< Yuhanna 11 >

1 ni kange wi dendo Liazaru ma' twirak cin ni baitanya, la ki no bwar lor bi Maryamu kange yi tubcebo Mata.
Mtu mmoja aitwaye Lazaro, mwenyeji wa Bethania, alikuwa mgonjwa. (Kijiji cha Bethania kilikuwa mahali walipokaa Maria na Martha, dada yake.
2 Maryamu woro beltang teluwe nin nuwang yila nir cinen na ko ki yiri duwece. wuro yice Liyazaro dam ki twiranke.
Maria ndiye yule aliyempaka Bwana marashi na kumpangusa kwa nywele zake. Lazaro, kaka yake, ndiye aliyekuwa mgonjwa.)
3 yitub Marta tom tomange kirittin coki, tee, to co ni wo mwo cwitiyeu nuwabo luma.
Basi, hao dada wakatuma ujumbe huu kwa Yesu: “Bwana, rafiki yako ni mgonjwa!”
4 kambo kiritti nuwa, la ci tokki mani yatico bwar, la tuka liyar kwama nyo, dige bwiyeu na bi bwe kwama fiya layar cer cinen.”
Yesu aliposikia hivyo akasema, “Ugonjwa huo hautaleta kifo, ila ni kwa ajili ya kumtukuza Mungu; ameugua ili kwa njia hiyo Mwana wa Mungu atukuzwe.”
5 Yeecu cwi Martati, kange yice kange, Liazaru nuwa luma co ci tiyang yi.
Yesu aliwapenda Martha, dada yake na Lazaro.
6 na curori cin nyi bi beiyo lo ce, ban ya yafu diya tak
Alipopata habari kwamba Lazaro ni mgonjwa, Yesu aliendelea kukaa mahali hapo alipokuwa kwa siku mbili zaidi.
7 la bi beiyo loce cin nyi co, teluwe yafu diya tak
Kisha akawaambia wanafunzi wake, “Twendeni tena Yudea!”
8 la bi bei yo lo co cin nyi co, teluwe yafuda donen ti wi duwal naci ya naci mubangnen ki ter yilo mu cwi yila kati witak?”
Wanafunzi wakamwambia, “Mwalimu! Muda mfupi tu umepita tangu Wayahudi walipotaka kukuua kwa mawe, nawe unataka kwenda huko tena?”
9 kiritti ciya kebo kene kwab culombo yob na ka kaku ko win ne ce ka?
Yesu akajibu, “Je, saa za mchana si kumi na mbili? Basi, mtu akitembea mchana hawezi kujikwaa kwa kuwa anauona mwanga wa ulimwengu huu.
10 ta no ni yayam ki kumeri an kottange dige bwiyeu filang ko mani kange co?
Lakini mtu akitembea usiku atajikwaa kwa maana mwanga haumo ndani yake.”
11 co tok ki na wuro di ki bwi nyori con nyi ci, forkume layijaro daken dum. laman ya na kungum co mwor dume.”
Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, akawaambia, “Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini mimi nitakwenda kumwamsha.”
12 co bibeiyo loco nyi ki no dum ci datiyeri cin yuram
Wanafunzi wake wakamwambia, “Bwana, ikiwa amelala, basi atapona.”
13 la kiritti ciyeu ci tok ker bwar Liyazaru dila ci kwetiri ki ker dume wo fubkakko ce.
Wao walidhani kwamba alikuwa amesema juu ya kulala usingizi, kumbe alikuwa amesema juu ya kifo cha Lazaro.
14 la kiritti fwetang ci nen, “Layazaru bwiyam.
Basi, Yesu akawaambia waziwazi, “Lazaro amekufa;
15 mi bilangti ki den kumer. na ki mi mani wiri na kom ne bilingke di la biya cinen.”
Lakini nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini. Haya, twendeni kwake.”
16 to wuro ci ciwoti ki bi bwe wo ci bo yob di wine nyi tangnim bi beiyo biya nabi bwiya wari kange kiritti.”
Thoma (aitwaye Pacha) akawaambia wanafunzi wenzake, “Twendeni nasi tukafe pamoja naye!”
17 kambo kiritti laweu la con kwabti dam kume nar tuwe
Yesu alipofika huko alikuta Lazaro amekwisha kaa kaburini kwa siku nne.
18 baitanya yilo ki no bi dom kange uracalima, be yame nyo bidom ti beryer.
Kijiji cha Bethania kilikuwa karibu na Yerusalemu umbali upatao kilomita tatu.
19 Yafudawa ducce cin bou na ci fiya co na ci ma cinen dangneri bibwei yiciye.
Wayahudi wengi walikuwa wamefika kwa Martha na Maria kuwafariji kwa kifo cha kaka yao.
20 kambo nuwa ki kiritti bou ti yori yaken na ci fiya co nan di Maryamu yim mwor luwe.
Basi, Martha aliposikia kwamba Yesu alikuwa anakuja, akaenda kumlaki; lakini Maria alibaki nyumbani.
