< Yoube 21 >

1 Yoube da amane sia: i,
Ndipo Ayubu akajibu:
2 Na sia: be nabima! Na da amo dogo denesisu fawane dilima adole ba: sa.
“Yasikilizeni maneno yangu kwa makini; hii na iwe faraja mnayonipa mimi.
3 Dilia na sia: ma: ne, logo doasima! Amasea, na sia: da dagosea, dilia da hanaiba: le, ba: sola: le gagama!
Nivumilieni ninapozungumza, nami nikishazungumza, endeleeni kunidhihaki.
4 Na sia: ga gegesu da osobo bagade dunu ilima hame. Be na momabo hou da bai bagade gala.
“Je, kwani malalamiko yangu yanaelekezwa kwa mwanadamu? Kwa nini nisikose subira?
5 Nama ba: ma! Dilia fofogadigi ouiya: le ha: gi nama sosodomu da defea.
Niangalieni mkastaajabu; mkaweke mkono juu ya vinywa vyenu.
6 Na da nama hamoi hou amo bu dawa: sea, na da dawa: su hamedei amola na da yagugusa.
Ninapowaza juu ya hili, ninaogopa, nao mwili wangu unatetemeka.
7 Abuliba: le Gode da wadela: i hou hamosu dunu esaloma: ne yolesisala: ? E abuliba: le ili da: i hamone amola bagade gaguiwane esaloma: ne yolesisala: ?
Kwa nini waovu wanaendelea kuishi, wakifikia umri wa uzee na kuendelea kuwa na nguvu?
8 Ilia da ilia mano amola ilia aowalali ilia asigilabe ba: musa: sosodo esafulu.
Huwaona watoto wao wakithibitika wakiwa wamewazunguka, wazao wao mbele za macho yao.
9 Gode da ili diasu amoga gugunufinisisu hou hame iasisa. Ilia da beda: didigisa hame esalumu.
Nyumba zao zi salama wala hakuna hofu; fimbo ya Mungu haiko juu yao.
10 Dafawane, ilia bulamagau da galuli amola mae se nabawane mano lalelegesa.
Madume yao ya ngʼombe huvyaza bila kushindwa kamwe; ngʼombe wao huzaa wala hawaharibu mimba.
11 Ilia mano da sibi mano defele, hehenaiya hehedela lafiadala.
Huwatoa watoto wao nje kama kundi; wadogo wao huchezacheza.
12 Ilia sani baidama amola fulabosu amo dudududabe amoga gafosa.
Huimba nyimbo kwa matari na kwa kinubi, nao huifurahia sauti ya filimbi.
13 Ilia olofole agoane esalu, se mae nabawane bogosa. (Sheol h7585)
Huitumia miaka yao katika mafanikio nao hushuka kaburini kwa amani. (Sheol h7585)
14 Wadela: i hamosu dunu da Godema ili udigili yolesima: ne sia: sa. Gode da ilia esala hamomu ilegesa. Be ilia amo ilegei dawa: mu hame hanai.
Lakini humwambia Mungu, ‘Tuache sisi!’ Hatuna haja ya kufahamu njia zako.
15 Ilia da Godema hawa: hamomu da hamedei liligi agoane dawa: sa. Ilia Godema sia: ne gadosu da ilia hou hame fidima: beyale dawa: lala.
Mwenyezi ni nani hata tumtumikie? Tutapata faida gani kumwomba?
16 Ilia da ilila: gasaga didili hamosa sia: sa. Be na da ilia asigi dawa: su hou amo hame lale gamu.
Lakini kufanikiwa kwao hakupo mikononi mwao wenyewe, hivyo najitenga mbali na shauri la waovu.
17 Dilia da wadela: i hamosu dunu afae ea hadigi ha: ba: doi dagoi ba: bela: ? Wadela: i hamosu dunu afae da gugunufinisisu hou ema doaga: be ba: bela: ? Gode da ougiba: le, wadela: i hamosu dunu afae amoma se dabe ibela: ?
“Lakini ni mara ngapi taa ya waovu huzimwa? Ni mara ngapi maafa huwajia, yale yawapatayo ambayo Mungu huwapangia katika hasira yake?
18 E da wadela: i hamosu dunu amo gisi foga mini asi defele, ili fulabole fasibala: ? O gulu isuga mini asi defele, ili fulabole fasibala: ?
Ni mara ngapi huwa kama majani makavu mbele ya upepo, kama makapi yachukuliwayo na dhoruba?
