< ܡܬܝ 4 >
ܗܝܕܝܢ ܝܫܘܥ ܐܬܕܒܪ ܡܢ ܪܘܚܐ ܕܩܘܕܫܐ ܠܡܕܒܪܐ ܕܢܬܢܤܐ ܡܢ ܐܟܠܩܪܨܐ | 1 |
Kisha Yesu akaongozwa na Roho Mtakatifu kwenda nyikani ili akajaribiwe na ibilisi.
ܘܨܡ ܐܪܒܥܝܢ ܝܘܡܝܢ ܘܐܪܒܥܝܢ ܠܝܠܘܢ ܐܚܪܝܬ ܕܝܢ ܟܦܢ | 2 |
Baada ya kufunga siku arobaini usiku na mchana, hatimaye akaona njaa.
ܘܩܪܒ ܗܘ ܕܡܢܤܐ ܘܐܡܪ ܠܗ ܐܢ ܒܪܗ ܐܢܬ ܕܐܠܗܐ ܐܡܪ ܕܗܠܝܢ ܟܐܦܐ ܢܗܘܝܢ ܠܚܡܐ | 3 |
Mjaribu akamjia na kumwambia, “Ikiwa wewe ndiye Mwana wa Mungu, amuru mawe haya yawe mikate.”
ܗܘ ܕܝܢ ܥܢܐ ܘܐܡܪ ܟܬܝܒ ܕܠܐ ܗܘܐ ܒܠܚܡܐ ܒܠܚܘܕ ܚܝܐ ܒܪܢܫܐ ܐܠܐ ܒܟܠ ܡܠܐ ܕܢܦܩܐ ܡܢ ܦܘܡܗ ܕܐܠܗܐ | 4 |
Lakini Yesu akajibu, “Imeandikwa: ‘Mtu haishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.’”
ܗܝܕܝܢ ܕܒܪܗ ܐܟܠܩܪܨܐ ܠܡܕܝܢܬ ܩܘܕܫܐ ܘܐܩܝܡܗ ܥܠ ܟܢܦܐ ܕܗܝܟܠܐ | 5 |
Ndipo ibilisi akamchukua Yesu mpaka mji mtakatifu na kumweka juu ya mnara mrefu wa Hekalu,
ܘܐܡܪ ܠܗ ܐܢ ܒܪܗ ܐܢܬ ܕܐܠܗܐ ܫܕܝ ܢܦܫܟ ܠܬܚܬ ܟܬܝܒ ܓܝܪ ܕܠܡܠܐܟܘܗܝ ܢܦܩܕ ܥܠܝܟ ܘܥܠ ܐܝܕܝܗܘܢ ܢܫܩܠܘܢܟ ܕܠܐ ܬܬܩܠ ܒܟܐܦܐ ܪܓܠܟ | 6 |
akamwambia, “Kama wewe ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini. Kwa kuwa imeandikwa: “‘Atakuagizia malaika zake, nao watakuchukua mikononi mwao ili usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.’”
ܐܡܪ ܠܗ ܝܫܘܥ ܬܘܒ ܟܬܝܒ ܕܠܐ ܬܢܤܐ ܠܡܪܝܐ ܐܠܗܟ | 7 |
Yesu akamjibu, “Pia imeandikwa: ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’”
ܬܘܒ ܕܒܪܗ ܐܟܠܩܪܨܐ ܠܛܘܪܐ ܕܛܒ ܪܡ ܘܚܘܝܗ ܟܠܗܝܢ ܡܠܟܘܬܐ ܕܥܠܡܐ ܘܫܘܒܚܗܝܢ | 8 |
Kwa mara nyingine, ibilisi akamchukua Yesu mpaka kwenye kilele cha mlima mrefu na kumwonyesha falme zote za dunia na fahari zake,
ܘܐܡܪ ܠܗ ܗܠܝܢ ܟܠܗܝܢ ܠܟ ܐܬܠ ܐܢ ܬܦܠ ܬܤܓܘܕ ܠܝ | 9 |
kisha akamwambia, “Nitakupa hivi vyote kama ukinisujudia na kuniabudu.”
