< Yone 18 >

1 Yesu da amo sia: ne gadoi dagoloba, E amola Ea ado ba: su dunu, amo sogebi yolesili, Gidalone Hano degei dagoi. Amo sogebi da ifabi dialu. Amo ganodini, Yesu amola Ea ado ba: su dunu asi.
Yesu alipomaliza kuomba, akaondoka na wanafunzi wake wakavuka Bonde la Kidroni. Upande wa pili palikuwa na bustani, yeye na wanafunzi wake wakaingia humo.
2 Yudase (hohonosu dunu) da amo sogebi dawa: i galu. Bai Yesu amola Ea ado ba: su dunu da eso bagohame amogawi gilisilalu.
Basi Yuda, yule aliyemsaliti alipafahamu mahali hapo kwani Yesu alikuwa akikutana humo na wanafunzi wake mara kwa mara.
3 Amaiba: le Yudase da amo ifabia doaga: i. Louma dadi gagui dunu amola Debolo sosodo aligisu dunu (gobele salasu dunu amola Fa: lisi dunu da amo asunasi), Yudase ea baligiga aligi. Ilia dadi, gigi, gobihei, gamali amola hanu amo gagaguli misi.
Hivyo Yuda akaja bustanini. Aliongoza kikosi cha askari wa Kirumi, na baadhi ya maafisa kutoka kwa viongozi wa makuhani na Mafarisayo. Nao walikuwa wamechukua taa, mienge na silaha.
4 Ema misunu hou huluane dawa: beba: le, Yesu da gusuba: iwane aliagusuli, ilima amane adole ba: i, “Dilia da nowa hogosala: ?”
Yesu akijua yale yote yatakayompata, akajitokeza mbele yao akawauliza, “Mnamtafuta nani?”
5 Ilia bu adole i, “Ninia Yesu, Na: salede dunu, hogosa!” E amane sia: i, “Na wea!” Yudase, hohonosu dunu, da ili gilisili lelu.
Wao wakamjibu, “Yesu wa Nazareti.” Yesu akawajibu, “Mimi ndiye.” Yuda, yule aliyemsaliti alikuwa amesimama pamoja nao.
6 Yesu da, “Na wea!” amo sia: beba: le, ilia fofogadigili baligiduli ahoanu, osoba diasa: i.
Yesu alipowaambia, “Mimi ndiye,” walirudi nyuma na kuanguka chini!
7 Yesu da ilima bu adole ba: i, “Dilia da nowa hogosala: ?” Ilia bu amane sia: i, “Yesu, Na: salede dunu!”
Akawauliza tena, “Mnamtafuta nani?” Nao wakamjibu, “Yesu wa Nazareti.”
8 Yesu E amane sia: i “Na da wea!, amo Na da sia: i dagoi! Na fawane dilia hogole ba: beba: le, amo eno dunu gui esala ilima hahawane masa: ne sia: ma.”
Yesu akawaambia, “Nimekwisha kuwaambia kuwa, mimi ndiye; kwa hiyo kama mnanitafuta mimi, waacheni hawa watu waende zao.”
9 (Ea musa: sia: i amane, “Ada! Dia Nama iasu dunu huluane, Na da afadafa hame fisi,” amo sia: dafawaneyale ba: musa: , E sia: i.)
Hii ilikuwa ili litimie lile neno alilosema, “Sikumpoteza hata mmoja miongoni mwa wale ulionipa.”
10 Saimone Bida da gegesu gobihei bagade gaguiba: le, ea gobihei duga: le gadole, gobele salasu Ouligisu dunu ea hawa: hamosu dunu amo ea gedafa, damuni fasi. (Amo hawa: hamosu dunu ea dio amo Ma: lagase.)
Simoni Petro, aliyekuwa na upanga, akaufuta na kumkata sikio la kuume mtumishi wa kuhani mkuu. Jina la mtumishi huyo aliitwa Malko.
11 Yesu da Bidama amane sia: i, “Dia gegesu gobihei bu salima! Na da se nabasu faigelei amo Na Ada Nama i, amo Na da hame manu di dawa: bela: ? Na da manu!”
Yesu akamwambia Petro, “Rudisha upanga wako kwenye ala yake. Je, hainipasi kukinywea kikombe alichonipa Baba?”
