< Katwa Nono Katwa 2 >

1 Nanaya wui une a Yahudawa wadin ubuki kusana (Upentakos) mine, anan yinu sauyenu wadi kitikirum nanya Urshalima.
Siku ya Pentekoste ilipowadia, waamini wote walikuwa mahali pamoja.
2 Nin kubi kwak ilanza ufunu likara inin lanza liwui unuzu kitene kana. Anit vat kikane na iwa sosin ku ilenza ukara liwuiye.
Ghafula sauti kama mvumo mkubwa wa upepo mkali uliotoka mbinguni ukaijaza nyumba yote walimokuwa wameketi.
3 Kikanere ntutun inin yene Ufunu Ulau kitene aniti mine nafo ula. Tilem ule so kitenen kogye, umon nanya mine nuzu ada kitenen litin nanan yinnu sanu.
Zikatokea ndimi kama za moto zilizogawanyika na kukaa juu ya kila mmoja wao.
4 Vat mine kulo nin Funu Ulau, inin tinna bellu tipipin bgarden, nafo na Ufunu Ulau wa dursuzo nanin.
Wote wakajazwa na Roho Mtakatifu, wakaanza kunena kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia.
5 Kubi kone, among Ayahudawa wa sosin nanya Urshalima iniydge wadi anan fiwu Kutelleri na iwa dak nitiniti gbardan.
Basi walikuwepo Yerusalemu Wayahudi wanaomcha Mungu kutoka kila taifa chini ya mbingu.
6 Dana ilanza liwui umosin ufun, anite tinna ipitiruno kidowo kiti kirum kikana anan yinnu sauyenu wadiku. lipitirin nanite wa su umamak bara kogha nanya na nananyinu sauyenu wadin belu tipipin mine.
Waliposikia sauti hii, umati wa watu ulikusanyika pamoja wakistaajabu, kwa sababu kila mmoja wao aliwasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe.
7 Ilanza umamaki i woro nin na timine, ''Na vat alele na idin lire ina nuzu kusarin Galiliari iyiziari yinno to ti lembite?
Wakiwa wameshangaa na kustaajabu wakauliza, “Je, hawa wote wanaozungumza si Wagalilaya?
8 Vat bite tidin lanzu nanin liru nin ti pipinbite na ina maru nari mun,
Imekuwaje basi kila mmoja wetu anawasikia wakinena kwa lugha yake ya kuzaliwa?
9 among bite na nuzu kusarin Patia nin Midia au Elam, among nanya bite nuzukusarin Umesopotamia, Uyahudia, Cappadocia, Pentus nin Uasia.
Wapathi, Wamedi, Waelami, wakazi wa Mesopotamia, Uyahudi, Kapadokia, Ponto na Asia,
10 Kikane among anit wa nuzu kusarin Firizia nin Panfilia, Umasar nin kusarin kagbirin libia idadas nin kagbirin Cirian. Kikane among bite amara Urshalima unuzun Roma.
Frigia, Pamfilia, Misri na pande za Libya karibu na Kirene na wageni kutoka Rumi,
11 Umunu nin na Yahudawe, au a Yahudawa na ina yinin nin nilemong na arik a Yahudawe yinamung. Among bite nuzu kusarin Island na Krete nin kusarin ka gbirin Arabia. Bari yan-aarin ta ale anite din belu tipipin bite kitene nilemong na Kutelle nasua?
Wayahudi na waongofu, Wakrete na Waarabu, sote tunawasikia watu hawa wakisema mambo makuu ya ajabu ya Mungu katika lugha zetu wenyewe.”
12 Anite wa lanza umamaki na iwa yininin yari neba itin na tiru natimine “Ile imone yaria?”
Wakiwa wameshangaa na kufadhaika wakaulizana, “Ni nini maana ya mambo haya?”
