< Aisaia 36 >

1 Ode 14 amo hina bagade Hesigaia ea Yuda fi ouligibiga, Sena: gelibi (Asilia hina bagade) da Yuda gagoi gagili sali moilai amoma doagala: le, suguli lai dagoi.
Katika mwaka wa kumi na nne wa utawala wa Mfalme Hezekia, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaishambulia miji yote ya Yuda yenye ngome na kuiteka.
2 Amalalu, e da ea bisilua ouligisu dunu, amo da dadi gagui dunu gilisisu amoma bisili, La: igisi moilai bai bagade fisili, Yelusalemega asili, hina bagade Hesigaia amoma e da bu gegesu fisili, Yelusaleme ema imunu, amo sia: ma: ne asunasi. Amo ouligisu dunu da asili, logo amoga abula hahamosu dunu da hawa: hamosu (amo da hano logo da gadodili hano wayabo amoga hano gaguli maha, amo gadenene), amo logoga esalu.
Kisha mfalme wa Ashuru akamtuma jemadari wa jeshi pamoja na jeshi kubwa kutoka Lakishi hadi kwa Mfalme Hezekia huko Yerusalemu. Jemadari wa jeshi akasimama kwenye mfereji wa Bwawa la Juu, lililojengwa katika barabara iendayo kwenye Uwanja wa Dobi.
3 Yuda dunu udiana da ema misi. Ilia dio da Ilaiagime (Hiligaia egefe) amola Siebena (sia: dedesu dunu) amola Youa (A: isa: fe egefe).
Eliakimu mwana wa Hilkia aliyekuwa msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna aliyekuwa katibu, na Yoa mwana wa Asafu mwandishi wakamwendea.
4 Asilia bisilua ouligisu dunu da Hesigaia da Asilia hina bagadema abuliba: le hame beda: i, amo hou dawa: musa: hanai galu.
Jemadari wa jeshi akawaambia, “Mwambieni Hezekia, “‘Hili ndilo asemalo mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru: Ni wapi unapoweka hili tumaini lako?
5 E amane sia: i, “Dilia da adi dawa: bela: ? Sia: fawane da gasa bagade dadi gagui gilisisu amola gegesu dawa: su hou amoga hasanasima: bela: ? Dilia da Asilia ilima odoga: sea, nowa da fidima: bela: ?
Unasema mnayo mikakati na nguvu za kijeshi, lakini unasema maneno matupu tu. Je, wewe unamtegemea nani, hata ukaniasi mimi?
6 Dilia da Idibidi da dili fidimu dawa: lala. Be amo hou da dilia gasa hame saga: lale, galiamo hamomusa: dawa: su defele. Amo da fili, dia lobo somu. Idibidi hina bagade ea hou da agoaiwane gala. Nowa da ea fidisu hou dafawaneyale dawa: sea da se nabimu.”
Tazama sasa, unaitegemea Misri, fimbo ile ya mwanzi uliopasuka, ambayo huuchoma na kuujeruhi mkono wa mtu akiiegemea! Hivyo ndivyo alivyo Farao mfalme wa Misri, kwa wote wanaomtegemea.
7 Asilia ouligisu dunu da eno amane sia: i, “Dilia da dilia Hina Gode da dili fidima: ne dawa: bela: ? Hesigaia da Yuda dunu amola Yelusaleme dunu ilima ilia ‘oloda’ afae fawane amoga Godema sia: ne gadomusa: sia: beba: le, e da dilia Hina Gode Ea ‘oloda’ amola sia: ne gadosu liligi eno wadela: lesi dagoi.
Nawe kama ukiniambia, “Tunamtumainia Bwana Mungu wetu”: je, siyo yeye ambaye Hezekia aliondoa mahali pake pa juu pa kuabudia miungu na madhabahu zake, akiwaambia Yuda na Yerusalemu, “Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu haya”?
8 Na da na hina bagade ea dioba: le, dilima agoane hou hamomu. Dilia da dunu 2000 agoane, hosi fila heda: ma: ne defele esala amo hogole ba: sea, na da dilima hosi 2000 agoane ili fila heda: ma: ne imunu.
“‘Njooni sasa, fanyeni mapatano na bwana wangu, mfalme wa Ashuru: Nitakupa farasi elfu mbili, kama unaweza kuwapandisha waendesha farasi juu yao!
9 Dilia da Asilia ouligisu dunu afae fonobahadidafa hasaliimu defele hame ba: sa. Amaiba: le, dilia abuliba: le Idibidi dunu da dilima sa: liode amola hosi da: iya fila heda: i dadi gagui dunu dilima asunasima: ne dawa: sala: ?
Utawezaje kumzuia hata afisa mmoja aliye mdogo kati ya maafisa wa bwana wangu, ijapo unategemea Misri kwa magari ya vita na wapanda farasi?
10 Hina Gode da na fidibiba: le, na da dilia soge amo doagala: le wadela: lesi dagoi. Hina Gode Hisu da na asunasi dagoiba: le, na da agoane hamosu.”
Zaidi ya hayo, je, nimekuja kushambulia na kuangamiza nchi hii bila Bwana? Bwana mwenyewe ndiye aliniambia niishambulie nchi hii na kuiangamiza.’”
11 Amalalu, Ilaiagime amola Siebena amola Youa da amane sia: i, “Elama: igi sia: amoga ninima sia: ma! Ninia da amo sia: dawa: Hibulu sia: amoga mae sia: ma. Bai dunu huluane gagoi da: iya esalebe da nabasa: besa: le, Elama: igi sia: sia: ma.”