12 Amalalu, Louma dadi gagui dunu amola ilia ouligisu dunu, amola Yu ouligisu dunu, ilia da Yesu afugili, efega la: gi.
Hivyo wale askari, wakiwa pamoja na majemadari wao na maafisa wa Wayahudi, wakamkamata Yesu na kumfunga.
13 Ilia da E A: nasema bisili hiouginana asi. A: nase da gobele salasu Ouligisu dunu Ga: iafa: se ea esoa: esalu.
Kwanza wakampeleka kwa Anasi, mkwewe Kayafa, aliyekuwa kuhani mkuu mwaka ule.
14 Ga: iafa: se da musa: Yu ouligisu dunuma amane sia: i dagoi, “Dunu huluane gaga: ma: ne, dunu afadafa fawane bogomu da defea.”
Kayafa ndiye alikuwa amewashauri Wayahudi kwamba imempasa mtu mmoja kufa kwa ajili ya watu.
15 Saimone Bida, eno ado ba: su dunu afadafa, da Yesuma fa: no bobogelalu. Eno ado ba: su dunu, e da gobele salasu Ouligisu dunu dawa: beba: le, e da Yesu sigi ahoanu, gobele salasu Ouligisu dunu ea diasu gagoi amo ganodini golili sa: i.
Simoni Petro pamoja na mwanafunzi mwingine walikuwa wakimfuata Yesu. Huyu mwanafunzi mwingine alikuwa anafahamika kwa kuhani mkuu, hivyo aliingia ndani ya ukumbi pamoja na Yesu.
16 Be Bida da gadili ouesalu. Be eno ado ba: su dunu da a: fini logo holeiga ouesalu, ema sia: beba: le, e da Bida ganodini oule misi.
Lakini Petro alisimama nje karibu na lango, ndipo yule mwanafunzi mwingine, aliyejulikana na kuhani mkuu, akazungumza na msichana aliyekuwa analinda lango, akamruhusu Petro aingie ndani.
17 Logo holei ouligisu a: fini da Bidama amane sia: i, “Di da amo dunu Ea ado ba: su dunula: ?” Be Bida bu adole i, “Nnn! Na da hame!”
Yule msichana akamuuliza Petro, “Je, wewe pia si mmoja wa wanafunzi wa mtu huyu?” Petro akajibu, “Sio mimi.”
18 Anegagiba: le, hawa: hamosu dunu amola sosodo aligisu dunu, ilia da nasuba gilisili, lalu didi. Amalalu, ilia lalu amoga sisiga: le housa lelu. Amaiba: le, Bida da amoga asili, ilia gilisili housa lelu.
Wale watumishi na askari walikuwa wamesimama wakiota moto wa makaa kwa sababu palikuwa na baridi, Petro naye alikuwa amesimama pamoja nao akiota moto.
19 Gobele salasu Ouligisu dunu da Yesu Ea ado ba: su dunu ilia hou, amola Yesu Ea olelesu, amo dawa: ma: ne, Yesuma adole ba: su.
Wakati huo kuhani mkuu akawa anamuuliza Yesu kuhusu wanafunzi wake na mafundisho yake.
20 Yesu da bu adole, i, “Na da wamowane hame, be dunu huluane ilima moloiwane sia: su. Na da Debolo, sinagoge, amola dunu ilia gilisisu sogebi, amoga fawane sia: olelesu. Na da sadoga sia: hamedafa sia: su.
Yesu akamjibu, “Nimekuwa nikizungumza waziwazi mbele ya watu wote. Siku zote nimefundisha katika masinagogi na Hekaluni, mahali ambapo Wayahudi wote hukusanyika. Sikusema jambo lolote kwa siri.
21 Amaiba: le, di da abuliba: le Nama adole ba: sa? Na sia: nabi dunu ilima adole ba: ma! Na ilima adoi, amo ilima adole ba: ma. Ilia Na adoi dawa: !”
Mbona unaniuliza mimi maswali? Waulize wale walionisikia yale niliyowaambia. Wao wanajua niliyosema.”
22 Yesu da amo sia: beba: le, Debolo Diasu sosodo aligisu dunu afadafa da Yesu Ea odagia fai. E amane sia: i, “Di da abuliba: le gobele salasu Ouligisu dunu ema agoane sia: bela: ?”
