< 1 Sa:miuele 14 >

1 Eso afaega Yonada: ne da ayeligi amo da ea gegesu liligi gagagula ahoasu, ema amane adoi, “Anisu Filisidini ilia ha wa: i fisisu amoga ahoa: di” Be Yonada: ne da eda Soloma hame adoi.
Siku moja, Yonathani mwana wa Sauli alimwambia mbeba silaha wake aliye mdogo, “Njoo, hebu twende hadi upande mwingine kwenye ngome ya Wafilisti.” Lakini hakumjulisha baba yake.
2 Solo da Migalone sogebi (Gibia moilai gadenenewane) amoga ‘bomegala: nide’ ifa hagudu esalu. Dunu 600 agoane da e fisili esalu.
Sauli alikuwa akikaa nje ya mji wa Gibea chini ya mti wa mkomamanga ulio katika Migroni. Takribani watu mia sita walikwa pamoja naye,
3 Gobele salasu dunu amo da ‘ifode’ gaguli ahoasu amo da Ahaidia. E da Igabode ea ola Ahaidabe amo ea mano. Ahaidabe da Finia: se, Ilai (Hina Gode Ea gobele salasu dunu Siailou moilaiga esalu) ea mano amo ea aowa galu. Dunu ilia da Yonada: ne da asi dagoi amo hame nabi.
akiwemo Ahiya mwana wa Ahitubu (nduguye Ikabodi) mwana wa Finehasi, mwana wa Eli, kuhani wa BWANA huko Shilo, aliyevaa naivera. Watu hao hawakujua kwamba Yonathani ameondoka.
4 Yonada: ne da Fisilidini ha wa: i fisisuga masusa: dawa: i. Amoga ahoasu logo da Migema: se Adobo Gigiadofa Ahoasu. Amo ahoasu logoga, igi agesoi aduna la: idi la: idili dialebe ba: i. Eno amo ea dio da Bousese, amola eno amo ea dio da Sine.
Katikati ya vichochoro, ambavyo Yonathani alinuia kuvipita hadi ngome ya Wafilisti, kulikuwa na mwamba wenye mteremko mkali upande mmoja, na mteremko mkali upande mwingine. Jabali moja liliitwa Bosesi, na jingine liliitwa Sene.
5 Afae da ga (north) logo bega: amodili Migima: sega ba: legale danu, amola eno da ga (south) logo bega: amodili Gibaga ba: legale danu.
Lile jabali lenye mteremko mkali zaidi liliinuka upande wa kaskazini mbele ya Mikmashi, na jingine upande wa kusini mbele ya Geba.
6 Yonada: ne da goi ayeligi ema amane sia: i, “Ania da galuli Gode Ea hou hame dawa: Filisidini dunu ilia ha wa: i fisisuga ahoa: di. Hina Gode da ani fidima: bela: ? Ani da anisuba: le, mae dawa: ma. Hina Gode da ani fidisia, ani da dafawane ili hasalimu.”
Yonathani akamwambia kijana mbeba silaha, “Njoo, na tuvuke hadi ngome ya hawa wasiotahiriwa. Pengine BWANA atatenda kwa niaba yetu, kwa maana hakuna kitu kiwezacho kumzuia BWANA asiokoe kwa wengi au kwa watu wachache.”
7 Goi ayeligi da bu adole i, “Dia da adi hamomusa: dawa: sea, na da ani galu hamomu. Na da dimagai lela!”
Mbeba silaha wake akajibu, “Fanya kila kitu kilicho ndani ya moyo wako. Songa mbele, tazama, niko pamoja nawe, nitatii maagizo yako yote.”
8 Yonada: ne da amane sia: i, “Defea! Ania da galuli giadofale gale, Filisidini dunu ilia da ani ba: ma: mu.
Ndipo Yonathani akasema, “Tutavuka twende kwa watu hao, na tutajionesha wenyewe kwao.
9 Be ilia da anima ili misa: ne ouligima: ne sia: sea, ani da amogaiwane oulelumu.
Kama watatuambia, 'Subirini hapo hadi tutakapokuja kwenu' - basi tutabaki katika sehemu yetu na hatutavuka kwenda kwao.
