< Katwa Nono Katwa 5 >

1 Nanin umong wadiku unan yinusa uyenu lisame wadi Hananiya nin wani me Sarfatu. Amini wa lewu kunen me.
Lakini mtu mmoja jina lake Anania pamoja na mkewe Safira waliuza kiwanja.
2 Amini wa ceu imong ikubu ilena alewe kunen gye. anin daa nmin kagisingyekiti nono kadura. Uwani me wang wayinin asuu nanin,
Huku mkewe akijua kikamilifu, Anania alificha sehemu ya fedha alizopata, akaleta kiasi kilichobaki na kukiweka miguuni pa mitume.
3 Bitrus nin woro gye. “Hananiya bara yangyari shetan pira kibinai fee uminin taa Ufunu Ulau kulapi. bari yangya ri taa uminin su imong ine? Uceu imong ikubu kitife kitene ni lemon na ulewe kunen fie na una nari ikube vat baa.
Petro akamuuliza, “Anania, mbona Shetani ameujaza moyo wako ili kumwambia uongo Roho Mtakatifu, ukaficha sehemu ya fedha ulizopata kutokana na kiwanja?
4 Kubi na iwadi isa lewe kunene ba, kunfere wadi ba? Na una lewe, na ikube wadi nacara fere ba? Ani bara yangyari taa uma su imong inazan ilele? Aina arikari urusuzo nari ba, Kutelle ri udi cinu urusuzu gye.
Je, kabla hujauza hicho kiwanja si kilikuwa mali yako? Hata baada ya kukiuza, fedha ulizopata si zilikuwa kwenye uwezo wako? Kwa nini basi umewaza hila hii moyoni mwako kufanya jambo kama hili? Wewe hukumwambia uongo mwanadamu bali Mungu.”
5 Dana Hananiya lanza timape atin na adeu kutin akuu camcam. Vat alena ilanza ilemong na ise Hananiya ku tin ilanza fiu kang.
Anania aliposikia maneno haya akaanguka chini na kufa. Hofu kuu ikawapata wote waliosikia jambo lililokuwa limetukia.
6 Uzaman tina idaa iyira libe idikasa.
Vijana wakaja, wakaufunga mwili wake sanda, wakamchukua nje kumzika.
7 Kubi nikoro itat ame uwani me pira, na awa yiru ilemong na ise ba.
Saa tatu baadaye mkewe Anania akaingia, naye hana habari ya mambo yaliyotukia.
8 Bitrus nin nuna gye ikubu ilena ulesume damun anin tiringye.”Benli, ligang nikubere ina lewu kunengye? Aminin wa belin nenere ilemong na tina lewu kunengye.
Petro akamuuliza, “Niambie, je, mliuza kiwanja kwa thamani hii?” Akajibu, “Ndiyo, tuliuza kwa thamani hiyo.”
9 Bara nanin Bitrus nin woro gye,”vat mine suu imong inanzan! Anin na bea, yinna irusuzu Ufunu Ulau Cikilari! Lanza! ulanza ucin nazamang alena inuzu kasu cikilari fea? idin das kibulun gye, ima yiru fii udu das tutun.
Ndipo Petro akamwambia, “Imekuwaje mkakubaliana kumjaribu Roho wa Bwana? Tazama! Nyayo za vijana waliomzika mumeo ziko mlangoni, wewe nawe watakuchukua nje.”
10 Nanin molu kubi ba Sarfatu tin na adiu kutin libe na bunu Bitrus. Angyene pira yene gye adio libe tutun iyira libea itin idi kasu kupopo kisek lese.
Saa ile ile akaanguka chini miguuni mwake na kufa. Nao wale vijana wakaingia, wakamkuta amekufa, wakamchukua wakamzika kando ya mumewe.
11 Vat anin yinu sauyenu nanya Urshalima laza fiu kang, bara nilemong na Kutelle su Hananiya nin Sarfatu ku. kogya na lanza ile imongye lazan fiu kang.
Hofu kuu ikalipata kanisa lote pamoja na watu wote waliosikia juu ya matukio haya.
