< Mousese Ea Malasu 34 >
1 Mousese da Moua: be umi soge yolesili, Nibou Goumi sogega asi. Amogawi e da Bisiga Goumi (Yeligou moilai bai bagadega gusu gala) amoba: le heda: i. Amogawi Hina Gode da soge huluane ema olelei amane; Gilia: de soge amo da asili, ga (north) asili Da: ne moilaiga doaga: i;
Kisha Mose akaupanda mlima Nebo kutoka tambarare za Moabu mpaka kilele cha Pisga, ngʼambo ya Yeriko. Huko Bwana akamwonyesha nchi yote: kutoka Gileadi mpaka Dani,
2 Na: fadalai soge huluane; Ifala: ime amola Mana: se ilia soge; Yuda fi ilia soge amo da asili, Medidela: inia Hano Wayabo Bagade guma: goe doaga: i;
Naftali yote, nchi ya Efraimu na Manase, nchi yote ya Yuda mpaka bahari ya magharibi,
3 Yuda fi ilia ga (south) soge, umi soge amo da Soua moilai bai bagadega asili Yeligou moilai bai bagade (amo ganodini da fasela agoane ifa bagohame ba: i) amoga doaga: sa.
Negebu na nchi yote kuanzia Bonde la Yeriko, Mji wa Mitende, hadi Soari.
4 Amalalu, Hina Gode da Mousesema amane sia: i, “Amo da soge Na da hemonega A: ibalaha: me, Aisage amola Ya: igobe amo iligaga fi ilima imunu ilegele sia: i. Di amo soge ba: mu, amo Na da olelei dagoi. Be di da amo ganodini hame masunu.”
Kisha Bwana akamwambia, “Hii ndiyo nchi niliyomwahidi Abrahamu na Isaki na Yakobo kwa kiapo niliposema, ‘Nitawapa wazao wako.’ Nimekuruhusu uione kwa macho yako, lakini hutavuka kuingia.”
5 Amalalu, Mousese, Hina Gode Ea hawa: hamosu dunu, da amo Moua: be soge ganodini, Hina Gode Ea sia: i defele, bogoi dagoi.
Naye Mose mtumishi wa Bwana akafa huko Moabu, kama Bwana alivyokuwa amesema.
6 Hina Gode Hisu da Moua: be umi sogebi Bedebio moilai gadenene la: ididili amo ganodini Mousese ea da: i hodo uli dogone sali. Be dunu da ea uli dogoi sogebi hame dawa: i, amola wali hame dawa:
Mungu akamzika huko Moabu, katika bonde mkabala na Beth-Peori, lakini hakuna ajuaye kaburi lake lilipo mpaka leo.
7 120Mousese da lalelegele, ode120 gidigili bogoi. Be e bogoloba, ea si da wadela: i hame amola ea gasa da hame wadela: lesi.
Mose alikuwa na umri wa miaka mia moja na ishirini alipofariki; hata hivyo nguvu ya macho yake haikufifia wala mwili wake haukudhoofika.
8 Isala: ili dunu da Mousese dawa: beba: le, eso 30 Moua: be umi amo ganodini didiga: su olei defele didiga: lalu yolesi.
Waisraeli wakaomboleza kwa ajili ya Mose kwenye tambarare za Moabu kwa siku thelathini, mpaka wakati wa kulia na kuomboleza ulipopita.
9 Amola Yosiua (Nane egefe) da asigi dawa: su noga: i amoga nabai galu. Bai Mousese da ema ea lobo ligisi galu. Amaiba: le, Isala: ili dunu da ea sia: nabasu. Ilia da Hina Gode Ea hamoma: ne sia: i E da Mousesema olelei, amoma fa: no bobogei.
Basi Yoshua mwana wa Nuni alijazwa roho ya hekima kwa sababu Mose alikuwa ameweka mikono yake juu yake. Kwa hiyo Waisraeli wakamsikiliza na wakafanya yale ambayo Bwana alikuwa amemwagiza Mose.
10 Fa: no agoane, balofede dunu Mousese defele da Isala: ili soge ganodini hame heda: i. Hina Gode da Mousese ea odagia moloiwane sia: su.
Tangu wakati huo, katika Israeli hajainuka nabii mwingine kama Mose, ambaye Bwana alimjua uso kwa uso,
11 Hina Gode da e asunasiba: le, e da Idibidi soge ganodini musa: hame ba: i dawa: digima: ne olelesu amola hou eno hamosu. E da amo hou Felou amola ea ouligisu dunu amola Idibidi dunu huluane ilima amane hamoi. Mousese bagia, balofede dunu afae da ea hou defele hamedafa hamosu.
aliyetenda ishara zote zile za miujiza na maajabu ambayo Bwana alimtuma kuyatenda huko Misri, yaani kwa Farao na maafisa wake wote na nchi yake yote.
12 Mousese da Isala: ili dunu huluane ba: ma: ne gasa bagadedafa beda: ma: ne amola hamomu hamedei liligi hamoi. Fa: no agoai, balofede dunu eno da amo hou defele hamomu da hamedei. Sia: Ama Dagoi
Kwa kuwa hakuna mtu yeyote aliyewahi kuonyesha nguvu nyingi ama kutenda matendo ya kutisha ambayo Mose aliwahi kuyafanya mbele ya Israeli yote.