Alipomaliza kusema hayo, mmoja wa askari aliyekuwa amesimama karibu naye, akampiga Yesu kofi usoni, kisha akasema, “Je, hivyo ndivyo unavyomjibu kuhani mkuu?”
23 Yesu E bu adole i, “Na da wadela: i hou hamoi galea, defea, amo hou dunu huluane ilima adoma. Be Na da dafawane sia: i galea, dia da abuliba: le Na fabela: ?”
Yesu akamjibu akasema, “Kama nimesema jambo baya, shuhudia huo ubaya niliousema. Lakini kama nimesema yaliyo kweli, mbona umenipiga?”
24 Amalalu, A:nase da Yesu E Ga: iafa: se (gobele salasu Ouligisu dunudafa) ema afugili la: gili hiouginana asi.
Ndipo Anasi akampeleka Yesu kwa kuhani mkuu Kayafa, akiwa bado amefungwa.
25 Bida da lalu gadenei housa lelu. Amalalu, eno dunu ilia da ema adole ba: i, “Di, da amo dunu Ea ado ba: su dunula: ?” Be Bida amane sia: i, “Nnn! Hame mabu!”
Wakati huo Simoni Petro alikuwa amesimama akiota moto. Baadhi ya wale waliokuwepo wakamuuliza, “Je, wewe si mmoja wa wanafunzi wake?” Petro akakana, akasema, “Sio mimi.”
26 Gobele salasu Ouligisu dunu ea udigili hawa: hamosu dunu afadafa (amo da dunu Bida ea ge damuni fasi, amo ea fi dunu) e Bidama adole ba: i, “Na da Di amola Yesu, alia gilisili ifabi ganodini esalebe ba: bela: ?”
Mmoja wa watumishi wa kuhani mkuu, ndugu yake yule mtu ambaye Petro alikuwa amemkata sikio, akamuuliza, “Je, mimi sikukuona kule bustanini ukiwa na Yesu?”
27 Be Bida e bu sia: i, “Hame mabu!” Sia: noba, gagala gawali ga: be nabi.
Kwa mara nyingine tena Petro akakana, naye jogoo akawika wakati huo huo.
28 Hahabedafa, ilia da Ga: iafa: se diasu yolesili, Yesu Gamane hina dunu ea diasuga hiouginana asi. Yu dunu ilia sema da eno dunuma gilisisia, ledo hamobeba: le, Baligisu Lolo manu da hamedei. Yu ouligisu dunu da amo sema dawa: beba: le, Gamane hina diasu ganodini hame golili sa: i.
Ndipo Wayahudi wakamchukua Yesu kutoka kwa Kayafa na kumpeleka kwenye jumba la kifalme la mtawala wa Kirumi. Wakati huo ilikuwa ni alfajiri, ili kuepuka kuwa najisi kwa taratibu za ibada, Wayahudi hawakuingia ndani kwa sababu ya sheria za Kiyahudi. Wangehesabiwa kuwa najisi kama wangeingia nyumbani mwa mtu asiye Myahudi na wasingeruhusiwa kushiriki katika Sikukuu ya Pasaka.
29 Amaiba: le, Bailade da gadili misini, ilima amane adole ba: i, “E da adi wadela: i hou hamoiba: le, dilia amo dunuma diwaneya udidisala: ?”
Hivyo Pilato akatoka nje walikokuwa akawauliza, “Mmeleta mashtaka gani kumhusu mtu huyu?”
30 Ilia bu adole i, “E da wadela: i hame hamoi ganiaba, ninia dima hame oule ma: noba.”
Wao wakamjibu, “Kama huyu mtu hakuwa mhalifu tusingemleta kwako.”
31 Bailade da ilima amane sia: i, “Defea! Amaiba: le, dilia sema defele, dilisu amo dunuma fofada: ma!” Be ilia bu adole i, “Ninia da dunu fuga: ma: ne fofada: mu, amo Gamane sema bagade gala.”
Pilato akawaambia, “Basi mchukueni ninyi mkamhukumu kwa kufuata sheria zenu.” Wayahudi wakamjibu, “Sisi haturuhusiwi kutoa hukumu ya kifo kwa mtu yeyote.”
