< Mui 7 >
1 Amalalu, Hina Gode da Nowa: ma amane sia: i, “Di amola dia sosogo fi huluane, amo dusagai bagade amoga golili sa: ima. Bai waha esalebe fi amo ganodini, Na da di fawane hahawane ba: i.
Ndipo Bwana akamwambia Noa, “Ingia katika safina wewe na jamaa yako yote, kwa sababu katika kizazi hiki nimeona ya kuwa wewe ni mwenye haki.
2 Ohe fi hisu hisu liligi ledo hamedei amo gawali amola aseme amo fesuale agoane dusagai ganodini oule masa. Amola liligi ledo gala amo gawali amola aseme aduna aduna fawane oule masa.
Uchukue wanyama saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, na wanyama wawili wawili wa kila aina walio najisi wa kiume na wa kike.
3 Amola sio fi hisu hisu mae bogole osobo bagadega esaloma: ne, amo fesuale gawali amola aseme dusagai ganodini oule masa.
Pia uchukue ndege saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, ili kuhifadhi aina zao mbalimbali katika dunia yote.
4 Eso fesuale aligili, Na da gibu bagade osobo bagadega iasimu. Gibu da eso 40 amola gasi 40 sa: imu. Amoga na da esalebe liligi huluane Na hamoi, amo huluane osobo bagadega mugululi fasimu.
Siku saba kuanzia sasa nitaleta mvua juu ya nchi kwa siku arobaini usiku na mchana, nami nitafutilia mbali kutoka uso wa nchi kila kiumbe hai nilichokiumba.”
5 Nowa: da Gode Ea hamoma: ne sia: i liligi huluane hamoi.
Noa akafanya yote kama Bwana alivyomwamuru.
6 Hano bagade da osobo bagadega doaga: loba, Nowa: da ode 600 agoane ba: i.
Noa alikuwa na miaka 600 gharika ilipokuja juu ya dunia.
7 Amola Nowa: , ea manolali, ea uda amola ea mano ilia uda da hano bagade fisimusa: , dusagai ganodini fila heda: i.
Noa na mkewe na wanawe na wake zao wakaingia katika safina ili waepuke ile gharika.
8 Ledo hamedei ohe fi amola ledo gala liligi aduna aduna, sio fi, osoboa sugi ahoasu liligi,
Jozi ya wanyama walio safi na walio najisi, ndege na viumbe vitambaavyo,
9 gawali amola aseme amo huluane Nowa: ma misini, dusagai ganodini fila heda: i. Gode da Nowa: ma hamoma: ne sia: i, amo defele hamoi dagoi ba: i.
wa kiume na wa kike, walikuja kwa Noa wakaingia katika safina kama Mungu alivyomwamuru Noa.
10 Amola eso fesuale aligili galu, hano bagade da moi bagadega doaga: i.
Baada ya siku saba, maji ya gharika yakaja juu ya dunia.
11 Nowa: da ode 600 esalu. Amo ode ganodini, oubi ageyadu amola eso 17 - amo esoga, hano osobo hagudu dialu amo da fudagala: i amola mu amo ganodini gibu ea logo ga: su da fudagala: le, doasi dagoi.
Katika siku ya kumi na saba ya mwezi wa pili mwaka wa 600 wa kuishi kwake Noa, siku hiyo ndipo chemchemi zote hata zilizo chini sana ya ardhi zilibubujika kwa nguvu, na malango ya mafuriko ya mbinguni yakafunguliwa.
12 Eso 40 amola gasi 40 amoga gibu da osobo bagadega sa: i.
Mvua ikanyesha juu ya nchi siku arobaini usiku na mchana.
13 Amo esoga, Nowa: amola egefe udiana Sieme, Ha: me amola Ya: ifede, ea uda amola egefe ilia uda huluane da dusagaiga fila heda: i.
Siku hiyo Noa, na mkewe, na wanawe Shemu, Hamu na Yafethi pamoja na wake zao wakaingia katika ile safina.
14 Ilia da ohe fi hisu hisu, lai gebo amola sigua amola sania fi ilia osoboga sugi ahoa, amola sio fi huluane ilia da ougiga hagili ahoabe, amo huluane ilia da ganodini oule asi.
Nao walikuwa pamoja na kila mnyama wa mwituni kufuatana na aina yake, wanyama wote wafugwao kufuatana na aina zao, kila kiumbe kitambaacho juu ya ardhi kwa aina yake, na kila ndege kufuatana na aina yake, naam kila kiumbe chenye mabawa.
15 Gawali, aseme amola esalebe liligi huluane da mifo laha, amo huluane da Nowa: ma misini, dusagaiga fila heda: i.
Viumbe vyote vyenye pumzi ya uhai ndani yake vikaja kwa Noa viwili viwili, vikaingia katika safina.
16 Ohe fi da ganodini ahoa amo huluane da gawali, aseme amola esalebe liligi huluanedafa, Gode da Nowa: ma sia: i amo defele. Amalalu, Nowa: da ganodini asi amola Gode da dusagai logo ga: si dagoi.
Wanyama walioingia katika safina walikuwa wa kiume na wa kike, wa kila kiumbe chenye uhai kama Mungu alivyomwamuru Noa, ndipo Bwana akamfungia ndani.
17 Gibu bagade da osobo bagadega sa: ili, eso 40 amanega dalu. Hano da leda: le, dusagai gaguia gadole bila sedagawane gado heda: i.
Kwa siku arobaini mafuriko yaliendelea kujaa duniani na maji yalivyozidi kuongezeka, yaliinua safina juu sana kutoka kwenye uso wa nchi.
18 Hano da bagade hamoi amola bagade heda: i. Dusagai da hano da: iya mae magufale lalu.
Maji yakajaa na kuongezeka sana juu ya nchi, na safina ikaelea juu ya uso wa maji.
19 Hano da bagade heda: le, goumi huluane mu haguduga dialu da dedeboi dagoi ba: i.
Maji yakazidi kujaa juu ya nchi, yakaifunika milima yote mirefu chini ya mbingu yote.
20 Hano bagade heda: le, goumi huluane dedebole, bu 7 mida agoane heda: i.
Maji yakaendelea kujaa yakaifunika milima kwa kina cha zaidi ya dhiraa kumi na tano.
21 Osobo bagadega esalebe liligi huluane, amo lai gebo, sogega esalu ohe fi, sio fi amola dunu fi huluane da bogogia: i dagoi.
Kila kiumbe hai kitambaacho juu ya nchi kikaangamia: Ndege, wanyama wa kufugwa, wanyama pori, viumbe vyote juu ya nchi na wanadamu wote.
22 Liligi huluane da hafoga: i osobo bagadega esalu amola mifo lasu, amo huluane da bogogia: i dagoi.
Kila kiumbe juu ya nchi kavu chenye pumzi ya uhai kikafa.
23 Osobo bagadega esalebe liligi huluane da fadegale fasi dagoi ba: i. Dunu, ohe fi, osoboga sugi ahoasu liligi amola sio fi osobo bagadega hame ba: i. Be Nowa: hi fawane amola ea sosogo fi dusagai ganodini esalu, ilia fawane esalebe ba: i.
Kila kitu chenye uhai juu ya uso wa nchi kilifutiliwa mbali, watu, wanyama, viumbe vitambaavyo na ndege warukao angani wakafutiliwa mbali toka duniani. Waliobaki ni Noa peke yake na wale waliokuwa pamoja naye ndani ya safina.
24 Hano bagade da osobo bagade dedeboi dialu eso 150 agoane dialebe ba: i.
Maji yakaifunika dunia kwa siku 150.