12 Kutelle suu kata ka zikiki nanya na cara nono kadura me ninin anit yino kidere ilemon na iwa din dursuzu anit. Vat ananyinu sa uyenu tinna tina zursuzu kolome liri nanya kuti lira kika na idin yici nin lisa Solomo perch.
Mitume wakafanya ishara nyingi na miujiza miongoni mwa watu. Walioamini wote walikuwa wakikusanyika katika ukumbi wa Solomoni.
13 Vat anite alena iyina nin Yesu ba lanza ifeu anan yinusauyene. Bara nanin anit alele leu ubun lanzu fiu nananyinu sauyenu.
Hakuna mtu mwingine aliyethubutu kuambatana nao ijapokuwa waliheshimiwa sana na watu.
14 Among anit nin awni tin na iyina nin Cikilari Yesu, inin munu atii nin nananyinusauyenu.
Hata hivyo, waliomwamini Bwana wakazidi kuongezeka, wanaume na wanawake.
15 Bara nanin taa, anite tinna dasu nin na tikunu kitene libau danna inin nonkuzo nanin kupia nin nanin andi kuyulin Bitrus na dudo nanin inan shino ti konumine.
Hata wakawa wanawaleta wagonjwa na kuwalaza kwenye magodoro na kwenye vitanda barabarani ili yamkini Petro akipita kivuli chake kiwaguse baadhi yao.
16 Anit gbardan nuzu ni gbirin Urshalima daa kiti nono kata. Inanin wadasu nin nanan tikonu kiti minenin nalena ufunu na gwerganu kifo nanin. Kutelle mini wa shin nanin tikonu mine.
Pia watu wakakusanyika kutoka miji iliyokuwa karibu na Yerusalemu, wakileta wagonjwa na watu walioteswa na pepo wachafu. Hao wote wakaponywa.
17 Aprist adidewe vat nin nale na iwadi ligowe nin na Sandikiwa iwa di ligo mine inin lanza ayi nin nono katawe.
Kisha kuhani mkuu na wenzake wote waliokuwa pamoja naye, waliokuwa wa kundi la Masadukayo, wakajawa na wivu.
18 Bara nanin inin taa anan sun caa kiti lira ikifo nono kataa we inanin watii nanin nanya kuti licin.
Wakawakamata mitume na kuwatia gerezani.
19 Nin kitik anan kadura Kutelle daa atina apuno kiti licin atina anutuno nono Kutelle nutuno nanin das! nin nanin unan kadura Kutelle woro
Lakini wakati wa usiku, malaika wa Bwana akaja, akafungua milango ya gereza na akawatoa nje. Akawaambia,
20 nono kadure, “can udu kiti lira ibeling anite kadura tucu lai usalin ligang.
“Nendeni, mkasimame Hekaluni mkawaambie watu maneno yote ya uzima huu mpya.”
21 Nin lanzu nanin itinna ipira nanya kutin lirainin tin na dursuzu anit kitenen Yeesu tutun. Nin nanin ku Prist kudiawe nin na lena iwa di ligowe ipitrino a Yahudawe. Ligowe nin na dide na Israila. Nin kidun na ipitirino ligowe, inin tuo apolise kuti licingye inan nutuno nono kadure.
Waliposikia haya wakaenda Hekaluni alfajiri wakaendelea kufundisha watu. Kuhani mkuu na wale waliokuwa pamoja nao walipowasili, alikusanya baraza na wazee wote wa Israeli wakatuma wale mitume waletwe kutoka gerezani.
22 A me ulena awa di unan kutii licin gye yene nono kata we dikub. Nin nanin intin ikwilla udu kiti na didemine ulire.
Lakini wale walinzi wa Hekalu walipokwenda gerezani hawakuwakuta mitume mle. Kwa hiyo wakarudi na kutoa habari.
23 “Ti yene kuti licin wa kunlun kan anan sungadi wa yisin kitiy. Vat nin nanin dana tipira ti kifo anit ane tinanin se kutiye mmpono tinanin dira nanin kuti licin gye.
