< Yuhana 8 >

1 Yesu wa ghana likup in Zaitun.
lakini Yesu akaenda kwenye mlima wa Mizeituni.
2 Nin kwui dindin akuru ada nanya kutii nlira, anite vat da kitime; a tunna aso a dursuzo anite.
Kesho yake asubuhi na mapema alikwenda tena Hekaluni. Watu wote wakamwendea, naye akaketi akawa anawafundisha.
3 Anan niyerte nin na Farisawa da nin mong uwani na iwa kifoghe nanya kulapi nfunu nin mong, iceoghe kitikmine.
Basi, walimu wa Sheria na Mafarisayo wakamletea mwanamke mmoja aliyefumaniwa katika uzinzi. Wakamsimamisha katikati yao.
4 Inin woro Yesu ku. “Unan Dursuzu, uwani ulele, ikifogheari nanya kulapin nfunu, ima niyitan nsure.
Kisha wakamwuliza Yesu, “Mwalimu! Mwanamke huyu alifumaniwa katika uzinzi.
5 Nene nanya duke, Musa na woro nari asa ti filiso imus nnit une; fe nworo iyaghari kiteneme?”
Katika Sheria yetu Mose alituamuru mwanamke kama huyu apigwe mawe. Basi, wewe wasemaje?”
6 Iwa belli nani inan kifoghe nin tikanci. Yesu tunna a tumuno a su inyerte kutyen nin licin me.
Walisema hivyo kumjaribu, wapate kisa cha kumshtaki. Lakini Yesu akainama chini, akaandika ardhini kwa kidole.
7 Na iwa li ubu nin tirighe, a fita a yissina a woro nani, “Ame ulenge na addi nin kulapi ba nanya mine, na amere cizin ufilughe nin litale.”
Walipozidi kumwuliza, Yesu akainuka, akawaambia, “Mtu asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza kumpiga jiwe.”
8 Akurru atumuno tutung niyerte nin licin me kutyen.
Kisha akainama tena, akawa anaandika ardhini.
9 Na inung lanza nani, itunna nyizu na lalarum, ucizunu nin kune udak unan ni maline. Ida malizina isuna Yesu ku nin usanme nin wani une na awa di kityek mine.
Waliposikia hivyo, wakaanza kutoweka mmojammoja, wakitanguliwa na wazee. Yesu akabaki peke yake, na yule mwanamke amesimama palepale.
10 Yesu fita aworo nwane, “Uwani, inung anan kifufe nde? Na umong mine nmolofi ba?”
Yesu alipoinuka akamwuliza huyo mwanamke, “Wako wapi wale watu? Je, hakuna hata mmoja aliyekuhukumu?”
11 A wor, “Ko unit urum, Cikilari.” Yesu woro, “Na meng wang nse fi nin kulapi ba, Canfi, ucizunu nene udu nbun, na uwa kuru uti kulapi ba.”
Huyo mwanamke akamjibu, “Mheshimiwa, hakuna hata mmoja!” Naye Yesu akamwambia, “Wala mimi sikuhukumu. Nenda zako; na tangu sasa usitende dhambi tena.”
12 Yesu kuru asu uliru nin nanite aworo, “Menghari nkanang in yi; ulenge na a dofini na ama cinu nanya nsirti ba nani ama se nkanang nlai.”
Yesu alipozungumza nao tena, aliwaambia, “Mimi ndimi mwanga wa ulimwengu. Anayenifuata mimi hatembei kamwe gizani, bali atakuwa na mwanga wa uzima.”
13 A Farisawa woroghe, “Una ushaida litife; na ushaida fe kidegeneri ba.”
Basi, Mafarisayo wakamwambia, “Wewe unajishuhudia mwenyewe; kwa hiyo ushahidi wako si halali.”
14 Yesu kawa aworo nani, Andi ma nna ushaida litining, ushaida ning kidegenari. Meng yiru kikanga na nna nuzu ku, in yiru kikanga na ndin cinu udue, na anung dinin yiru kiti ka na inan nuzuku ba, sa kika na ndin cinu udue.
Yesu akawajibu, “Hata kama ninajishuhudia mwenyewe, ushahidi wangu ni wa kweli kwa sababu mimi najua nilikotoka na ninakokwenda. Lakini ninyi hamjui nilikotoka wala ninakokwenda.
15 Anung din su ushara un yenju nyizi, meng din su umong ushara ba.
Ninyi mnahukumu kwa fikira za kibinadamu, lakini mimi simhukumu mtu.