13 Among many mine imagining wish nanin lninworo, “Ale white din lirunafo isono intoro moninmolo naninkan!”
Lakini wengine wakawadhihaki wakasema, “Hawa wamelewa divai!”
14 Bitrus fita alirina kan aworo anan lipitin; nanite, “Anin anan Yahudia nin nalenaisosin in Urshalima, ma Latiszannin vat mine, ima benlinminu ilemong idin yenju.
Ndipo Petro akasimama pamoja na wale mitume kumi na mmoja, akainua sauti yake na kuhutubia ule umati wa watu, akasema: “Wayahudi wenzangu na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, jueni jambo hili mkanisikilize.
15 Among nanya mine din du untoro molo nari nanere ba ai nene kubi karfe tarari nin kudin, anit alele sonon utoro nin kokubi nin lolire ba!
Hakika watu hawa hawakulewa kama mnavyodhania, kwa kuwa sasa ni saa tatu asubuhi!
16 Bara nanin elemon na iyene kiti bite ina malin yertinu ku annabi Joel na belin uworu.
La, hili ni jambo lililotabiriwa na nabii Yoeli, akisema:
17 Kubi nayiru nimalin gye, Ima niUfunu Ulau kiti nanite vat, ason nin na shono mine ma belu anite kadura ningye, Inani anyana mine uyejun, akune inma ninanin amoron yenju kiti.
“‘Katika siku za mwisho, asema Mungu, nitamimina Roho wangu juu ya wote wenye mwili. Wana wenu na binti zenu watatabiri, vijana wenu wataona maono, na wazee wenu wataota ndoto.
18 Kubi nayira ne ima ni Ufunu Ulau kiti nono nin, inan bele anit tipipin nin.
Hata juu ya watumishi wangu, wanaume kwa wanawake, katika siku zile nitamimina Roho wangu, nao watatabiri.
19 Imati imong idiya ti kitene kani, nin kutin idurso minu imong icine naimase. Kikane kutin, mmi nin ula nin cin vat niti.
Nami nitaonyesha maajabu juu mbinguni, na ishara chini duniani: damu, moto, na mawimbi ya moshi.
20 Kite kane ma ti uwui uti bibit kiti na nit nin pui uti ushine nafo kiti mine. Umong ine mati ma innin dak ida, Men Kutelle manin dak ida su mawusuwusu. kitin konyge.
Jua litakuwa giza na mwezi utakuwa mwekundu kama damu, kabla ya kuja siku ile kuu ya Bwana iliyo tukufu.
21 Iminin ma tucu anit alena idin yici in bin nanin.'”
Na kila mtu atakayeliitia jina la Bwana, ataokolewa.’
22 Bitrus tin alau ubin in lire,”Nuana nin a Iraila latizani! Kubi kona Yesu nazaret wa di nan yginu Kutelle na dura minu amere na tuu gye a su matiza ma zikiki mane maana maanaduro amere KutelleAnin natimene yiru nin limo umongye kidene.
“Enyi Waisraeli, sikilizeni maneno haya nisemayo: Yesu wa Nazareti alikuwa mtu aliyethibitishwa kwenu na Mungu kwa miujiza, maajabu na ishara, ambayo Mungu alitenda miongoni mwenu kupitia kwake, kama ninyi wenyewe mjuavyo.
23 Nin nanin iyiru, anin gyere na nakwa Yesu ku kiti nanan ni vira me. Nin nanin Kutelle na malin yinu mu, amini yiru nin nimone. Inin taa anit alena iyiru nin udoka Kutelle ba anan molo Yesu ku. Inani wa kotin gye akusa kite kuca.
Huyu mtu akiisha kutolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa kwa kujua kwake Mungu tangu zamani, ninyi, kwa mikono ya watu wabaya, mlimuua kwa kumgongomea msalabani.
24 Amini na kuu, Kutelle na feagye tutun, bara nanin ukul wagya kifo gye kutinba. Kutelle nati Yesu afita tutun.
Lakini Mungu alimfufua kutoka kwa wafu akamwondolea uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana yeye kushikiliwa na nguvu za mauti.