Wakasema, “Tumekuta milango ya gereza imefungwa sawasawa na askari wa gereza wamesimama nje ya mlango, lakini tulipofungua milango hakuwepo mtu yeyote ndani.”
24 Dana ude na kaptin kutii lira nin na Prist lanza nani, inanin wa nibinai mine tin na ni bunkurno, ilanza umamaki iyizari imon ne mati nanin.
Basi mkuu wa walinzi wa Hekalu na viongozi wa makuhani waliposikia haya, wakafadhaika na kushangaa sana kwa ajili yao kwamba jambo hili litakuwaje.
25 Umong nin da ada belle nanin “latizani! ai nene anit ane na ina ti nanin kutii licingye inanin yisin nanya Kutin lira inanin din dursuzu anite.
Ndipo mtu mmoja akaja akawaambia, “Tazameni watu mliowatia gerezani wako Hekaluni wakiwafundisha watu.”
26 Nanin ukaptin bkuti lira nuzu aduo kutin lira nin nanan kataa me, ina wa danin nono ktawe kutii ma wucuwucu mine. Nanin ma, na iwasu nanin ti kanci b. bara iwa laza fiu anite ma molu nanin nin na tala.
Ndipo yule mkuu wa walinzi wa Hekalu wakaenda pamoja na askari wakawaleta wale mitume, lakini bila ghasia kwa sababu waliogopa kupigwa mawe na watu.
27 Nin kidun ukaptin nin nanan kataa me daa nin nono katawe kuti mawucuwucu, inanin wa tii nanin iyisin mmbung nanite nanya kutii licin gye nin nanin ku Prist kudewe tirino nanin
Wakiisha kuwaleta mitume wakawaamuru kusimama mbele ya baraza ili kuhani mkuu awahoji.
28 Anin woro nanin,”Ti belin minu na iwa su madursuzu nin lisa Yesu b. inanin nari ulanzun liru bit, inanin dursuzo anite vat nanye Urshalima kitene me. Nin linbung, inanin duro anit nafo arikari dinin kulapi inkulme!
“Tuliwaonya kwa nguvu msifundishe kwa jina hili, lakini ninyi mmeijaza Yerusalemu yote mafundisho yenu na tena mmekusudia kuleta damu ya mtu huyu juu yetu.”
29 Bara nanin Bitrus, lirina mmemoku nono katawe woro,”Tima lanzu uliru ule na Kutell benle nari ti su, na ilemon na anit benle nari ti su ba!
Petro na wale mitume wengine wakajibu, “Imetupasa kumtii Mungu kuliko wanadamu.
30 Ai anigyere na molu Yesu ku nin kotigye nakusa kitene kuca koneVat nanin Kutelle kona acif bit na rugye na fea gye amini idinin lai tutun nin kidun na ana kuu.
Mungu wa baba zetu alimfufua Yesu kutoka kwa wafu, ambaye ninyi mlimuua kwa kumtundika kwenye msalaba.
31 Kutelle na antin Yesu ku nin bun nin kogy. Ana tiigye asu nari utucu nin su umulkibit. Amini na tii nanar ti cin kulapi. Bara anin shawa nin kulapi bit
Mungu alimtukuza, akamweka mkono wake wa kuume kuwa Kiongozi na Mwokozi ili awape Israeli toba na msamaha wa dhambi.
32 Tidin belu anit kitene ni lemong gyere na ina se Yesu ku. Ufunu Ulau ulena Kutelle na ninar, yinna ule ulire kiden ahri.
Nasi tu mashahidi wa mambo haya, vivyo hivyo na Roho Mtakatifu ambaye Mungu amewapa wale wanaomtii.”
33 Dana anan ma wucuwucu lanza nanin, inanin wa lanza ayii kan nin gyinu, inanin wa cinu umolu nanin
Wale wajumbe wa baraza la wazee waliposikia haya, walijawa na ghadhabu, wakataka kuwaua mitume.