10 Be ilia da ani ilima masa: ne sia: sea, ani da ilima masunu. Bai Hina Gode da anima ili hasalima: ne, dawa: digisu olelesa, ania da dawa: digimu.”
Lakini kama watajibu, 'Njoni kwetu,' ndipo tutavuka; kwa sababu BWANA amewaweka mkononi mwetu. Hii ndiyo itakuwa ishara yetu.”
11 Amaiba: le, elea da Filisidini dunu ilia ela ba: ma: ne odagi olei. Amola Filisidini dunu ilia amane sia: i, “Ba: ma! Hibulu dunu oda da ilia wamoaligisu uli dogoi amodili maha.”
Kwa hiyo wote wawili wakajifunua mbele ya ngome ya Wafilisti. Wafilisti wakasema, “Angalia, Webrania wanakuja kutokea kwenye mashimo walimojificha.”
12 Amalalu, ilia da Yonada: ne amola goi ayeligi elama amane wele sia: i, “Guiguda: misa! Ninia da alima adomu gala.” Yonada: ne da goi ayeligima, amane sia: i, “Na bobogema! Hina Gode da Isala: ili dunu ilia Filisidini dunuma hasalima: ne logo doasi dagoi.”
Ndipo watu wa ile ngome wakamwita Yonathani na mbeba silaha wake, wakisema, “Njoni huku kwetu, tutawaonesha jambo fulani.” Na Yonathani akamwambia mbeba silaha wake; “Nifuate nyuma yangu, kwa sababu BWANA amewaweka katika mkono wa Israeli.”
13 Yonada: ne da adobo logodili muguniga lobo ososa: heda: i. Amola ayeligi da e bobogei. Yonada: ne da Filisidini dunu doagala: le, fane sali. Amola goi ayeligi da ili medole legei.
Yonathani alipanda juu kwa mikono na miguu yake, na mbeba silaha akimfuata nyuma yake. Wafilisti waliuwawa mbele ya Yonathani, na mbeba silaha wake akiwaua baadhi nyuma yake.
14 Yonada: ne amola goi ayeligi da sogebi fonobahadi amo ganodini, dunu 20 agoane medole legei.
Hilo shambulio la kwanza walilofanya Yonathani na mbeba silaha wake, waliua watu wapatao ishirini katika urefu wa nusu handaki kwenye eka moja ya ardhi.
15 Filisidini dunu huluane amo soge ganodini esalu da bagadewane beda: gia: i. Fana ahoasu dunu amola dadi gagui dunu ha wa: i fisisuga esalu da beda: ga hesei. Gode da hamobeba: le, osobo da fogole amola dunu huluane da beda: ga bulila lafia: i.
Kukawa na hofu kubwa katika kambi, uwandani, na katika watu. Hata ngome ya jeshi na watekaji nyara nao wakawa na hofu kubwa
16 Solo ea logo sosodo ouligisu dunu da Gibia moilai (Bediamini ea ouligi soge ganodini) amogai Filisidini dunu ilia beda: ga doula lafia: lebe ba: i.
Ndipo walinzi wa Sauli huko Gibea ya Benyamini wakaona kundi la askari wa Wafilisti likitawanyika, wakienda kule na huku.
17 Amaiba: le, Solo da ea dunuma sia: i, “Ninia dadi gagui dunu idili ba: ma. Nowa da hameyale ba: ma!” Ilia da idili ba: loba, Yonada: ne amola ayeligi dunu amo da ea gegesu liligi gagusisu hame ba: i.
Kisha Sauli akawaambia watu aliokuwa nao, “Mjihesabu ili muone nani hayupo hapa.”Walipokuwa wamehesabu, wakagundua kuwa Yonathani na mbebaji wa silaha zake hawapo.
18 Solo da gobele salasu dunu Ahaidia ema amane sia: i, “Gode Ea Gousa: su Sema Gagili gaguli misa. (Amo esoha Abaidia da Gode Ea Gousa: su Sema Gagili amo Isala: ili dunuma bisili gaguli ahoasu.)