25 Tuntuni ugo Dauda na yertin kitenen Missiah aworo,”In yiru fewe ku Kutelle, uma lanzi kokome kubi, idi kusa nin mina ima lanzu infiu na le na iin su ivira nin mi ba.
Kwa maana Daudi asema kumhusu yeye: “‘Nalimwona Bwana mbele yangu daima. Kwa sababu yuko mkono wangu wa kuume, sitatikisika.
26 Bara nanin kibinai nin ma ti pau, konin kul nin, inyiru uma buni.
Kwa hiyo moyo wangu unafurahia, na ulimi wangu unashangilia; mwili wangu nao utapumzika kwa tumaini.
27 Uma cini kikana anan kule diku ba. Na uma kuru cin kidawo nin bijuba, bara idi ni fi nin dortu fi nin su ubiyanya' (Hadēs g86)
Kwa maana hutaniacha kaburini, wala hutamwacha Aliye Mtakatifu wako kuona uharibifu. (Hadēs g86)
28 Una malin benle tibou tona ima dfunu ina taa ulai tutun. Umati kibinai nin ti paubara udi nin me sa ligan.
Umenionyesha njia za uzima, utanijaza na furaha mbele zako.’
29 Nuana, nwasa nlira nanghinu sa fiu kitenen kaa bite Dauda: awa ku ikuru ikasaghe, kissek me di nanghirik udak kitimone.
“Ndugu zangu Waisraeli, nataka niwaambie kwa uhakika kwamba baba yetu Daudi alikufa na kuzikwa, nalo kaburi lake lipo hapa mpaka leo.
30 Bara nani, awadi gono katwa Kutelleri ayiro nwo Kutelle wasughe issilin, nworu ama ceo umong nanya fisudu me kitenen kutet tigo.
Lakini alikuwa nabii na alijua ya kuwa Mungu alikuwa amemwahidi kwa kiapo kwamba angemweka mmoja wa wazao wake penye kiti chake cha enzi.
31 Awa yene ile imone, alira nbellen fitun Kristi nanya nkul, 'Na iwa shawa ninghe nanya kisseke ba, ana na kidowo me wa yene ubiju ba.' (Hadēs g86)
Daudi, akiona mambo yaliyoko mbele, akanena juu ya kufufuka kwa Kristo, kwamba hakuachwa kaburini, wala mwili wake haukuona uharibifu. (Hadēs g86)
32 Nin kidun ame Yesu na kuu. Kutelle na fegye tutu. Vat arik anan dortu gyer, tiru mung bara tina yeneyge.
Mungu alimfufua huyu Yesu na sisi sote ni mashahidi wa jambo hilo.
33 Kutelle na Yesu kutet kudiya amini na ce gye incara ulime me asu ti goo nin Cife. Amini na niri Ufunu Ulau unere taa idin yenju nin lan ze.
Basi ikiwa yeye ametukuzwa kwa mkono wa kuume wa Mungu, amepokea kutoka kwa Baba ahadi ya Roho Mtakatifu, naye amemimina kile mnachoona sasa na kusikia.
34 Tiyiru kap Dauda wadin liru litimere b, bara ame Dauda na duo kitene ba nafo Yesu, nin nanin wang. Dauda litime na be3ling uliru kitene Yesu amere Missiah. Cikilari Kutelle na bwabelin Cikilari nin Missia, su tigo in cara ulime nin
Kwa kuwa Daudi hakupaa kwenda mbinguni, lakini anasema, “‘Bwana alimwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume,
35 Ma inin kata likara nanan ni vira nin.”
hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”’
36 Bitrus nin mala uliru me aworo,”idinin suo iyini vat a Israila Kutelle nati Yesu ku asuo Cikilari nin Missiah, Yesu unere ulena iwa kotinyge ti kusa kitene kuca inin mologye.