32 (Amo hou da Yesu Ea bogomu hou sia: i, amo sia: dafawaneyale ba: ma: ne misi. Bai Louma dunu ilia bogoma: ne se iasu da bulufalegeiga medosu hou.)
Walisema hivyo ili yale maneno aliyosema Yesu kuhusu kifo atakachokufa yapate kutimia.
33 Bailade da bu ea diasu ganodini sa: ili, Yesu ema misa: ne sia: ne, Ema amane adole ba: i, “Di da Yu fi dunu ilia Hina Bagadela: ?”
Kwa hiyo Pilato akaingia ndani ya jumba la kifalme, akamwita Yesu, akamuuliza, “Wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?”
34 Yesu da bu adole i, “Amo adole ba: su da di adobela: ? Ma eno dunu ilia adoiba: le di adole ba: sala: ?”
Yesu akamjibu, “Je, unauliza swali hili kutokana na mawazo yako mwenyewe, au uliambiwa na watu kunihusu mimi?”
35 Bailade bu adole i, “Na da Yu dunu di dawa: bela: ? Dia fidafa dunu amola gobele salasu ouligisu dunu, ilia da Di nama oule misi. Dia adi hamobela: ?”
Pilato akamjibu, “Mimi si Myahudi, ama sivyo? Taifa lako mwenyewe na viongozi wa makuhani wamekukabidhi kwangu. Umefanya kosa gani?”
36 Yesu E amane sia: , “Na Hinadafa Hou da osobo bagade liligi hame. Na Hinadafa Hou da osobo bagade liligi ganiaba, Yu ouligisu dunu ilia da Na mae lama: ne, Na fa: no bobogesu dunu da gegena: noba. Be hame! Na Hinadafa Hou da guiguda: liligi hame!”
Yesu akajibu, “Ufalme wangu si wa ulimwengu huu. Ufalme wangu ungekuwa wa ulimwengu huu, wafuasi wangu wangenipigania ili nisitiwe mikononi mwa Wayahudi. Lakini kama ilivyo, ufalme wangu hautoki hapa ulimwenguni.”
37 Amalalu, Bailade da Ema amane adole ba: i, “Amaiba: le, Di da Hina Bagade esalabela: ?” Yesu da bu adole i, “Na da Hina Bagade di da sia: sa! Di dafawane sia: sa! Bai Na da dafawanedafa hou olelema: ne, amo fawane Na da lalelegei, amola osobo bagadega misi. Nowa da dafawanedafa hou dafawaneyale dawa: sea, e da Na sia: naba.”
Pilato akamuuliza, “Kwa hiyo wewe ni mfalme?” Yesu akajibu, “Wewe wasema kwamba mimi ni mfalme. Kwa kusudi hili nilizaliwa, na kwa ajili ya hili nilikuja ulimwenguni, ili niishuhudie kweli. Mtu yeyote aliye wa kweli husikia sauti yangu.”
38 Bailade da adole ba: i, “Dafawanedafa hou da adi houla: ?” Amalalu, Bailade da bu gadili asili, dunu huluane ilima amane sia: i, “Na da Ema se imunusa: fofada: su hamedafa ba: sa.
Pilato akamuuliza Yesu, “Kweli ni nini?” Baada ya kusema haya Pilato akaenda nje tena akawaambia wale viongozi wa Wayahudi waliomshtaki Yesu, “Sioni kosa lolote alilotenda mtu huyu.
39 Be dilia hou defele, Baligisu Lolo Nasu amoha ode huluane se iasu diasu hamosu dunu afadafa ea se iasu diasu logo na doasisa. Na da Yu dunu ilia Hina Bagade Ea se iasu diasu logo doasimu da defeala: ?”
Lakini ninyi mna desturi yenu kwamba wakati wa Pasaka nimwachie huru mfungwa mmoja mnayemtaka. Je, mnataka niwafungulie huyu ‘Mfalme wa Wayahudi’?”
40 Be ilia ha: giwane halasu, “Hame mabu! E hame! Ninia da Bala: ba: se hanai!” (Bala: base da fasu amola wamolasu dunu.)
Wao wakapiga kelele wakisema, “Si huyu mtu, bali tufungulie Baraba!” Yule Baraba alikuwa mnyangʼanyi.

< Yone 18 >