< Gadili Asi 13 >

1 Hina Gode da Mousesema amane sia: i,
Bwana akamwambia Mose,
2 “Magobo dunu mano huluane, Na ouligima: ne Nama ima. Bai Isala: ili dunu mano magobo huluane amola ohe fi magobo gawali huluane da Na:
“Niwekeeni wakfu kila mzaliwa wa kwanza wa kiume. Kila mtoto wa kwanza aliye kifungua tumbo miongoni mwa Waisraeli ni mali yangu, akiwa wa mwanadamu au wa mnyama.”
3 Mousese da Isala: ili dunu ilima amane sia: i, “Wali eso mae gogolema. Dilia da Idibidi ganodini se nabawane udigili hawa: hamosu dunu esalu. Be wali eso dilia da gadili misi. Hina Gode Ea gasa bagade amoga dili fisili masa: ne asunasi. Agi yisidi sali amo mae moma.
Ndipo Mose akawaambia watu, “Ikumbukeni siku hii, siku ambayo mlitoka katika nchi ya Misri, katika nchi ya utumwa, kwa sababu Bwana aliwatoa humo kwa mkono wenye nguvu. Msile chochote kilichotiwa chachu.
4 Dilia da wali eso oubi age amoga (oubi dio da Abibi) Idibidi soge yolesili gadili ahoa.
Leo, katika mwezi wa Abibu, mnatoka.
5 Hina Gode da dafawane sia: i. E da Ga: ina: naide, Hidaide, A:moulaide, Haifaide amola Yebusaide amo dunu fi huluane ilia soge dilima imunu ilegele sia: i. E da dili amo soge noga: idafa amoga oule ahoasea, dilia da wali lolo nabe gilisisu ode huluane oubi age amoga hamoma.
Bwana atakapokuleta katika nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Wahivi na Wayebusi, nchi aliyowaapia baba zako kukupa, nchi itiririkayo maziwa na asali, utaiadhimisha sikukuu hii katika mwezi huu:
6 Eso fesuale amoga dilia yisidi hame sali agi fawane moma. Eso fesu amoga dilia Hina Godema nodomusa: gilisima.
Kwa siku saba utakula mikate isiyotiwa chachu na katika siku ya saba utamfanyia Bwana sikukuu.
7 Eso fesuale ganodini dilia yisidi sali agi maedafa moma. Dilia soge ganodini, yisidi amola agi yisidi sali liligi da sema bagade.
Kwa muda wa siku saba utakula mikate isiyotiwa chachu, pasionekane kitu chochote kilicho na chachu miongoni mwako, wala chachu yoyote isionekane popote ndani ya mipaka yako.
8 Ode huluane, amo gilisisu dilia hemosea, dilia egefe ilima dilia da Hina Gode Ea dili Idibidi yolesili gadili masa: ne fidisu amo dawa: ma: ne, agoane hamoma amo dilia egefelali ilima olelema.
Siku ile utamwambia mwanao, ‘Nafanya hivi kwa sababu ya jambo ambalo Bwana alinitendea nilipotoka katika nchi ya Misri.’
9 Amo gilisisu da dilima liligi dilia loboga o odagiga ga: i agoai gala ba: mu. Dilia da Hina Gode Ea hou (E da Ea gasa bagade amoga dili Idibidi sogega fisili masa: ne asunasi) amo bu dawa: sea, dilia da Hina Gode Ea hamoma: ne sia: i idimu amola dawa: ma: ne sia: mu.
Adhimisho hili, litakuwa kama alama kwenye mkono wako na ukumbusho katika paji lako la uso, kwamba sheria ya Bwana inapaswa iwe kinywani mwako. Kwa kuwa Bwana alikutoa katika nchi ya Misri kwa mkono wake wenye nguvu.
10 Dilia eso ilegei ode huluane amoga, amo lolo nabe gilisisu hamoma.
Ni lazima uishike amri hii kwa wakati uliopangwa mwaka baada ya mwaka.
11 Hina Gode da dilia aowalali ilima, E da dili Ga: ina: naide fi ilia soge ganodini oule misunu ilegele sia: i. Amo E da hamomu. E da amo soge dilima iasea,
“Baada ya Bwana kukuingiza katika nchi ya Wakanaani na kukupa nchi hiyo, kama alivyokuahidi kwa kiapo na kwa baba zako,
12 dilia da magobo dunu mano huluane Ema ima. Ohe fi magobo gawali huluane da Gode Ea: liligi.
inakupasa kumtolea Bwana mzaliwa wa kwanza wa kila tumbo. Wazaliwa wote wa kwanza wa kiume wa mifugo yako ni mali ya Bwana.
13 Be magobo gawali dougi amo dilia Ema bu bidi lama: mu. Dilia dougi bu lale, sibi mano Godema ima. Be dilia da dougi bu lamu higasea, defea, ea galogoa fima. Dilia dunu magobo mano amo huluane Godema bu bidi lama: mu.
