai hamedene ougisa, ilia idi da na dialuma hinabo idi amo baligisa. Nama ha lai dunu da na wadela: musa: bagadewane ogogosa. Ilia da gasa bagade amola na fane legemusa: hanai gala. Ilia da liligi amo na hame wamolai, amo nama samogele lai dagoi.
Wale wanaonichukia bila sababu ni wengi kuliko nywele za kichwa changu; wengi ni adui kwangu bila sababu, wale wanaotafuta kuniangamiza. Ninalazimishwa kurudisha kitu ambacho sikuiba.
5 Gode! Na wadela: i hou da Dima hame wamolegesa. Dia dawa: ! Na da gagaoui hamoi dagoi.
Ee Mungu, wewe unajua upumbavu wangu, wala hatia yangu haikufichika kwako.
6 Ouligisudafa Hina Gode Bagadedafa! Na da dunu amo da Dima dafawaneyale dawa: be, ilima na da gogosiasu mae gaguli misa: ma! Isala: ili Gode! Na da dunu amo da Dima nodone sia: ne gadosa, ilima na da gogosiasu mae gaguli misa: ma!
Ee Bwana, ewe Bwana Mwenye Nguvu Zote, wakutumainio wasiaibishwe kwa ajili yangu; wakutafutao wasifedheheshwe kwa ajili yangu, Ee Mungu wa Israeli.
7 Na da Dima fa: no bobogebeba: le, nama ha lai da nama gadebeba: le, na da gogosiasu amoga dedeboi dagoi.
Kwa maana nimestahimili dharau kwa ajili yako, aibu imefunika uso wangu.
8 Na nolalalia ilia siga, na da sofe misi dunu agoai ba: sa. Amola na sosogo fi da na ga fi misi dunu agoai ba: sa.
Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, mgeni kwa wana wa mama yangu mwenyewe.
9 Na da Dia Debolo Diasuga asigi hou da na dogo ganodini lalu agoane nesa. Dunu da Dima gadele sia: sea, na da Dima madelagiba: le, ilia da defele nama gadesa.
Kwa kuwa wivu wa nyumba yako unanila, matukano ya wale wanaokutukana yameniangukia.
10 Na da na hou asaboma: ne, ha: i mae nawene esala. Amola eno dunu da nama gadesa.
Ninapolia na kufunga, lazima nivumilie matusi.
11 Na da disa eboboi abula amoga gaga: sa. Amola ilia da na ba: le oufesega: sa.
Ninapovaa nguo ya gunia, watu hunidharau.
12 Ilia da logo bega: naba: le sia: daha. Amola adini ba: i dunu da nama oufesega: ne, gesami ge lasa.
Wale wanaoketi mlangoni wananisimanga, nimekuwa wimbo wa walevi.
13 Be Hina Gode! Na da amo mae dawa: le Dima sia: ne gadomu. Dia eso ilegei amoga nama dabe adole ima. Dia da osobo bagade dunu ilima asigi bagadeba: le, nama adole ima. Bai Dia gaga: ma: ne ilegele sia: i, amo Di da hame gogolesa.
Lakini Ee Bwana, ninakuomba, kwa wakati ukupendezao; katika upendo wako mkuu, Ee Mungu, unijibu kwa wokovu wako wa hakika.
14 Na da fafu amoga bosona dasa: besa: le, na gaga: ma! Nama ha lai dunu, ilia na fasa: besa: le, na gaga: ma! Na da hano lugudu amo ganodini magufasa: besa: le, na gaga: ma!
Uniokoe katika matope, usiniache nizame; niokoe na hao wanichukiao, kutoka kwenye vilindi vya maji.
15 Hano heda: i da na dedebole fane legesa: besa: le, na gaga: ma! Na da hano wayabo bagade lugudu amoga magufale gela dasa: besa: le, na gaga: ma! Na da bogoi uli dogoiga dasa: besa: le, na gaga: ma!
Usiache mafuriko yanigharikishe au vilindi vinimeze, au shimo lifumbe kinywa chake juu yangu.
16 Hina Gode! Dia da mae fisili, noga: idafa asigi hou dawa: Amaiba: le, na sia: ne gadosu amoma adole ima. Nama ba: le guda: ma!
Ee Bwana, unijibu, kwa wema wa upendo wako; kwa huruma zako nyingi unigeukie.
17 Na da Dia hawa: hamosu dunu. Nama mae wamoaligima! Na da bidi hamosu bagadewane ba: sa. Wahadafa nama dabe adole ima.
Usimfiche mtumishi wako uso wako, uharakishe kunijibu, kwa sababu niko katika shida.
18 Nama misini, na gaga: ma! Nama ha lai da na hasalasa: besa: le, na gaga: ma!
Njoo karibu uniokoe, nikomboe kwa sababu ya adui zangu.
19 Nama ha lai dunu ilia da nama gadesa amola na gogosiama: ne hamosa. Dia da nama ha lai dunu huluane ba: lala.
Unajua jinsi ninavyodharauliwa, kufedheheshwa na kuaibishwa, adui zangu wote unawajua.
