< 2 Hou Olelesu 16 >

1 Yuda hina bagade A: isa ea ouligibi ode36 amoga, Isala: ili hina bagade Ba: iasia da Yuda soge doagala: le, golili sa: ili, e da Yuda gadili ahoasu logo ga: ma: ne, muni La: ima moilai gagili sali.
Katika mwaka wa thelathini na sita wa utawala wa Asa, Mfalme Baasha wa Israeli akashambulia Yuda na kuweka ngome mji wa Rama ili kumzuia yeyote asitoke wala kuingia nchi ya Mfalme Asa wa Yuda.
2 Amaiba: le, hina bagade A: isa da silifa amola gouli huluane Debolo amola hina bagade diasu amo ganodini hame lai dialebe ba: i, amo lale, eagene ouligisu dunu ilia Dama: saga: se moilai bai bagade, Silia hina bagade Beneha: ida: de (Da: balimone egefe amola Hisione ea aowa) amoma imunusa: gaguli masa: ne sia: i. Amola e da ilia ema amane sia: ma: ne sia: si,
Ndipo Asa akachukua fedha na dhahabu kutoka hazina ya Hekalu la Bwana na kutoka jumba lake mwenyewe la kifalme na kumpelekea Ben-Hadadi mfalme wa Aramu, ambaye alikuwa anatawala huko Dameski.
3 “Ani da anianini, ania adalali defele, dogolegemu da defea. Amo silifa amola gouli da digili hahawane dogolegele iasu. Wali di amola Isala: ili hina bagade Ba: iasia alialisu gousa: su hamoi amo damuma. Amasea, e da ea dadi gagui na soge ganodini asunasili esala, amo fadegale fasimu.”
Akasema, “Pawepo na mkataba kati yangu na wewe, kama ulivyokuwepo kati ya baba yangu na baba yako. Tazama, nimekuletea fedha na dhahabu. Sasa vunja mkataba wako na Baasha mfalme wa Israeli ili aniondokee mimi.”
4 Hina bagade Beneha: ida: de da A: isa ea sia: i hahawane ba: i. Amaiba: le, e da ea dadi gagui wa: i ouligisu dunu amola dadi gagui dunu ilia Isala: ili moilale gagale fi amo ili doagala: ma: ne, asunasi. Ilia da Aidione, Da: ne, A:ibele Bede Ma: iga moilale gagai, amola Na: fadalai soge moilai bai bagade huluane (amo ganodini ilia liligi ligisisu) fefedele lai.
Ben-Hadadi akakubaliana na Mfalme Asa na kutuma majemadari wa majeshi yake dhidi ya miji ya Israeli. Wakashinda Iyoni, Dani, Abel-Maimu na miji yote ya hazina ya Naftali.
5 Hina bagade Ba: iasia da amo hamoi sia: nababeba: le, La: ima moilai gagili salalu, amo yolesili, fisili asi.
Baasha aliposikia jambo hili, akasimamisha kujenga Rama na kuacha kazi yake.
6 Amalalu, hina bagade A: isa da Yuda soge ganodini amo dunu huluanedafa da gele amoga Ba: iasia da La: ima gagili sali, amo gaguli masa: ne sia: si. Amo liligi lale, A:isa da Bediamini soge moilai bai bagade Giba amola Misiba moilai bai bagade, amo gagili sali.
Ndipo Mfalme Asa akawaleta watu wote wa Yuda, nao wakachukua mawe na miti ambayo Baasha alikuwa anavitumia huko Rama. Kwa vitu hivyo akajenga Geba na Mispa.
7 Amogalu, balofede dunu Hana: inai da hina bagade A: isama asili, amane sia: i, “Di da Hina Gode Ea fidisu dafawaneyale mae dawa: le, be Silia hina bagade ea fidisu fawane lai dagoiba: le, Isala: ili hina bagade ea dadi gagui wa: i da diba: le hobea: i dagoi.
Ikawa wakati huo mwonaji Hanani akamjia Mfalme Asa wa Yuda na kumwambia: “Kwa sababu ulimtegemea mfalme wa Aramu nawe hukumtegemea Bwana Mungu wako, jeshi la mfalme wa Aramu limeponyoka mkononi mwako.
8 Idioubia dunu amola Libia dunu ilia dadi gagui wa: i amolawane da bagadedafa ba: i, amola ilia sa: liode amola hosiga fila heda: i dunu da bagohame ba: i. Be di da Hina Gode Ea fidisu hou dafawaneyale dawa: beba: le, E da dima hasalasu hou i dagoi.
Je, hukumbuki lililotendeka kwa Wakushi na Walibia, hawakuwa jeshi lenye nguvu na magari mengi ya vita na wapanda farasi? Hata hivyo, ulipomtegemea Bwana yeye aliwatia mkononi mwako.
9 Hina Gode da osobo bagade fi huluane dadawa: le sosodo ouligisa. Amola E da nowa dunu Ema madelagi amola hame hagasea, ema gasa iaha. Di da gagaoule hamoi dagoi. Amaiba: le, wahawinini, di da gegenana ahoanumu.”
Kwa kuwa macho ya Bwana hukimbiakimbia duniani kote ili kujionyesha mwenye nguvu kwa ajili ya wale ambao mioyo yao inamtegemea kwa ukamilifu. Umefanya jambo la upumbavu na kuanzia sasa na kuendelea utakuwa na vita.”
10 Amo sia: nababeba: le, A:isa da ougi bagade ba: i. Ea sia: beba: le, ilia da balofede dunu sia: inega lagili yolesi. Amogalu, A:isa da muni Yuda fi dunu mogili ilima dodona: gi hou hamosu.
Asa akamkasirikia mwonaji kwa sababu ya jambo hili. Alikuwa ameghadhibika sana hata akamweka gerezani. Wakati huo huo Asa akaanza kuwatesa na kuwaonea baadhi ya watu kwa ukatili.
11 Hou huluane hina bagade A: isa hamoi, ea muni hamoi asili ea bogosu, amo huluane da “Yuda hina bagade ilia Hamonanu Meloa” amo ganodini dedene legei.
Matukio ya utawala wa Asa, kuanzia mwanzo mpaka mwisho, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.
12 A: isa ea ouligibi ode 39 amoga, e da olobeba: le, emo gasuga: igi. Be amomane, e da Hina Godema hame sinidigi. E da udigili manoma legesu dunu ilima e fidima: ne hogoi.
Katika mwaka wa thelathini na tisa wa utawala wake, Asa alipatwa na ugonjwa kwenye miguu yake. Ingawa ugonjwa wake ulimzidia sana, hata katika kuugua kwake hakutafuta msaada kutoka kwa Bwana bali kwa matabibu tu.
13 E da olole, ode aduna gidigili, bogoi.
Katika mwaka wa arobaini na moja wa utawala wa Asa, alikufa na kulala na baba zake.
14 Ilia da ea da: i hodo amo gele gelabo hisu dogoi Daibidi ea Moilai bai bagadega dialu, amo ganodini sali. Ilia da ha: i manu fodole nasu amola gabusiga: manoma ea da: i hodoma dogone salimusa: momagema: ne legei. Amola ema didigia: musa: , lalu bagadedafa didi.
Nao wakamzika katika kaburi lile alilokuwa amejichongea mwenyewe katika Mji wa Daudi. Wakamzika kwa jeneza lililowekwa vikolezi na mchanganyiko wa manukato ya aina mbalimbali yaliyotengenezwa kwa utaalamu wa mtengeneza marashi, nao wakawasha moto mkubwa kwa heshima yake.

< 2 Hou Olelesu 16 >