< Mousese Ea Malasu 17 >

1 Dilia Hina Godema gobele salimusa: , wadela: i o bahoi bulamagau o sibi mae ima. Hina Gode da amo hou higasa.
Msimtolee Bwana Mungu wenu dhabihu ya maksai au kondoo ambaye ana dosari yoyote au hitilafu ndani yake, kwa kuwa hilo litakuwa chukizo kwake.
2 Dilia moilai amo ganodini dunu o uda afae da Hina Godema wadela: le hamosea amola Ea gousa: su gugunufinisisia,
Ikiwa mwanaume au mwanamke anayeishi kati ya mojawapo ya miji akupayo Bwana, anakutwa anafanya uovu mbele za Bwana Mungu wenu, kwa kuvunja Agano lake,
3 e da eno ogogosu ‘gode’ liligi o eso o oubi o gasumuni, Gode Ea sia: wadela: musa: ilima nodone sia: ne gadosea,
naye amekwenda kinyume na agizo langu kuabudu miungu mingine na kuisujudia, kama vile jua, mwezi au nyota za angani,
4 amo sia: nabasea, dilia bai dawa: ma: ne noga: le hogoma. Amo wadela: i hou da dafawane Isala: ili soge ganodini hamoi dagoi ba: sea,
hili likiwa limeletwa mbele yenu, ni lazima kulichunguza kikamilifu. Ikiwa ni kweli na kuwa limehakikishwa kwamba hili ni chukizo lililofanyika katika Israeli,
5 amo dunu moilai gadili oule asili, igiga gala: le, medole legema.
mchukueni huyo mwanaume au mwanamke ambaye amelifanya tendo hili ovu kwenye lango la mji wenu na kumpiga mawe mtu huyo mpaka afe.
6 Be hedolo mae medole legema. Ba: su dunu aduna o aduna baligi da ea wadela: i hou dafawane ba: i dagoiba: le fawane, medole legema. Be dunu afae fawane da ba: su dunu esalea, mae medole legema.
Kwa ushuhuda wa mashahidi wawili au watatu mtu huyo atauawa, bali hakuna mtu atakayeuawa kwa ushuhuda wa shahidi mmoja tu.
7 Ba: su dunu da degabo amo dunu medole legema: ne, igiga gala: ma: ma. Amasea, dunu huluane da amo igiga medomu. Amasea, dilia da wadela: i hou Isala: ili amo ganodini fadegale fasimu.
Ni lazima kwanza mikono ya mashahidi itangulie kumuua huyo mtu, kisha mikono ya watu wote. Ni lazima mwondoe uovu miongoni mwenu.
8 Be moilai fofada: su dunu da fofada: su eno da ilima hamedei agoane ba: sea - amo da medole legesu o sogega gegesu o fasu - dilia da amo dunu dilia Hina Gode Ea ilegei sogebi amoga oule masa.
Kama mashauri yanaletwa katika mahakama zenu ambayo ni magumu zaidi kwenu kuyaamua, ikiwa ni umwagaji wa damu, madai au mashambulio, yapelekeni mahali ambapo Bwana Mungu wenu atapachagua.
9 Dilia gobele salasu dunu (Lifai dunu) amola fofada: su dunu bagade amoga adole ba: musa: masa. Ilia da fofada: lalu, sia: dilima olelemu.
Nendeni kwa makuhani, ambao ni Walawi, na kwa mwamuzi ambaye atakuwa kazini wakati huo. Ulizeni kwao nao watawapa maamuzi.
10 Ilia da Hina Gode Ea ilegei sogebi amogawi dilima hou olelemu. Dawa: ma! Dilia ilia sia: huluane defele hamoma.
Ni lazima mtende sawasawa na maamuzi watakayowapa mahali Bwana atakapopachagua. Kuweni waangalifu kufanya kila kitu watakachowaongoza kufanya.
11 Ilia da sema amola hou huluane dilima olelemu. Ilia olelei defele, noga: le hamoma. Lobodafa la: ididili o lobo fofadi la: ididili amoga mae masa be moloidafa gusuba: i masa.
Fanyeni sawasawa na sheria wanayowafundisha na maamuzi wanayowapa. Msigeuke mkono wa kuume au kushoto kuacha kufanya yale wanayowaambia.