34 Bara umong unit wa diku lisa me Gamaliyal. Ame ma wa di owa rum nanya na Farisawa. Ana dursuzo anit ma dudu na Yahudawe, vat a Yahudawe din lanzu infiu m, anin fitananya kuti mawucuwucu aworo, inutun nono kaduro inutun nanin udas nin kubi baat.
Lakini Farisayo mmoja, jina lake Gamalieli, aliyekuwa mwalimu wa sheria, aliyeheshimiwa na watu wote, akasimama mbele ya baraza akaamuru mitume watolewe nje kwa muda.
35 Nin kidung, itina inutuno nono kadura udas, amini wa beling usaran anan mawucuwuce,”Nuana nin Israila na ti su uhankali nin nilemon na tima su anite alele,
Ndipo alipowaambia wajumbe wa baraza, “Enyi watu wa Israeli, fikirini kwa uangalifu mnayotaka kuwatendea watu hawa.
36 Nin nakus kidung, umong lisame wa di Tidawus awa su kulapi. Amini wa beling anit ame unit ucinari, anin akut ku tocun dofingye. Inanin wa molugy, vat anit alena iwa din dortugye tin mala kiti. bara nanin na iwa yinin isu ilemon ana yinin amsu ba.
Kwa maana wakati uliopita, aliinuka mtu mmoja jina lake Theuda, alijidai kuwa yeye ni mtu maarufu, akapata wafuasi wapatao 400 walioambatana naye. Lakini aliuawa, na wafuasi wake wote wakatawanyika, wakawa si kitu.
37 Nin kidung nani, kubi kone na iwa nyerti tisa nanit na ima su, umong lisa me Yahuda, kusaring ka gbirin Galili ta kulapi amini wa tii anit idofingye. Bara nanin iwa molugye vat anit alena iwadin dortugye mala kiti kap udu nitiniti.
Baada yake, alitokea Yuda Mgalilaya wakati wa kuorodhesha watu, naye akaongoza kundi la watu kuasi. Yeye pia aliuawa, nao wafuasi wake wakatawanyika.
38 Nene in beling minu: Na lanza anite le ukule ba! Cinon nanin! Inbenle nanin bara, andi imong ilena idinsusu inuzu kitin nitar, umong ma tii nanin icin, Inanin ima diu.
Kwa hiyo, kwa habari ya jambo hili nawashauri, jiepusheni na watu hawa. Waacheni waende zao! Kwa maana kama kusudi lao na shughuli yao imetokana na mwanadamu, haitafanikiwa.
39 Andi Kutelleri taa nanin isu ile imone, na iwagya iwatina nanin use ba, bara nanin ima na se idin suugaba nin Kutele ri! Among nanya wucuwucu yina nin liri Gamalial.
Lakini ikiwa imetoka kwa Mungu, hamtaweza kuwazuia watu hawa. Badala yake mtajikuta mnapigana na Mungu.”
40 Inani wa yiccila nono kadure nanya, ikpizo nanin. Anan mawucuwucu nin kpada nani na iwa dursuzo anit kitenen Yesu tutun ba inin cino nani.
Wakapokea ushauri wa Gamalieli. Wakawaita mitume ndani, wakaamuru wachapwe mijeledi, kisha wakawaagiza wasinene tena kwa jina la Yesu, wakawaachia waende zao.
41 Nono kadure cino kiti ma wucuze, nin liburi libo kan, bara i wa yiru Kutelle angtina nanin kan nin ni nanite icin bara udortu Yesu
Nao mitume wakatoka nje ya baraza, wakiwa wamejaa furaha kwa sababu wamehesabiwa kustahili kupata aibu kwa ajili ya jina la Yesu.
42 Kolome liri nin kidun nono kadura pira kutin lira nin ni lari nanit inanin wa libun indursuzu nanite ai Yesu unaere Christe.
Kila siku, Hekaluni na nyumba kwa nyumba, hawakuacha kufundisha na kuhubiri habari njema kwamba Yesu ndiye Kristo.

< Katwa Nono Katwa 5 >