ܗܝܕܝܢ ܐܡܪ ܠܗ ܝܫܘܥ ܙܠ ܠܟ ܤܛܢܐ ܟܬܝܒ ܓܝܪ ܕܠܡܪܝܐ ܐܠܗܟ ܬܤܓܘܕ ܘܠܗ ܒܠܚܘܕܘܗܝ ܬܦܠܘܚ | 10 |
Yesu akamwambia, “Ondoka mbele yangu, Shetani! Kwa maana imeandikwa, ‘Mwabudu Bwana Mungu wako, na umtumikie yeye peke yake.’”
ܗܝܕܝܢ ܫܒܩܗ ܐܟܠܩܪܨܐ ܘܗܐ ܡܠܐܟܐ ܩܪܒܘ ܘܡܫܡܫܝܢ ܗܘܘ ܠܗ | 11 |
Ndipo ibilisi akamwacha, nao malaika wakaja na kumhudumia.
ܟܕ ܫܡܥ ܕܝܢ ܝܫܘܥ ܕܝܘܚܢܢ ܐܫܬܠܡ ܫܢܝ ܠܗ ܠܓܠܝܠܐ | 12 |
Yesu aliposikia kwamba Yohana Mbatizaji alikuwa ametiwa gerezani, alirudi Galilaya.
ܘܫܒܩܗ ܠܢܨܪܬ ܘܐܬܐ ܥܡܪ ܒܟܦܪܢܚܘܡ ܥܠ ܝܕ ܝܡܐ ܒܬܚܘܡܐ ܕܙܒܘܠܘܢ ܘܕܢܦܬܠܝ | 13 |
Akaondoka Nazareti akaenda kuishi Kapernaumu, mji ulioko karibu na bahari, katika mipaka ya nchi ya Zabuloni na Naftali,
ܕܢܬܡܠܐ ܡܕܡ ܕܐܬܐܡܪ ܒܝܕ ܐܫܥܝܐ ܢܒܝܐ ܕܐܡܪ | 14 |
ili kutimiza unabii wa nabii Isaya, kama alivyosema:
ܐܪܥܐ ܕܙܒܘܠܘܢ ܐܪܥܐ ܕܢܦܬܠܝ ܐܘܪܚܐ ܕܝܡܐ ܥܒܪܘܗܝ ܕܝܘܪܕܢܢ ܓܠܝܠܐ ܕܥܡܡܐ | 15 |
“Nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, kwenye njia ya kuelekea baharini, ngʼambo ya Yordani, Galilaya ya watu wa Mataifa:
ܥܡܐ ܕܝܬܒ ܒܚܫܘܟܐ ܢܘܗܪܐ ܪܒܐ ܚܙܐ ܘܐܝܠܝܢ ܕܝܬܒܝܢ ܒܐܬܪܐ ܘܒܛܠܠܐ ܕܡܘܬܐ ܢܘܗܪܐ ܕܢܚ ܠܗܘܢ | 16 |
watu wale waliokaa gizani wameona nuru kuu; nao wale walioishi katika nchi ya uvuli wa mauti, nuru imewazukia.”
ܡܢ ܗܝܕܝܢ ܫܪܝ ܝܫܘܥ ܠܡܟܪܙܘ ܘܠܡܐܡܪ ܬܘܒܘ ܩܪܒܬ ܠܗ ܓܝܪ ܡܠܟܘܬܐ ܕܫܡܝܐ | 17 |
Tangu wakati huo, Yesu alianza kuhubiri akisema: “Tubuni, kwa maana Ufalme wa Mbinguni umekaribia.”
ܘܟܕ ܡܗܠܟ ܥܠ ܝܕ ܝܡܐ ܕܓܠܝܠܐ ܚܙܐ ܬܪܝܢ ܐܚܝܢ ܫܡܥܘܢ ܕܐܬܩܪܝ ܟܐܦܐ ܘܐܢܕܪܐܘܤ ܐܚܘܗܝ ܕܪܡܝܢ ܡܨܝܕܬܐ ܒܝܡܐ ܐܝܬܝܗܘܢ ܗܘܘ ܓܝܪ ܨܝܕܐ | 18 |
Yesu alipokuwa anatembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona ndugu wawili, Simoni aitwaye Petro, na Andrea ndugu yake. Walikuwa wakizitupa nyavu zao baharini kwa kuwa wao walikuwa wavuvi.