21 matta nyi kiritti. teluwe naki mun wi fori no yimi ti bwiyabo.
Martha akamwambia Yesu, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!
22 bwentano can na wori min nyimom gwam dige mu kinongi kang kwamari atin ne nen.”
Lakini najua kwamba hata sasa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa.”
23 kiritti nyi co, “yimwe atin kwenum kwarce.”
Yesu akamwambia, “Kaka yako atafufuka.”
24 la matta nyi co ki min nyimom bidiye kwenka nob bware an kwenum.”
Martha akamjibu, “Najua kwamba atafufuka wakati wa ufufuo, siku ya mwisho.”
25 kiritti nyi co Matta mo mi kunga nob bware, mo mi dume ni wo ne bilengke, mi neneu bwantano bwiyamri, can kwenum;
Yesu akamwambia, “Mimi ndimi ufufuo na uzima. Anayeniamini mimi hata kama anakufa, ataishi:
26 gwam ni wo ki dume no ci neya bilengkere mani ca bwiyati dong. mon ciya kange wura?” (aiōn g165)
na kila anayeishi na kuniamini, hatakufa kamwe. Je, waamini hayo?” (aiōn g165)
27 la can nyi co ong min ciya mwo Almaciya, bi bwe kwama wuro bouti fo kalewo.”
Martha akamwambia, “Ndiyo Bwana! Naamini kwamba wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yule ajaye ulimwenguni.”
28 ki kwama co tok ki nyo, la con yilaken con cuwo yice Maryamu dinge win co ki, teluwe biyegen, yilo cu wo nenti.”
Baada ya kusema hayo, Martha alikwenda kumwita Maria, dada yake, akamwabia faraghani, “Mwalimu yuko hapa, anakuita.”
29 kambo co nuwa nyeri la con kweni con yaken cinen wulom.
Naye aliposikia hivyo, akainuka mara, akamwendea Yesu.
30 kiritti kweri doubo bwaror nwi fiye Matta yafiyaco wiyeu.
Yesu alikuwa hajaingia kijijini, ila alikuwa bado mahali palepale Martha alipomlaki.
31 kange yafudawa wuro ci wari kange Maryamu we in co nubo buro ne ka cekko dangneri to cin ciri mwor luwe. wulom, la cin bwangten co, ci kwatiri cin cu cin ci wiye tuwe.
Basi, Wayahudi waliokuwa nyumbani pamoja na Maria wakimfariji walipomwona ameinuka na kutoka nje ghafla, walimfuata. Walidhani alikuwa anakwenda kaburini kuomboleza.
32 kambo Maryamu lam fiye tuwe wiyeri, la cin yarken kabum nace konin co ki teluwe, naki wo wari kange nyori yiye ti bwiyabo.”
Basi, Maria alipofika mahali pale Yesu alipokuwa na kumwona, alipiga magoti, akamwabia, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!”
33 kambo kiritti to co ci wiye tiyeri kange Yafudawa wuri ci bwangten ceu, co ci nyimangi yuwa tangbe kange co wi kange co.
Yesu alipomwona analia, na wale Wayahudi waliokuja pamoja naye wanalia pia, alijawa na huzuni na kufadhaika moyoni.
34 la co to ki fiye wuni ki daken ci ke?” la cin nyi co ki teluwe bouti.”
Kisha akawauliza, “Mlimweka wapi?” Wakamwambia, “Bwana, njoo uone.”
35 kiritti ci wiye.
Yesu akalia machozi.
36 la Yafudawa ciki to kambo co cwi Liyazaru tiye; “
Basi, Wayahudi wakasema, “Tazameni jinsi alivyompenda!”
37 dila nubo buro ciki, nii wuro ne fukma toka fiyeu noti kobo bwiyak ni wuroka?”
Lakini baadhi yao wakasema, “Je, huyu aliyemfumbua macho yule kipofu, hakuweza kumfanya Lazaro asife?”
38 kiritti dim ki yuwa tangbe ki bwici la cin cuken tuwe nin tuwe cim mummuwe nyi tuweu cin comti terowi.
Basi, Yesu akiwa amehuzunika tena moyoni, akafika kaburini. Kaburi lenyewe lilikuwa pango, na lilikuwa limefunikwa kwa jiwe.
39 la kiritti ki okm tungum tero Matta yi liyazaru wo bwiyame nyi teluwe, can neu bwiyo fuyem ki kume ta'ar can ki bwi yaka cekko.”
Yesu akasema, “Ondoeni hilo jiwe!” Martha, dada yake huyo aliyekufa, akamwambia, “Bwana, amekwishaanza kunuka; amekaa kaburini siku nne!”
40 kiritti tok ki mi nyi nen bono mu ne bilengkari mwan fiya liyar kwama ka?”
Yesu akamwambia, “Je, sikukwambia kwamba ukiamini utaona utukufu wa Mungu?”
41 di la cin kungum tero. kiritti kung nuwe ce dii tokki tee mi, min bumwen kang dige bwiyeu mu nuwa yeti,
Basi, wakaliondoa lile jiwe. Yesu akatazama juu mbinguni, akasema, “Nakushukuru Baba kwa kuwa wewe wanisikiliza.