Sauli akamwambia Ahiya, “Lete hapa naivera ya Mungu”- kwa maana siku hiyo Ahiya alivaa naivera akiwa pamoja na askari wa Israeli.
19 Solo da gobele salasu dunu ema sia: daloba, Filisidini dunu ilia ha wa: i fisisu dadoula lafia: su da bagadewane alelasi. Amaiba: le, Solo da Ahaidiama amane sia: i, “Hina Godema adole ba: mu da dibi hame gala.”
Wakati Sauli akiongea na kuhani, kelele na ghasia kubwa iliendelea na kuongezeka katika kambi ya Wafilisti. dipo sauli akamwambia kuhani, “Acha kazi unayofanya.”
20 Amalalu, Solo amola ea dadi gagui dunu da mogodigili Filisidini dadi gagui dunu ilima doagala: musa: heda: i. Be Filisidini dunu da dadoula lafia: le, ili gobele gegei.
Sauli na watu wote aliokuwa nao wakajipanga na kwenda kwenye mapigano. Upanga wa kila Mfilisti ulikwa juu ya Mfilisti mwenzake, na kulikuwa na ghasia kubwa.
21 Hibulu dunu mogili da musa: hohonone, Isala: ili ha wa: i fisili, Filisidini dunu amogale gegei. Be amo dunu da sinidigili bu Solo amola Yonada: ne elama bu madelale gegei.
Basi Waebrania ambao mwanzoni walijiunga na Wafilisti, na kwenda kwenye kambi yao, wao pia waliungana na Waisraeli waliokuwa pamoja na Sauli na Yonathani.
22 Hibulu dunu mogili Ifala: ime agolo sogega wamoaligili esalu, da Filisidini dunu da hobeabe nababeba: le, ilia wamoaligisu yolesili, Filisidini dunu doagala: i.
Waisraeli wote waliokuwa wamejificha katika milima karibu na Efraimu waliposikia kwamba Wafilisti wamekimbia, nao pia wakawafuata Wafilisti nakuwafukuza kwenye hiyo vita.
23 Amo esoha, Hina Gode da Isala: ili fi gaga: i dagoi. Amola, ilia da Filisidini dunu se bobogelala, Beda: ifane moilai baligi.
Hivyo siku hiyo BWANA aliwaokoa Israeli, na mapigano yalivuka kupitiliza Beth aveni.
24 Amo esohaga, Isala: ili dunu da ha: ga gasa hamedei galu. Bai Solo ea ili ha: i mae moma: ne, sema bagade ilegei. E amane sia: i, “Na ha lai ilima dabe i dagoiba: le fawane, bu ha: i moma.” Amaiba: le, amo esoha, Isala: ili dunu da ha: i hamedafa mai.
Siku hiyo watu wa Israeli walifadhaika kwa sababu Sauli aliwaweka watu chini ya kiapo akasema, “Na alaaniwe mtu atakaye kula chakula kabla ya jioni na kabla sijalipiza kisasi kwa maadui zangu.” Hivyo hakuna hata mmoja kati ya watu wote aliyeonja chakula.
25 Ilia da iwilaga mana ba: loba, agime hano bagade ba: i.
Ndipo watu wote wakaingia msituni na kuona asali ikiwa juu ya ardhi.
26 Iwila da agime hano bagadedafa dialebe, be ilia da Solo ea ilima gasa bagade gagabusu aligima: ne sema ilegei amoma beda: iba: le, hamedafa mai.
Watu walipoingia humo msituni, asali ilitiririka, lakini hakuna aliyeweka mkono wake kinywani kwa maana watu waliogopa kiapo.
27 Be Yonada: ne da eda ea sema ilegei amo hame nabi galu. Amaiba: le, e da ea galiamoga sone lale, agime diasu gelaba sone, agime hano mai.
Lakini Yonathani alikuwa hajasikia kwamba baba yake amewaagiza watu kwa kiapo. Akanyoosha ncha ya fimbo iliyokuwa mkononi mwake na kuichovya kwenye sega la asali. Kisha akanyoosha mkono wake hadi kinywani mwake, na macho yake yakaangaziwa.