ܘܐܡܪ ܠܗܘܢ ܝܫܘܥ ܬܘ ܒܬܪܝ ܘܐܥܒܕܟܘܢ ܕܬܗܘܘܢ ܨܝܕܐ ܕܒܢܝ ܐܢܫܐ | 19 |
Yesu akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.”
ܗܢܘܢ ܕܝܢ ܡܚܕܐ ܫܒܩܘ ܡܨܝܕܬܗܘܢ ܘܐܙܠܘ ܒܬܪܗ | 20 |
Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
ܘܟܕ ܥܒܪ ܡܢ ܬܡܢ ܚܙܐ ܐܚܪܢܐ ܐܚܐ ܬܪܝܢ ܝܥܩܘܒ ܒܪ ܙܒܕܝ ܘܝܘܚܢܢ ܐܚܘܗܝ ܒܐܠܦܐ ܥܡ ܙܒܕܝ ܐܒܘܗܘܢ ܕܡܬܩܢܝܢ ܡܨܝܕܬܗܘܢ ܘܩܪܐ ܐܢܘܢ | 21 |
Alipoendelea mbele kutoka pale, akawaona ndugu wengine wawili, Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana nduguye, wakiwa wamekaa kwenye mashua pamoja na baba yao Zebedayo, wakizitengeneza nyavu zao. Yesu akawaita.
ܗܢܘܢ ܕܝܢ ܡܚܕܐ ܫܒܩܘ ܠܐܠܦܐ ܘܠܐܒܘܗܘܢ ܘܐܙܠܘ ܒܬܪܗ | 22 |
Nao mara wakaiacha mashua yao, pamoja na baba yao, wakamfuata.
ܘܡܬܟܪܟ ܗܘܐ ܝܫܘܥ ܒܟܠܗ ܓܠܝܠܐ ܘܡܠܦ ܗܘܐ ܒܟܢܘܫܬܗܘܢ ܘܡܟܪܙ ܤܒܪܬܐ ܕܡܠܟܘܬܐ ܘܡܐܤܐ ܟܠ ܟܐܒ ܘܟܘܪܗܢ ܒܥܡܐ | 23 |
Yesu akapita katika Galilaya yote, akifundisha katika masinagogi yao, akihubiri habari njema za Ufalme, na akiponya kila ugonjwa na kila aina ya maradhi miongoni mwa watu.
ܘܐܫܬܡܥ ܛܒܗ ܒܟܠܗ ܤܘܪܝܐ ܘܩܪܒܘ ܠܗ ܟܠܗܘܢ ܐܝܠܝܢ ܕܒܝܫ ܒܝܫ ܥܒܝܕܝܢ ܒܟܘܪܗܢܐ ܡܫܚܠܦܐ ܘܐܝܠܝܢ ܕܐܠܝܨܝܢ ܒܬܫܢܝܩܐ ܘܕܝܘܢܐ ܘܕܒܪ ܐܓܪܐ ܘܡܫܪܝܐ ܘܐܤܝ ܐܢܘܢ | 24 |
Kwa hiyo sifa zake zikaenea sehemu zote za Shamu, nao watu wakamletea wote waliokuwa na magonjwa mbalimbali na maumivu, waliopagawa na pepo wachafu, wenye kifafa na waliopooza, naye akawaponya.
ܘܐܙܠܘ ܒܬܪܗ ܟܢܫܐ ܤܓܝܐܐ ܡܢ ܓܠܝܠܐ ܘܡܢ ܥܤܪܬ ܡܕܝܢܬܐ ܘܡܢ ܐܘܪܫܠܡ ܘܡܢ ܝܗܘܕ ܘܡܢ ܥܒܪܐ ܕܝܘܪܕܢܢ | 25 |
Makutano makubwa ya watu yakawa yanamjia kutoka Galilaya, Dekapoli, Yerusalemu, Uyahudi na kutoka ngʼambo ya Mto Yordani.