42 min nyimom bwen tano ki kwama wuniri mu wari kange timfo ker kangum yere mi tok tiye, mi naci bilengke mwo mo tomuyere.”
Najua kwamba unanisikiliza daima. Lakini nimesema hayo kwa ajili ya watu hawa waliopo hapa ili wapate kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma.”
43 kambo co tok kero wuro nyeri la con kung diro coki, “Layazaru di cerou.
Alipokwisha sema hayo, akaita kwa sauti kubwa: “Lazaro! Toka nje!”
44 la ni wo bwiyammeu cereu naceko kange kangko bwabe ki yi lang. tigom ce bo yi co canji langum ki yakka yi lange. kiritti ki nyi ci ki kom kwim co na cu.”
Huyo aliyekuwa amekufa akatoka nje, huku amefungwa sanda miguu na mikono, na uso wake umefunikwa. Yesu akawaambia, “Mfungueni, mkamwache aende zake.”
45 la nubo ducce mwor Yafudawa nin wo bo maryamu ni nen ci to dige bi bwe kwama mane cin ciya kange co.
Basi, Wayahudi wengi waliokuwa wamefika kwa Maria walipoona kitendo hicho alichokifanya Yesu wakamwamini.
46 la kangem bo yi la ken Faricawa nin cin nyi ci dige kiritti mane,
Lakini baadhi yao walikwenda kwa Mafarisayo wakatoa taarifa ya jambo hilo alilofanya Yesu.
47 la nob werfun durko kange Faricayawa cin mwen dor ciyero, fiye win ci tok ki nye ba matiye, ni wuro madigerti ducce.
kwa hiyo makuhani wakuu na Mafarisayo wakafanya kikao cha Baraza kuu, wakasema, “Tufanye nini? Mtu huyu anafanya ishara nyingi mno.
48 no bo dobco koni nawori, nubo ducce atin bwangten co. Ramawa an bou yom fiye beu kange bitine beu.
Tukimwacha tu watu wote watamwamini, nao Waroma watakuja kuliharibu Hekalu letu na taifa letu!”
49 gwam nyo tak ni kange wi tiber ciyer, kayafa co ci ni bifumero durko ki coro wuro, nyi ki nyom bo diger.”
Hapo, mmoja wao aitwaye Kayafa, ambaye alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo, akawaambia, “Ninyi hamjui kitu!
50 ki nyombo daten ni win na bwiyam ki den nubo ducce na bwiya kange wo kale kwarum a kwenum tiye.”
Je, hamwoni kwamba ni afadhali kwenu mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, kuliko taifa zima liangamizwe?”
51 tok digewuro kebo na dor cero la kambo cin dur ni bi wabir, tok kero dur coki deten, kiritti na bwiyam ki den nubem.
Yeye hakusema hivyo kwa hiari yake mwenyewe, bali kwa vile alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo, alibashiri kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa lao;
52 la kebo ki den nubo kwarub la ki den na murangu bi bei kwama wuro merangum fiye kutanrange nyo weu na mweru ci fiye win.
na wala si kwa ajili yao tu, bali pia apate kuwaleta pamoja watoto wa Mungu waliotawanyika.
53 di la ki kume di coru ci ter doka nure wuro ciya twal kiritti tiye.
Basi, tangu siku hiyo viongozi wa Wayahudi walifanya mipango ya kumwua Yesu.
54 di la na co kiritti mani nyo yanglang tiber Yafudawa dila ci yaken kange fiye bidom kange kii na kange cinar lor kange ci cuwoti Ifraimu. la ci beiyo loce.
Kwa hiyo, Yesu hakutembea tena hadharani kati ya Wayahudi, bali alitoka hapo, akaenda mahali karibu na jangwa, katika mji uitwao Efraimu. Akakaa huko pamoja na wanafunzi wake.
55 tano yab karko na Yafudawa lau bidomdi la nubo ducce firin Uracalima nyo bitine dinge wine bidi idi na yulang bwi ci.
Sikukuu ya Wayahudi ya Pasaka ilikuwa karibu, na watu wengi walikwenda Yerusalemu ili wajitakase kabla ya sikukuu hiyo.
56 cin ter doka kiritti ci tikkang ker ti ki kwama ci tirangum tirange ku kwama, tokti. nye kom kwaatiye? mani a bo iditi ka?
Basi, wakawa wanamtafuta Yesu; nao walipokusanyika pamoja Hekaluni wakaulizana, “Mwaonaje? Yaonekana kwamba haji kabisa kwenye sikukuu, au sivyo?”
57 ni dur wabiro kange Faricawa kweri cin neken nyel no ni wo to kiritti ri nyi ci na ci tam co.
Makuhani wakuu na Mafarisayo walikuwa wametoa amri kwamba mtu akijua mahali aliko Yesu awaarifu kusudi wamtie nguvuni.

< Yuhanna 11 >