Ndipo Eliakimu, Shebna na Yoa wakamwambia yule jemadari wa jeshi, “Tafadhali zungumza na watumishi wako kwa lugha ya Kiaramu, kwa kuwa tunaifahamu. Usiseme nasi kwa Kiebrania watu walioko juu ya ukuta wakiwa wanasikia.”
12 Be Asilia ouligisu da bu adole i, “Dilia adi dawa: bela: ? Asilia hina bagade da dili amola Yuda hina bagade amo fawane nabima: ne, na hame asunasi. Hame mabu! Na da dunu huluane gagoi amoga esalebe ilima sia: sa. Bai ilia da dili defele ilila: iga manu amola ilila: baea manu.”
Lakini yule jemadari wa jeshi akajibu, “Je, bwana wangu amenituma kutoa ujumbe huu kwa bwana wenu na kwenu tu? Je, hakunituma pia kwa watu walioketi ukutani, ambao, kama ninyi, itawabidi kula mavi yao na kunywa mikojo yao wenyewe?”
13 Amalalu, amo Asilia ouligisu dunu da wa: legadole amola Hibulu sia: amoga amane sia: i, “Nabima! Asilia hina bagade da dilima agoane sia: sa.
Kisha yule jemadari wa jeshi akasimama na kuita kwa lugha ya Kiebrania, akasema: “Sikieni maneno ya mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru!
14 E da dilima sisasu, amo Hesigaia ea ogogosu sia: mae nabima. Hesigaia da dili gaga: mu da hamedei.
Hili ndilo asemalo mfalme: Msikubali Hezekia awadanganye. Hawezi kuwaokoa!
15 Amola e da dilima Hina Gode da dili gaga: mu sia: sea, ea sia: mae nabima. Hina Gode da dili gaga: mu, amola ninia Asilia dadi gagui gilisisu ilia da dilia moilai bai bagade suguli lama: ne logo hedofamu, mae dawa: ma.
Msikubali Hezekia awashawishi kumtumaini Bwana kwa kuwaambia, ‘Hakika Bwana atatuokoa. Mji huu hautaangukia mikononi mwa mfalme wa Ashuru.’
16 Hesigaia ea sia: mae nabima. Asilia hina bagade da dilia huluane dilia moilai bai bagade fisili, gadili misini, ea se dabe iasu hawa: hamoma: ne sia: sa. Dilia da dilia waini sagai amola figi sagai amoga waini fage amola figi fage manu amola dilia si amoga hano manu.
“Msimsikilize Hezekia. Hili ndilo mfalme wa Ashuru asemalo: Fanyeni amani nami na mje kwangu. Kisha kila mmoja wenu atakula kutoka kwa mzabibu wake na mtini wake mwenyewe, na kunywa maji kutoka kisima chake mwenyewe,
17 Amasea, Asilia hina bagade da dili soge eno dilia soge agoane (amo ganodini da waini sagai amola gagoma dilia baledehamoma: ne) amoga fima: ne oule masunu.
mpaka nije nikawapeleke katika nchi iliyo kama nchi yenu wenyewe, nchi ya nafaka na divai mpya, nchi ya mkate na ya mashamba ya mizabibu.
18 Hesigaia ea sia: amo da Hina Gode da dili gaga: mu, amo da ogogosa. Mae nabima! Fifi asi gala eno huluane ilia ‘gode’ liligi da Asilia hina bagade ili mae hasanasima: ne gaga: bela: ? Hame mabu!
“Msikubali Hezekia awapotoshe asemapo, ‘Bwana atatuokoa.’ Je, yuko mungu wa taifa lolote aliyewahi kuokoa nchi yake kutoka mkononi mwa mfalme wa Ashuru?
19 Ha: ima: de amola Aba: de ilia ‘gode’ liligi da wali habila: ? Amola Sefafa: ime ilia ‘gode’ liligi ilia da habila: ? Nowa da Samelia fi gaga: bela: ?
Iko wapi miungu ya Hamathi na ya Arpadi? Iko wapi miungu ya Sefarvaimu? Je, imeokoa Samaria kutoka mkononi mwangu?
20 Amo soge ilia ‘gode’ liligi da ninia hina bagade ilima mae hasanasima: ne gaga: bela: ? Hame mabu! Amaiba: le, dilia da abuliba: le Hina Gode da Yelusaleme gaga: ma: ne defele esala, dawa: bela: ?”
Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya nchi hizi ameweza kuokoa nchi yake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Bwana aiokoe Yerusalemu mkononi mwangu?”
21 Be Yelusaleme fi dunu da hina bagade Hesigaia ea sia: defele ouiyale esalu. Ilia da sia: afadafa hame sia: i.
Lakini wale watu wakakaa kimya, wala hawakujibu lolote, kwa kuwa mfalme alikuwa amewaamuru, “Msimjibu lolote.”
22 Amalalu, Ilaiagime amola Siebena amola Youa da da: i dioiba: le, ilia abula gadelale, hina bagade Hesigaiama asili, Asilia ouligisu dunu ea sia: ema adole i.
Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna katibu, na Yoa mwana wa Asafu, mwandishi wakamwendea Hezekia, nguo zao zikiwa zimeraruliwa, na kumwambia yale jemadari wa jeshi aliyoyasema.

< Aisaia 36 >