28 Be dunu afae da Yonada: nema amane sia: i, “Ninia huluane da ha: ga gasa hamedei gala. Bai diada da nini beda: ma: ne gasa bagade sema ilegei. E da amane sia: i, “Nowa da wali eso ha: i nasea, amo dunuma da gagabusu aligima: ne dialumu.”
Ndipo mmoja wa watu hao, akamwambia, “Baba yako aliwaagiza watu kwa mkazo na kwa kiapo, kwa kusema, 'Alaaniwe mtu atakaye kula chakula kwa siku ya leo,' ingawa watu wamedhoofika kwa ajili ya njaa.”
29 Yonada: ne da bu adole i, “Na ada da ninia fi dunu wadela: ma: ne giadofale bagade hamoi. Ba: ma! Na da agime hano maiba: le, hahawane wea!
Baadaye Yonathani alisema, “Baba yangu amefanya matatizo katika nchi. Angalia jinsi macho yangu alivyotiwa nuru kwa sababu nilionja asali hii kidogo.
30 Ninia fi dunu da ha: i manu ilia ha lai ilima lai, amo hahawane manu da defea galu. Amaiyaba, Filisidini dunu eno bagohame medole legela: loba!”
Je, siyo vivuri sana kama leo watu wangekula bila kizuizi nyara walizopata kutoka kwa maadui zao? Kwa sababu sasa mauaji hayakuwa makubwa katikati ya Wafilisti.”
31 Amo esoha, Isala: ili dunu da Filisidini dunu hasali. Gegesu da Migema: se amogai muni, gegegena asili, A:idialone moilaiga doaga: i. Amogala, Isala: ili dunu da ha: ga bagadewane goaiya: igia: i.
Siku hiyo waliwashambulia Wafilisti kutoka Mikmashi hadi Aiyaloni. Na watu walikuwa wamechoka sana.
32 Amaiba: le, ilia da hehenaiya afia: le, ha lai dunuma sasamogei liligi lale, sibi amola bulamagau medole, maga: mena gahea mai.
Hivyo watu wakazivamia nyara na kuchukua kondoo, ng'ombe na ndama na kuwachinja hapo chini. Watu walikula nyama zao pamoja na damu.
33 Dunu eno da Soloma amane adoi, “Ba: ma! Dunu ilia da Hina Godema wadela: le bagade hamosa. Bai ilia da ohe hu gahea nabeba: le.” Solo da bagade halale sia: i, “Dilia da hohonosu dunu! Gele bagade nama fefedogole guda: ma!”
KIsha wakamwambia Sauli, “Tazama, watu wanamtenda BWANA dhambi kwa kula pamoja na damu.” Sauli akasema, “Mmetenda isivyo haki. Sasa, viringisheni jiwe kubwa kwangu.” Sauli akasema,
34 Amalalu, e da eno gasa bagade hamoma: ne sia: i, “Dunu gilisia amoga asili, ilia sibi amola bulamagau huluane guiguda: oule misa: ne sia: ma. Ilia da guiguda: medole moma: ne sia: ma! Ilia da Hina Godema bu wadela: le hamosa: besa: le, ohe hu gahea maedafa moma: ne sia: ma!” Amaiba: le, amogala gasia ilia huluane ilila: ohe amogai oule misini, medole lelegei.
“Nendeni kati watu, na muwaambie, 'Kila mtu alete ng'ombe na kondoo wake, wawachinje hapa, na kuwala. Msimtende BWANA dhambi kwa kula na damu.”' Kwa hiyo watu wote wakaleta kila mtu na ng'ombe wake usiku huo na kuwachinja mahali hapo.
35 Solo da Hina Godema gobele salasu oloda hamoi. E da musa: afae hame gagusu, amo degabo gagui.
Sauli akamjengea BWANA madhabahu, ambayo ilikuwa ya kwanza kwake kumjengea BWANA.
36 Solo da ea dunu fi amane adoi, “Ninia gasia gudu sa: ili Filisidini dunu doagala: le, ili huluane medole legele amola ilia liligi sasamogele lale, amananeawane hehebolo misa: mu.” Ilia da bu adole i, “Dia adi noga: i dawa: sea, amane hamoma.” Be gobele salasu dunu e da amane sia: i, “Ninia hidadea Godema adole ba: mu!”