16 Vat nani asa nsu ushara, ushara nighe kidegenari bara na ndi usanning ba ndi nin Cif ulenge na ana tuyi.
Hata nikihukumu, hukumu yangu ni ya haki kwa sababu mimi siko peke yangu; Baba aliyenituma yuko pamoja nami.
17 Nanere nanya nduka mine ina yertin au ushaida nanit anwaba kidegenere.
Imeandikwa katika Sheria yenu ya kwamba ushahidi wa watu wawili ni halali.
18 Menghari ame ulenge na ndin shaida litining, a ame Ucife na ana tuyi din nin ushaida litining.”
Mimi najishuhudia mwenyewe, naye Baba aliyenituma, ananishuhudia pia.”
19 I woroghe, “Uciffe din weri?” Yesu kawa nani, “Na iyiru menku sa Ucif nin ba; idafo ina yiri, iwa yiru Ucif nighe wang.”
Hapo wakamwuliza, “Baba yako yuko wapi?” Yesu akawajibu “Ninyi hamnijui mimi wala hamumjui Baba. Kama mngenijua mimi, mngemjua na Baba yangu pia.”
20 Awa belin uliru une susut nin kiti in nyeshizu nikurfu ayita ndursuzu nin kiti nanya kutii nlira, ana umong nkifoghe ba, bara na kubi me wa di kusa daba.
Yesu alisema maneno hayo kwenye chumba cha hazina alipokuwa anafundisha Hekaluni. Wala hakuna mtu aliyemtia nguvuni, kwa sababu saa yake ilikuwa haijafika bado.
21 Akuru a woro nani, “Mma su ucin, ima piziri, inin kuzu nanya nalapi mine. Kiti kanga na nma du, na iwa sa idaku ba.”
Yesu akawaambia tena, “Naenda zangu nanyi mtanitafuta, lakini mtakufa katika dhambi zenu. Niendako mimi, ninyi hamwezi kufika.”
22 A Yahudaw woro, “Ama molu litime, ame ulenge na aworo, 'kiti kanga na ndin cinu udue, anung wasa ida ba?”
Basi, viongozi wa Wayahudi wakasema, “Je, atajiua? Mbona anasema: Niendako ninyi hamwezi kufika?”
23 Yesu woro nani, 'Anung anan kadassari; Meng unan kitenari, Anung anan yi ulelere, Na meng unan le uyere ba.
Yesu akawaambia, “Ninyi mmetoka papa hapa chini, mimi nimetoka juu; ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu.
24 Bara nani, nworo minu, ima kuzu nanya nalapi mine. Andi na iyinna mere AME ba, ima kuzu nanya nalapi mine.”
Ndiyo maana niliwaambieni mtakufa katika dhambi zenu. Kama msipoamini kwamba Mimi ndimi, mtakufa katika dhambi zenu.”
25 Iworoghe nenge, “Feghari?” Yesu woro nani, “uliru urika na nna bellin minu nin cizine.
Nao wakamwuliza, “Wewe ni nani?” Yesu akawajibu, “Nimewaambieni tangu mwanzo!
26 Ndi nin nimon gbardang na nma su uliru ku, nkuru nsu ushara ku kitene mine. Vat nani, ulenge na ana tuyi di kidegen; a imon ilenge na nna lanza kitime, imonere ndin bellu uyie.
Ninayo mengi ya kusema na kuhukumu juu yenu. Lakini yule aliyenituma ni kweli; nami nauambia ulimwengu mambo yale tu niliyoyasikia kutoka kwake.”
27 Na iwa yinin nworu adin liru nanghinu liti Ncif ba.
Hawakuelewa kwamba Yesu alikuwa akisema nao juu ya Baba.
28 Yesu woro, “Asa i ghantina Usaun Nnit kitene kani, Ima nin yinnu MERE, ima yinnu tutung na ndi su imoimong in litining ba. Nafo na Ucif na duzsuzoi, ndin belu ilenge imone.
Basi, Yesu akawaambia, “Mtakapokwisha mwinua Mwana wa Mtu hapo ndipo mtakapojua kwamba Mimi ndimi, na kwamba sifanyi chochote mimi mwenyewe, ila nasema tu yale Baba aliyonifundisha.
29 Ulenge na ana tuyi di ligowe nin mi, ana ama suni ussaning ba, bara ndin su imon ilenge na idin puzughe liburi.”
Yule aliyenituma yuko pamoja nami; yeye hakuniacha peke yangu kwani nafanya daima yale yanayompendeza.”
30 Kube na Yesu wa din bellu nleli ulirue, gbardang nanit wa yinnin nighe.
Baada ya kusema hayo watu wengi walimwamini.