12 Be nowa dunu da fofada: su bagade dunu o gobele salasu dunu (amo da Godema hawa: hamonana) amo higasea, amo dunu dilia medole legema. Amo wadela: i hou Isala: ili fi ganodini diala, dilia fadegale fasima.
Mwanaume atakayeonyesha dharau kwa mwamuzi au kwa kuhani ambaye amewekwa kumtumikia Bwana Mungu wenu lazima auawe. Lazima mwondoe uovu katika Israeli.
13 Dunu huluane da amo hou nababeba: le, beda: mu. Amasea, ilia da amo higasu hou bu hame hamomu.
Watu wote watasikia na kuogopa, nao hawatakuwa wenye kudharau tena.
14 Dilia da soge amo dilia Hina Gode da dilima iaha amo ganodini fi dagosea, dilia da na: iyado fi dilima gadenene esala defele hina bagade dunu ilegemusa: dawa: mu.
Wakati utakapoingia katika nchi anayowapa Bwana Mungu wenu kuimiliki na kukaa humo, nanyi mkasema, “Na tumweke mfalme juu yetu kama mataifa yanayotuzunguka,”
15 Be dilia hina bagade ilegemusa: dawa: sea, noga: le dawa: ma! Hina Gode Ea ilegei dunu fawane lama. Dilia fidafa dunu fawane lama. Ga fi dunu amo maedafa ilegema.
kuweni na uhakika wa kumweka mfalme juu yenu ambaye Bwana Mungu wenu atamchagua. Ni lazima atoke miongoni mwa ndugu zenu wenyewe. Msimweke mgeni juu yenu ambaye si ndugu wa Kiisraeli.
16 Amo hina bagade dunu da hosi bagohame hame gagumu. Amola e da ea fi dunu hosi bidi lama: ne Idibidi sogega hame asunasimu. Bai Hina Gode da Ea fi dunu da Idibidi sogega hamedafa buhagima: ne sia: i dagoi.
Hata hivyo, kamwe mfalme asijipatie hesabu kubwa ya farasi kwa ajili yake mwenyewe, au kuwafanya watu warudi Misri ili kupata farasi zaidi, kwa maana Bwana amekuambia, “Hamtairudia njia ile tena.”
17 Hina bagade dunu da uda bagohame, amo hame lama: mu. Bai e da Hina Gode Ea hou fisisa: besa: le, uda eno hame lama: mu. E da silifa, gouli amola muni bagade hame lama: mu.
Kamwe asioe wake wengi, la sivyo moyo wake utapotoka. Kamwe asijilimbikizie kiasi kikubwa cha fedha na dhahabu.
18 E da hina bagade hawa: hamosu lalegagusia, e da Gode Ea sema amola Ea olelesu (amo Lifai gobele salasu dunu ilia gagusa) amo huluane dedene gaguma: mu.
Atakapokuwa amekalia kiti cha ufalme wake, ajiandikie kwenye kitabu nakala ya sheria kwa ajili yake mwenyewe kutoka zile sheria za makuhani ambao ni Walawi.
19 E da amo buga lalegaguli, eso huluane idilalumu. Amasea, e da amo dawa: le Hina Godema nodone dawa: mu amola mae yolesili, Gode Ea sia: defele lalumu.
Atakuwa na nakala hiyo, naye ataisoma siku zote za maisha yake ili kwamba ajifunze kumheshimu Bwana Mungu wake na kufuata kwa uangalifu maneno yote ya sheria hii na amri hizi,
20 Amasea, e da gasa fi hou mae hamone, ea hou da ea na: iyado Isala: ili fi amo baligisa e da hame dawa: mu. E da Gode Ea sia: amo giadofamu da hamedei ba: mu. E da hina bagade ouligisu hou ode bagohame hamoma: mu. Amola ea mano da Isala: ili dunu ilima hina bagade ouligisu dunu ode bagohame esalumu.
naye asijifikirie kuwa ni bora kuliko ndugu zake na kuipotosha sheria. Ndipo yeye na wazao wake watatawala katika ufalme wake kwa muda mrefu katika Israeli.

< Mousese Ea Malasu 17 >