19 Dilia da amane sia: sa! Gode da mano ea ada wadela: le hamoiba: le, amo manoma se dabe iaha. Hame mabu! Gode da wadela: i hamosu dunu, ilima fawane se dabe imunu da defea. E da ilia wadela: le hamoiba: le, ilima se dabe iaha, amo olelemu da defea.
Imesemekana, ‘Mungu huiweka akiba adhabu ya mtu kwa ajili ya wanawe.’ Mungu na amlipe mtu mwenyewe, ili apate kulijua!
20 Wadela: i hamosu dunu ilia da ilia hamobeba: le fawane se dabe lamu da defea. Ilia Gode Bagadedafa Ea ougi bagade hou ba: mu da defea.
Macho yake mwenyewe na yaone maangamizi yake; yeye na ainywe ghadhabu ya Mwenyezi.
21 Ninia esalusu da dagosea, ninia mano da hahawane esaloma: bela: le dawa: ma: bela: ?
Kwani anajali nini kuhusu jamaa anayoiacha nyuma, miezi yake aliyopangiwa ifikapo mwisho?
22 Dunu afae da Gode Ema hou olelema: bela: ? Hame mabu! Gode da dunu amo da baligili gadodafa heda: i, ilima fofada: sa.
“Je, yuko mtu yeyote awezaye kumfundisha Mungu maarifa, iwapo yeye ndiye ahukumuye hata walio juu ya wote?
Mtu mmoja hufa akiwa na nguvu zake kamili, akiwa salama na mwenye raha kamili,
24 Dunu mogili da dagumuiwane esalea bogosa. Ilia da hahawane se mae nabawane esalu, amalu bogosa.
mwili wake ukiwa umenawiri, nayo mifupa yake ikiwa imejaa mafuta ndani yake.
25 Mogili ilia da hahawane hame esalu, bogosa. Ilia da esalea amola bogosea, eso huluane hihiwane gala.
Mtu mwingine hufa katika uchungu wa nafsi, akiwa hajafurahia kamwe jambo lolote zuri.
26 Be dunu huluane da defele bogole, uli dogosa. Ili huluane da daba: ga dedeboi dagoi ba: sa.
Hao wote hulala mavumbini, nao mabuu huwafunika wote.
27 Dilia dogo ganodini ougi dialebe, amo na dawa:
“Ninayajua kikamilifu yale mnayoyafikiri, mipango ambayo kwayo mngenitendea mabaya.
28 Dilia da agoane adole ba: sa, ‘Mimogo dunu amo da wadela: le hamosu, amo ea diasu da wali habila: ?’
Mwasema, ‘Iko wapi sasa nyumba ya huyo mtu mkuu, mahema ambayo watu waovu walikaa?’
29 Dilia da lalusu dunu amo bisili sia: sa: ibela: ? Ilia ga asi misini, sia: ne iasu dilia hame nabibala: ?
Je, hamkuwahi kuwauliza hao wanaosafiri? Je, hamkutafakari taarifa zao:
30 Gode da ougiba: le, se dabe bidi iasea, E da wadela: le hamosu dunuma se dabe hame iaha.
kwamba mtu mwovu huepushwa kutoka siku ya maafa, kwamba huokolewa kutoka siku ya ghadhabu?
31 Dunu afae da wadela: le hamosu dunuma diwaneya udidimu, o ilia wadela: le hamobeba: le se dabe imunu da hamedafa gala.
Ni nani hulaumu matendo yake mbele ya uso wake? Ni nani ampatilizaye kwa yale aliyoyatenda?
Hupelekwa kaburini, nao ulinzi ukawekwa kwenye kaburi lake.
33 Dunu eno da ilia bogoi da: i hodo amo bogoi uli dogoiga gaguli ahoasea, dunu osea: idafa da ilima asigiba: le, mogodigili fa: no bobogesa. Amola osobo da ilia da: i da: iya gebewane dialebe ba: sa.
Udongo ulio bondeni ni mtamu kwake; watu wote watamfuata, nao umati wa watu usiohesabika umemtangulia.
34 Be dilia! Dilia da na dogo denesima: ne, hamedei sia: fawane sia: sa. Dilia nama adole iasu huluane da ogogosu sia: fawane.”
“Hivyo ninyi mnawezaje kunifariji kwa upuzi wenu? Hakuna kilichosalia cha majibu yenu isipokuwa uongo!”

< Yoube 21 >