< Mousese Ea Malasu 30 >

1 Na da wali logo aduna dilima olelei. Afae da Hahawane dogolegele aligima: ne logo, eno da gagabusu aligima: ne logo. Na sia: i liligi da dilima doaga: sea, amola dilia da ga fi (amoga Hina Gode da dili afagogomu) amo ganodini esalea, dilia da logo aduna na da dilima olelei amo bu dawa: mu.
Wakati baraka hizi zote pamoja na laana nilizoziweka mbele yako zitakapokujia, nawe ukazitafakari moyoni popote Bwana Mungu wako atakapokutawanya miongoni mwa mataifa,
2 Dilia amola diligaga fi da Hina Godema bu sinidigisia amola Ea hamoma: ne sia: i na da wali eso dilima olelesa amo noga: le nabawane hamosea,
hapo wewe na watoto wako mtakapomrudia Bwana Mungu wako, na kumtii kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote kulingana na kila kitu ninachokuamuru leo,
3 amasea dilia Hina Gode da dili gogolema: ne olofomu. E da fifi asi gala amoga E da dili afagogomu, amoga E da bu fadegale, dilia sogega bu oule misini, dili bu hahawane bagade gaguiwane esaloma: ne fidimu.
ndipo Bwana Mungu wako atakapokurudisha kutoka utumwani na kukuhurumia, naye atakukusanya tena kutoka mataifa yote kule alikutawanya.
4 Dilia da osobo bagade bega: bega: afagogoi ba: sea, dilia Hina Gode da dili bu gilisili, buhagima: ne oule misunu.
Hata kama umefukuziwa katika nchi ya mbali kiasi gani chini ya mbingu, kutoka huko Bwana Mungu wako atakukusanya na kukurudisha.
5 Amasea, dilia da soge amo ganodini dilia aowalali da musa: esalu, amo ganodini dilia da bu fimu. Amola dilia hou huluane amola dilia idi da dilia aowalali ilia musa: hou amola idi bagadewane baligimu.
Yeye Bwana atakurudisha katika nchi iliyokuwa mali ya baba zako, nawe utaimiliki. Naye atakufanya ufanikiwe sana na kukuzidisha kwa idadi kuliko baba zako.
6 Dilia Hina Gode da nabasu dogo amo dilima amola diligaga fi ilima imunu. Amaiba: le, dilia da dilia dogo huluane amoga Godema asigimu amola dilia da amo soge ganodini esalalalumu.
Bwana Mungu wako ataitahiri mioyo yenu na mioyo ya wazao wenu ili mweze kumpenda kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote ukaishi.
7 Amola E da gagabusu huluane sinidigili, dilima ha lai ilia dili bagadewane higasu amola se iasu, E da amo gagabusu aligima: ne ilima imunu.
Bwana Mungu wako ataweka laana hizi zote juu ya adui zako ambao wanakuchukia na kukutesa.
8 Amola dilia da bu Ema nabasu hou hamomu amola Ea hamoma: ne sia: i huluane na da wali eso dilima olelesa, amo huluane nabawane hamomu.
Utamtii tena Bwana na kuzishika amri zake zote ninazokupa leo.
9 Hina Gode da dilia labe hou huluane hahawane fidimu. Dilia da mano bagohame, ohe fi bagohame amola ha: i manu bagade ba: mu. E da hahawane dilia aowalali fidisu amo defele dili fidimuba: le, hahawane ba: mu.
Ndipo Bwana Mungu wako atakapokufanikisha sana katika kazi zote za mikono yako na katika uzao wa tumbo lako, wadogo wa mifugo yako na mazao ya nchi yako. Bwana atakufurahia tena na kukufanikisha, kama alivyowafurahia baba zako,
10 Be dilia da Ea sia: noga: le nabasea amola Ea sema huluane Ea olelesu buga ganodini dedei amoga noga: le fa: no bobogesea fawane, amo hahawane hou ba: mu. Dilia da dilia dogo huluane amoga Ema sinidigisia, amo hou ba: mu.
kama ukimtii Bwana Mungu wako, na kuzishika amri zake na maagizo yake ambayo yameandikwa katika Kitabu hiki cha Sheria, na kumgeukia Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote.
11 Hamoma: ne sia: i na da wali eso dilima olelelala da gasa bagade hame amola dilima hamedei liligi hame.
Ninachokuagiza leo sio kigumu sana kwako au usichokiweza.