“Kwa hiyo Israeli wote na wajue jambo hili kwa uhakika kwamba: Mungu amemfanya huyu Yesu, ambaye ninyi mlimsulubisha, kuwa Bwana na Kristo.”
37 Dana anite lanza elemon na Bitruse nin nanan kadura benle, iyino ita kulapi, inin woro nanin iyeri tima ti nene?
Watu waliposikia maneno haya yakawachoma mioyo yao, wakawauliza Petro na wale mitume wengine, “Ndugu zetu tufanye nini?”
38 Bitrus nin kwana nani, vat mine icin kulapi min, Andi iyinna nin yise tima su minu ubaptizma. Kutelle ma ma yashu nin kulapi mine, ani niminu Ufunu Ulau Me.
Petro akawajibu, “Tubuni, mkabatizwe kila mmoja wenu kwa jina la Yesu Kristo, ili mpate kusamehewa dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
39 Kutelle na malin su likawali amanimunu har nin nono mine nin na nela iyina nin Yesu nin nalena idi pii kusari kikane. Cikilari bite Kutelle mani Ufunu Ulau nin na lena a yicila gye uniti me.
Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu na watoto wenu, na kwa wote walio mbali, na kila mtu ambaye Bwana Mungu wetu atamwita amjie.”
40 Bitrus wa liru kang kiti mine, Anin woro nanin “Tirinon Kutelle anan shawa [yape]minu bara awan nimunu kikanci nafo ale anite na inanari Yesu ku.
Petro akawaonya kwa maneno mengine mengi na kuwasihi akisema, “Jiepusheni na kizazi hiki kilichopotoka.”
41 Anite na iwa yinin sa yenu nin liru Bitrus iwa ti ubaptisma. Anan yinu sa uyenu kpina kan har timui ti tat, unwui une.
Wale wote waliopokea ujumbe wa Petro kwa furaha wakabatizwa na siku ile waliongezeka watu wapatao 3,000.
42 Eliu ubun nanya indurtu nilemon na iwa dueso nani. Iwa din ga uzursuzu kookome kubi inin namong anan yinu sauyenu kikane ici liu emonli ligowe nin nin ti lira ligowe kiti kirem kolome liri.
Nao wakawa wanadumu katika mafundisho ya mitume, katika ushirika, katika kumega mkate na katika kusali.
43 Vat anite na iwa din nanya Ushalima ifio kifo nanin nin kata ka zikiki na almajaraye wadin sua nin lisa yesu.
Kila mtu akaingiwa na hofu ya Mungu, nayo miujiza mingi na ishara zikafanywa na mitume.
44 Vat na rika na iwa yinin warsu ko nyan ligowe. Inin leu ubun kosusu nin ligawe.
Walioamini wote walikuwa mahali pamoja, nao walikuwa na kila kitu shirika.
45 Unuzu kubikubi kogha lese anen me adasamu kiti nanan katawe. Nin nimong ile na kogha nadimun
Waliuza mali zao na vitu walivyokuwa navyo, kila mtu akagawiwa kadiri ya mahitaji yake.
46 Ko kishi iwa din zursusu kiti lira kikaneIwa li umonli ligowe ni picu nilari nilari. kubi kona isu nanin ni binai mine taah pau [lanza man ini niza ilemong na kogha diman lgowe.
Siku zote kwa moyo mmoja walikutana ndani ya ukumbi wa Hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, wakila chakula chao kwa furaha na moyo mweupe,
47 Dana su nani, ie ubung zazunu Kutell. Nin nanin vat anit Urshalima nananin ubagirma kubikona imong ine wa linbub ghe anan biye kwina kang kolome liri bara use utucu kusari kulapi mine.
wakimsifu Mungu na kuwapendeza watu wote. Kila siku Bwana akaliongeza kanisa wale waliokuwa wakiokolewa.

< Katwa Nono Katwa 2 >