20 Ilia da nama bagadewane gadebeba: le, na da gala: la sa: i agoai ba: sa. Na da heawi agoai diala. Na da eno dunu ilia da nama asigimu, na da dawa: i. Be ilia da nama hame asigi galu. Ilia da na dogo denesima: ne, na da hanai galu. Be agoane hame ba: i.
Dharau zimenivunja moyo na nimekata tamaa, nimetafuta wa kunihurumia, lakini sikumpata, wa kunituliza, lakini sikumpata.
21 Na da ha: i galea, ilia da nama bogoma: ne ha: i manu iasu. Na da hano hanai galea, ilia da nama wadela: i gamoga: i waini hano iasu.
Waliweka nyongo katika chakula changu na walinipa siki nilipokuwa na kiu.
22 Ilia lolo nasu da ili wadela: lesimu da defea. Ilia hamoma: ne sia: i lolo nasu da ilila: dafama: ne hamomu da defea.
Meza iliyoandaliwa mbele yao na iwe mtego, nayo iwe upatilizo na tanzi.
23 Gode! Dia ilia si wadela: lesima! Ilia baligi eso huluane gasa hamedenesima!
Macho yao yatiwe giza ili wasiweze kuona, nayo migongo yao iinamishwe daima.
24 Dia ougi hou ili da: iya soga: sima! Dia ougi hou da ilima baligili heda: ma: ma!
Uwamwagie ghadhabu yako, hasira yako kali na iwapate.
25 Ilia fisisu sogebi da dunu hamedene ba: mu da defea! Ilia abula diasu ganodini, dunu afae esalebe hame ba: mu da defea!
Mahali pao na pawe ukiwa, wala asiwepo yeyote atakayeishi katika mahema yao.
26 Ilia da dunu ilima Di da se iasu, ilima baligili se iaha. Ilia da dunu amo Dia da fa: ginisi, amo ilia se nabasu ba: beba: le, oufesega: ne sia: daha.
Kwa kuwa wanawatesa wale uliowajeruhi, na kuzungumza juu ya maumivu ya wale uliowaumiza.
27 Ilia wadela: i hou hamoi huluane dedene sa: i dialoma! Dia gaga: su amoga ilia afae mae lama: ma!
Walipize uovu juu ya uovu, usiwaache washiriki katika wokovu wako.
28 Ilia dio Fifi Ahoanusu Meloa amo ganodini dedei dialebe, amo fadegama! Dia fi ilia dio dedei, amoga ilia dio mae dialoma: ma!
Wafutwe kutoka kitabu cha uzima na wasiorodheshwe pamoja na wenye haki.
29 Be na da heawini se bagade naba. Gode! Na gaguia gadole, amola na gaga: ma!
Mimi niko katika maumivu na dhiki; Ee Mungu, wokovu wako na unihifadhi.
30 Na da Godema nodone gesami hea: mu! Na da Ema nodobeba: le, Ea gasa bagade hou eno dunuma sisia: i lamu.
Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo, nami nitamtukuza kwa kumtolea shukrani.
31 Hina Gode da bulamagau gobele salasu amola bulamagau gawali noga: le dei, amo gobele salasu hahawane ba: sa. Be na da Ema dafawane nodosea, E da amo hou da ohe gobele salasu amo baligisa ba: sa.
Hili litampendeza Bwana kuliko ngʼombe dume, zaidi ya fahali akiwa na pembe na kwato zake.
32 Banenesi dunu da amo hou ba: sea, hahawane ganumu. Dunu amo da Godema nodosu da amo hou ba: sea, dogo denesi dagoi ba: mu.
Maskini wataona na kufurahi: ninyi mnaomtafuta Mungu, mioyo yenu na iishi!
33 Hina Gode da liligi hame gagui hahani dunu amo ilia adole ba: su naba. E da Ea dunu amo da afugi diasu ganodini esalebe, hame gogolesa.
Bwana huwasikia wahitaji wala hadharau watu wake waliotekwa.
34 Hebene amola osobo bagade amola hano wayabo bagade! Amo ganodini esalebe liligi huluane! Godema nodoma!
Mbingu na dunia zimsifu, bahari na vyote viendavyo ndani yake,
35 E da Yelusaleme moilai bai bagade gaga: mu! E da Yuda moilale gagai huluane bu gagumu. Ea fi dunu da amogawi esalumu, amola ilia da Isala: ili soge gaguli fimu.
kwa maana Mungu ataiokoa Sayuni na kuijenga tena miji ya Yuda. Kisha watu watafanya makao yao humo na kuimiliki,
36 Hina Gode Ea hawa: hamosu dunu iligaga fi dunu da amo soge, nana agoane lamu. Amola dunu amo da Ema asigi, ilia da amogai esalumu.
watoto wa watumishi wake watairithi na wale wote walipendao jina lake wataishi humo.

< Gesami Hea:su 69 >