Kila mzaliwa wa kwanza wa punda utamkomboa kwa mwana-kondoo, lakini kama hukumkomboa, utamvunja shingo yake. Kila mzaliwa wa kwanza mwanaume miongoni mwa wana wenu utamkomboa.
14 Hobea, dia gofe da dima amo hou ea bai adole ba: sea, ema bu adole ima, ‘Ninia da musa: Idibidi soge ganodini udigili hawa: hamosu dunu esalu. Be Hina Gode Ea gasa bagade amoga E da nini fisili masa: ne gadili asunasi dagoi.
“Katika siku zijazo, mwanao akikuuliza, ‘Hii ina maana gani?’ Mwambie, ‘Kwa mkono wenye nguvu Bwana alitutoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.
15 Idibidi hina bagade (Felou) da gasa fili ninia fisidigimu higaloba, Hina Gode da magobo dunu mano huluane Idibidi soge ganodini esalu, dunu amola ohe medole legei dagoi. Amaiba: le, ninia da wali ohe mano magobo gawali huluane Godema gobele salasu iaha. Be magobo dunu mano huluane ninia bu bidi laha.
Farao alipokataa kwa ukaidi kuturuhusu kuondoka, Bwana aliua kila mzaliwa wa kwanza wa Wamisri, mwanadamu na wa mnyama. Hii ndiyo sababu ninatoa dhabihu kwa Bwana mzaliwa wa kwanza wa kiume, wa kila tumbo na kumkomboa kila mzaliwa wa kwanza wa wana wangu.’
16 Amo hou ninia hamonana da ninia liligi ninia lobo o odagia ga: i agoai ganumu. Amo dawa: sea, ninia Hina Gode da Ea gasa bagade amoga nini Idibidi soge fisili masa: ne gadili asunasi dagoi dawa: sa.’”
Jambo hili litakuwa kama ishara kwenye mkono wako na kama alama kwenye paji la uso wako, kwamba Bwana alikutoa katika nchi ya Misri kwa mkono wake wenye nguvu.”
17 Idibidi hina bagade (Felou) da Isala: ili dunu gadili masa: ne fisidigiloba, Gode da ili logo dunumuni (amo da hano wayabo bagade bega: Filisidia sogega ahoasu) amoga hame oule asi. Gode da amane dawa: i, “Isala: ili dunu da se nabasea amola gegesu ba: sea, ilia asigi dawa: su sinidigili, Idibidi sogega bu hagimu Na higa: i hodosa.”
Farao alipowaachia watu waende, Mungu hakuwaongoza kufuata njia ipitiayo katika nchi ya Wafilisti, ingawa njia hiyo ilikuwa fupi zaidi. Kwa maana Mungu alisema, “Wakikabiliana na vita, wanaweza kubadili mawazo yao na kurudi Misri.”
18 Amaiba: le E da guga: loi ahoasu amo da wadela: i hafoga: i sogega asili Maga: me Hanoga doaga: musa: , amo logoga oule asi. Isala: ili dunu da ilia gegesu liligi gaguiwane ahoasu.
Kwa hiyo Mungu akawaongoza watu kupitia njia ya kuzunguka kupitia jangwani, kuelekea Bahari ya Shamu. Waisraeli walipanda kutoka nchi ya Misri wakiwa wamejiandaa kwa vita.
19 Mousese da Yousefe ea bogoi da: i hodo gaguli asi. Yousefe da esaloba, e da Isala: ili dunuma amane sia: i dagoi, “Gode da dili gaga: sea, amola dilia ga ahoasea, na da: i hodo amola gaguli masa.”
Mose akachukua mifupa ya Yosefu kwa sababu Yosefu alikuwa amewaapisha wana wa Israeli. Alikuwa amewaambia, “Hakika Mungu atakuja kuwasaidia, nanyi ni lazima mwiichukue mifupa yangu mwende nayo kutoka mahali hapa.”
20 Isala: ili dunu da Sagode moilai yolesili, asili, wadela: i hafoga: i soge bega: doaga: i. Ilia da Ida: me sogega abula diasu gilisisu gaguli, ouesalu.
Baada ya Waisraeli kuondoka Sukothi wakapiga kambi huko Ethamu pembeni mwa jangwa.
21 Esoga, Hina Gode da mumobi mogomogoi amo ganodini logo olelemusa: , ili bisili asi. Amola gasi ganodini E da lalu sawa: mogomogoi ganodini ilima hadigi olelemusa: bisili asi. Amalalu, ilia da eso amola gasia amoga hahawane ahoasu.
Wakati wa mchana Bwana aliwatangulia kwa nguzo ya wingu kuwaongoza katika njia yao, na wakati wa usiku aliwatangulia kwa nguzo ya moto kuwaangazia, ili waweze kusafiri mchana au usiku.
22 Eso huluane, mumobi mogomogoi da Isala: ili dunu bisili ahoanebe ba: i. Amola gasia huluane lalu sawa: mogomogoi agoane ili bisili ahoanebe ba: i.
Ile nguzo ya wingu wakati wa mchana au ile nguzo ya moto wakati wa usiku haikuondoka mahali pake mbele ya watu.

< Gadili Asi 13 >