Ndipo Sauli akasema, “Haya tuwafukuze Wafilisti usiku na kuwateka nyara hadi asubuhi; tusimwache hata mtu mmoja akiwa hai.” Nao wakamjibu, “Fanya unaloona linakupendeza.” Lakini kuhani akasema, “Hebu na tumkaribie Mungu mahali hapa.”
37 Amaiba: le, Solo da Godema adole ba: i, “Na da Filisidini dunu amo doagala: la: dula: ? Di da ninia ilima hasalima: ne fidima: bela: ?” Be amogala Gode da dabe hame adole i.
Sauli alitaka kumuuliza Mungu maswali zaidi, “Je, inanipasa kuwafukuza Wafilisti? Je, utawaweka katika mkono wa Israeli?” Lakini siku hiyo BWANA hakumjibu kitu.
38 Amalalu, Solo da Isala: ili dunu ilia ouligisu dunuma amane sia: i, “Guiguda: misini, wali adi wadela: i hou hamobela: le, adole boba: ma!
Ndipo Sauli akasema, “Njoni hapa, viongozi wote wa watu; mjue na kuona jinsi dhambi hii ilivyotokea leo.
39 Na da Hina Gode amo da Isala: ili fi hasalasu hou iaha, amo Ea Dioba: le, amane sia: sa. Nowa da amo wadela: i hou hamoi galea, ninia da medole legemu. Na mano Yonada: ne ea galea da e amolawane medole legemu.” Be dunu huluane da ouiya: i.
Kwa maana, kama BWANA aishivyo, aliyewaokoa Israeli, hata kama angekuwa mwanangu Yonathani, atapaswa kufa.” Lakini hakuna hata mtu mmoja miongoni mwa watu aliye mjibu neno.
40 Amalalu, Solo da ilima amane sia: i, “Dilia huluane ga (south) la: diga aligima. Na amola Yonada: ne ania da gui aligimu.” Ilia bu adole ba: i, “Dia adi noga: i dawa: sea, amane hamoma.”
Basi akawaambia Waisraeli wote, “Simameni upande mmoja, na mimi na Yonathani tutasimama upande mwingine.” Kisha watu wakamwambia Sauli, “Fanya lile unaloona jema kwako.”
41 Solo da Isala: ili Hina Godema amane sia: i, “Hina Gode! Di da abuliba: le na dima adole ba: i amoma dabe hame adole i? Isala: ili Hina Gode! Ninia sema igi aduna ba: sea, Dia amo bai ninima adole ima. Na o Yonada: ne da wadela: le hamoi galea, Iulimi igi amoga olelema. Be Isala: ili fi dunu eno da wadela: le hamoi galea, Damimi igi amoga olelema.” Amo adoba: su hamobeba: le, ilia Isala: ili dunu enoga hame, be Solo amola Yonada: ne ela fawane wadela: le hamoi ba: i.
Kwa hiyo, Sauli akamwambia BWANA, Mungu wa Israeli, “Tuoneshe Thumimu.” Yonathani na Sauli wakatwaliwa, lakini watu walinusurika kuchaguliwa.
42 Amalalu, Solo da amane sia: i, “Defea! Na o Yonada: ne ania galebeyale adoba: ma.” Amane hamone ba: loba, Yonada: ne hi da wadela: le hamoi ba: i.
Basi Sauli akasema, “Tupa mawe ya bahati nasibu tuone kati yangu na mwanangu Yonathani.” Ndipo Yonathani akatwaliwa.
43 Amalalu, Solo da Yonada: nema adole ba: i, “Nagofe! Dia abuli hamoi!” Yonada: ne bu adole i, “Na da agime hano fonobahadi fawane mai. Na da wea! Na da bogomusa: momagele lela!”
Kisha Sauli akamwambia Yonathani, “Niambie umefanya nini.” Yonathani akamwambia baba yake, “Nilionja asali kidogo kwa kutumia ncha ya fimbo iliyokuwa mkononi mwangu. Niko hapa; Nitakufa.”