31 Yesu wa woro na Yahudawa alenge na iwa yinnin nighe, “Asa ileo ubun nanya nliru nighe, kidegenere anung nono katwa nighari;
Basi, Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, “Kama mkiyazingatia mafundisho yangu mtakuwa kweli wanafunzi wangu.
32 Ima nin yinnu kidegene, kidegenere ma bunku minu utucu.”
Mtaujua ukweli, nao ukweli utawapeni uhuru.”
33 I kawa ghe, Arik kuwunun Ibrahimari na tisa su licin nacara nmong ba; inyizari uma woru, 'Ima se ubuntu iso fong?”
Nao wakamjibu, “Sisi ni wazawa wa Abrahamu, na hatujapata kamwe kuwa watumwa wa mtu yeyote yule. Una maana gani unaposema: mtakuwa huru?”
34 Yesu kawa nani, “Kidegenere ndin bellu minu, vat nlenge na ata kulapi, ame kucin kulapiari.
Yesu akawajibu, “Kweli nawaambieni, kila mtu anayetenda dhambi ni mtumwa wa dhambi.
35 Na kucin din so kilari cikilari me udu ukul ba, usaun ncikilarere din so udu uku me. (aiōn g165)
Mtumwa hana makao ya kudumu nyumbani, lakini mwana anayo makao ya kudumu. (aiōn g165)
36 Andi usaune ma bunku minu, nanere wang ima se ubuntu.
Kama mwana akiwapeni uhuru mtakuwa huru kweli.
37 Nyiru anung kuwunun Ibrahimari; idin pizuru umoli, bara na uliru ninghe se kitin so nanya mine ba.
Najua kwamba ninyi ni wazawa wa Abrahamu. Hata hivyo, mnataka kuniua kwa sababu hamuyakubali mafundisho yangu.
38 Nbele imon ilenge in yene nin Cifning, anung ani din su imon ilenge na ina lanza kitin Cif mine.”
Mimi nasema yale aliyonionyesha Baba, lakini ninyi mwafanya yale aliyowaambieni baba yenu.”
39 I kawa iworo, “Ucif bit Ibrahimari.” Yesu woro nani, Ndafo anung nonon Ibrahimari, iwa su katwan Ibrahime.
Wao wakamjibu, “Baba yetu ni Abrahamu!” Yesu akawaambia, “Kama ninyi mngekuwa watoto wa Abrahamu, mngefanya kama alivyofanya Abrahamu,
40 Vat nani, inani pizira imoli, unit ulenge na a belin minu kidegen kanga na a lanza kiti kutelle. Na Ibrahim nasu ilenge imone ba.
Mimi nimewaambieni ukweli niliousikia kwa Mungu; hata hivyo, ninyi mwataka kuniua. Abrahamu hakufanya hivyo!
41 Idin su nitwa ncif minere.” I woroghe, “Na iwa maru nari nanya nfunu ba; tidi nin Cif urum, Kutelle.”
Ninyi mnafanya mambo yaleyale aliyofanya babu yenu.” Wao wakamwambia, “Sisi si watoto haramu! Tunaye baba mmoja tu, yaani Mungu.”
42 Yesu woro nani, “Andi Kutelle Ucif minere, iwa yitu nin su ninghe, bara meng na nuzu kiti Kutellari nda; na nna dak bara litining ba, amere na tuyi.
Yesu akawaambia, “Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mngenipenda mimi, maana mimi nilitoka kwa Mungu na sasa niko hapa. Sikuja kwa mamlaka yangu mwenyewe, ila yeye alinituma.
43 Iyaghari nta na i yinno uliru nighe ba? Bara na idi nin su ilanza uliru nighere ba.
Kwa nini hamwelewi hayo ninayosema? Ni kwa kuwa hamwezi kuusikiliza ujumbe wangu.
44 Anung nonon cif minere, shaitan, inani din pizuru isu ntok imusun min cif mie. Ame unan molusu nanitari nworu ucizunue ana adi nin yissunu kitene kidegen ba, bara na kidegen di nanya me ba. Asa a belle kinu, asa asu dert nin yitu mere, bara ame unan kinuwari a Ucif kinu.
Ninyi ni watoto wa baba yenu Ibilisi na mnataka tu kutekeleza tamaa za baba yenu. Yeye alikuwa muuaji tangu mwanzo; hana msimamo katika ukweli, kwani ukweli haumo ndani yake. Kila asemapo uongo, husema kutokana na hali yake ya maumbile, maana yeye ni mwongo na baba wa uongo.