12 Amo sia: da muagado hame gala. Dilia amo dawa: ma: ne, ‘Nowa da muagado heda: le amo sia: ninia nabima: ne gaguli misa: bela: ?’ amane sia: mu da hamedei.
Hakiko juu mbinguni, ili uulize, “Ni nani atakayepanda mbinguni kukileta na kututangazia ili tuweze kutii?”
13 Amola amo sia: da hano wayabo bagade na: iyado bega: hame gala. Dilia da amo dawa: ma: ne, ‘Nowa da hano wayabo bagade degele, amo sia: ninia nabalu fa: no bobogemusa: gaguli misa: bela: ?’ amo sia: mu da hamedei.
Wala hakiko ngʼambo ya bahari, ili uulize, “Ni nani atakayevuka bahari kwenda kukichukua na kututangazia ili tupate kutii?”
14 Hame mabu! Amo sia: da dilima gadenene diala. Dilia noga: le nabima: ne, amo sia: da dilia lafi ganodini amola dilia dogo ganodini diala.
La hasha! Lile neno liko karibu sana nawe; liko kinywani mwako na ndani ya moyo wako ili uweze kulitii.
15 Na da wali logo aduna dilia afae lalegaguma: ne, dilima olelesa. Logo afae da noga: i, eno da wadela: i. Afae da Esalusu, eno da Bogosu.
Tazama, naweka mbele yako leo uzima na mafanikio, mauti na maangamizo.
16 Dilia da dilia Hina Gode amo Ea hamoma: ne sia: i na da wali eso dilima olelesa amo nabasea, dilia da Ema asigisia, Ema nabasu hou hamosea amola Ea sema amola hamoma: ne sia: i huluane amoma fa: no bobogesea, amasea dilia labe hou huluane da hahawane heda: mu amola dilia idi da bagade heda: mu. Dilia Hina Gode da soge amoga dilia da gesowale fimu amo ganodini dili hahawane dogolegelewane fidimu.
Ninakuamuru leo kwamba umpende Bwana Mungu wako, utembee katika njia zake, na kutunza maagizo yake, amri na sheria zake; ndipo utakapoishi na kuongezeka, naye Bwana Mungu wako atakubariki katika nchi unayoingia kuimiliki.
17 Be dilia da hame nabasea, amola nabasu hou higasea amola eno dunu fa: no bobogebeba: le, eno ogogosu ‘gode’ liligi ilima nodone sia: ne gadosea,
Lakini kama moyo wako ukigeukia mbali ukawa huna utii, kama umevutwa kuisujudia miungu mingine na kuiabudu,
18 na da wali guiguda: sisasu dilima olelesa. Dilia da gugunufinisi dagoi ba: mu. Amo soge Yodane Hano bega: dilia da gesowale fimu, amo ganodini dilia ode bagahame fawane esalumu.
nakutangazia leo hii kwamba hakika utaangamizwa. Hutaishi maisha marefu katika nchi unayovuka Yordani kuiingia na kuimiliki.
19 Amaiba: le, na da wali dili afae lalegaguma: ne logo aduna olelesa. Afae da Esalusu, eno da Bogosu. Afae da Gode Ea hahawane dogolegelewane fidisu, eno da Gode Ea gagabusu aligima: ne ilegesu. Wali, na da Hebene amola osobo bagade amoma ilia fedege sia: agoane amo dilima hou ba: su dunu elama wele sia: sa. Amaiba: le, dilia Esalusu lalegaguma.
Leo ninaziita mbingu na nchi kama mashahidi dhidi yako kwamba nimeweka mbele yako uzima na mauti, baraka na laana. Basi sasa chagueni uzima, ili wewe na watoto wako mpate kuishi,
20 Dilia Hina Godema asigima! Ema nabasu hou hamoma amola mae yolesima! Amasea, dilia amola diligaga fi da ode bagohame, soge amo Hina Gode da dilia aowalali eda A: ibalaha: me, Aisage amola Ya: igobe ilima imunu ilegele sia: i, amo ganodini esalumu.
na ili upate kumpenda Bwana Mungu wako, uisikilize sauti yake na kuambatana naye. Kwa kuwa Bwana ndiye uzima wako, na atakupa wingi wa siku ili upate kuishi katika nchi aliyoapa kuwapa baba zako Abrahamu, Isaki na Yakobo.

< Mousese Ea Malasu 30 >