44 Solo da ema amane sia: i, “Ninia da di medole legemu! Be ninia da di hame medole legesea, Gode da na fane legemu da defea!”
Sauli akasema, “Mungu afanye hivyo na kuzidi hata kwangu, kama Yonathani hautakufa.”
45 Be Isala: ili dunu ilia da Soloma amane sia: i, “Yonada: ne da Isala: ili dunu ilia Filisidini dunuma hasalima: ne, logo noga: le doasi. Amaiba: le, e medole legemu da defea hame. Ninia da Esalalalusu Gode Ea Dioba: le gasa bagade ilegele sia: sa. E da dialuma hinabo afae hamedafa fisimu. Ea wali eso hamobe, e da Gode Ea fidibiba: le fawane hamoi.” Amaiba: le, Isala: ili dunu da e gaga: iba: le, Yonada: ne da hame medole legei ba: i.
Basi watu wakamuuliza Sauli, “Je, inampasa Sauli afe, ni nani aliyetekeleza ushindi huu mkubwa kwa ajili ya Israeli? Mbali na hayo! Kama BWANA aishivyo, hata unywele mmoja wa kichwa chake hautaanguka chini, kwa maana leo amefanya kazi pamoja na Mungu.” Hivyo hao watu walimuokoa Yonathani ili asife.
46 Amalu fa: no, Solo da Filisidini dunuma sefasilalu yolesili, ilia da ilia sogedafa amoga buhagi.
Basi Sauli akasita kuwafuatia Wafilisti, nao wakarudi katika makao yao.
47 Solo da Isala: ili fi ilia hina bagade ilegei amo fa: no e da ea ha lai huluane ilima gegenanu. Ea ha lai da Moua: be fi, A:mone fi, Idome fi, Souba hina bagade amola Filisidini hina bagade.
Sauli alipoanza kutawala juu ya Israeli, alipigana na adui zake wote kila upande. Alipigana dhidi ya Moabu, dhidi ya watu wa Amoni, Edomu, wafalme wa Zoba, na Wafilisti. Popote alipogeukia aliwapiga kwa adhabu adui zake.
48 E da mae beda: ne, nimi bagadewane gegei. A: malege dunu da gasa bagade, be Solo da amo fi amola hasali. Dunu bagohame da Isala: ili dunuma doagala: musa: misi, be Solo da ea fi dunu gaga: i.
Alitenda kwa ushujaa mkubwa na kuwashinda Waamaleki. Aliwaokoa Israeli kutoka mikono ya watu ambao waliwateka nyara.
49 Solo egefelalia dio da Yonada: ne, Isifi amola Ma: lagisua. Ea uda mano magobo lalelegei da Milabe, amola fa: no lalelegei mano da Miga: le.
Basi wana wa Sauli walikuwa ni hawa Yonathani, Ishvi, na Malkishua. Na majina ya binti zake wawili yalikuwa ni haya, Merabu mzaliwa wa kwanza, na mdogo aliitwa Mikali.
50 Ea uda dio da Ahinoua: me (Ahima: ia: se ea idiwi). Ea dadi gagui dunu ouligisu dunu da ea gawia A: bena (Solo ea ayama Ne amo egefe) galu.
Jina la mke wa Sauli aliitwa Ahinoamu; naye alikuwa binti Ahimaasi. Na jina la Jemedari wa jeshi lake aliitwa Abneri mwana wa Neri, baba mdogo wa Sauli.
51 Solo ea ada Gisa amola A: bena ea ada Ne, ela da A: ibele egefela.
Kishi alikuwa baba yake Sauli; na Neri alikuwa baba yake na Abneri, wote walikuwa wana wa Abieli.
52 Eso huluane e da esalea, Solo da Filisidini dunuma gegesu bagadewane ba: i. E da habogala gasa bagade amola hame beda: su dunu ba: loba, e da amo dunu ea dadi gagui hamoma: ne ilegesu.
Kulikuwa na mapigano makali dhidi ya Wafilisti katika siku zote za Sauli. Naye alipomwona mtu yeyote mwenye nguvu, au mtu yeyote jasiri, alimuunganisha kwake.

< 1 Sa:miuele 14 >