45 Vat nani, bara na ndin belu kidegene, na anunghe in yinna ning me ba.
Mimi nasema ukweli, na ndiyo maana ninyi hamniamini.
46 Ghari nanya mine nseyi nin kulapi? Andi ndin bellu kidegen, iyaghari nta na iyinna nin mi ba?
Nani kati yenu awezaye kuthibitisha kuwa mimi nina dhambi? Ikiwa basi nasema ukweli, kwa nini hamniamini?
47 Ame ulenge na adi un Kutelle din lanzu uliru Kutelle; na anung din lanzu unin ba, bara anung anit Kutelleari ba.”
Aliye wa Mungu husikiliza maneno ya Mungu. Lakini ninyi hamsikilizi kwa sababu ninyi si (watu wa) Mungu.”
48 A Yahudawa kawa i woroghe, “Tina belin kidegene au fe kunan Samariyaridi, tutung udi nin na gbergenu?
Wayahudi wakamwambia, “Je, hatukusema kweli kwamba wewe ni Msamaria, na tena una pepo?”
49 Yesu kawa a woro, “Na meng di nin ku gbergenu ba; ama meng din ti Ucif ning gongong, anung ani na ita yi gongon ba.
Yesu akajibu, “Mimi sina pepo; mimi namheshimu Baba yangu, lakini ninyi hamniheshimu.
50 Na meng din pizuru ngongon lit ning ba, unit urumari din pizuru akuru asu ushara.
Mimi sijitafutii utukufu wangu mwenyewe; yuko mmoja mwenye kuutafuta utukufu huo, naye ni hakimu.
51 Kidegenere ndin bellu minu, asa umong lanza uliru nighe, asu katwa mun, na ama yenu ukul ba.” (aiōn g165)
Kweli nawaambieni, anayeuzingatia ujumbe wangu hatakufa milele.” (aiōn g165)
52 A Yahudawa woroghe, “Nene tiyinno udinin kugbergenu. Ibrahim nin na anabawa na kuzu; fe unin woro, 'Asa umon lanza uliru nighe na aba yenu ukul ba.' (aiōn g165)
Basi, Wayahudi wakasema, “Sasa tunajua kweli kwamba wewe ni mwendawazimu! Abrahamu alikufa, na manabii pia walikufa, nawe wasema ati, Anayeuzingatia ujumbe wangu hatakufa milele! (aiōn g165)
53 Na Fe katin Ucif bite Ibrahime, na ana kuba, sa ukatinghe? A a anabawa wang na kuzu, Fe yira litife iyaghari?”
Je, unajifanya mkuu zaidi kuliko baba yetu Abrahamu ambaye alikufa? Hata na manabii walikufa. Wewe unajifanya kuwa nani?”
54 Yesu kawa nani, aworo, “Asa nta liti ninghe ngongong, ngongong nighe di imon ba; Ucif nighari ulenge na ama ti ngongong- ame ulenge na anung woro Kutelle minere.
Yesu akawajibu, “Nikijitukuza mwenyewe, utukufu wangu si kitu. Baba yangu ambaye ninyi mwasema ni Baba yenu, ndiye anayenitukuza.
55 Anung pa na iyirughe ba, ame meng yirughe. Andi nma belle na nyirughe nma so nafo anughe, unan kinu. Vat nani, nyirughe, nmini din dortu uliru me.
Ninyi hamjapata kumjua, lakini mimi namjua. Na, nikisema simjui, nitakuwa mwongo kama ninyi. Mimi namjua na ninashika neno lake.
56 Ucif mine Ibrahim wasu liburi libo ninyenu nwui nighe; awa yene unin, ayi poghe.”
Abrahamu, baba yenu, alishangilia aione siku yangu; naye aliiona, akafurahi.”
57 A Yahudawa woroghe, “Na usa duru akus akut ataun ba, ama fe uni na yene Ibrahim kua?
Basi, Wayahudi wakamwambia, “Wewe hujatimiza miaka hamsini bado, nawe umemwona Abrahamu?”
58 Yesu woro nani, “kidegenere ndin bellu minu, a idutu sa umaru Ibarahim ku, MENG wa yita ku.”
Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, kabla Abrahamu hajazaliwa, mimi niko.”
59 I tunna i pila atala ima filusughe mun, Yesu tunna a nyeshe litime a nuzu nanya kutii nlire a nya.
Hapo wakaokota mawe ili wamtupie, lakini Yesu akajificha, akatoka Hekaluni.

< Yuhana 8 >