< Süleyman'In Özdeyişleri 24 >

1 Kötülere imrenme, Onlarla birlikte olmayı isteme.
Usiwaonee wivu watu waovu, usitamani ushirika nao;
2 Çünkü yürekleri zorbalık tasarlar, Dudakları belalardan söz eder.
kwa maana mioyo yao hupanga mambo ya jeuri, nayo midomo yao husema juu ya kuleta madhara.
3 Ev bilgelikle yapılır, Akılla pekiştirilir.
Kwa hekima nyumba hujengwa, nayo kwa njia ya ufahamu huimarishwa
4 Bilgi sayesinde odaları Her türlü değerli, güzel eşyayla dolar.
kwa njia ya maarifa vyumba vyake hujazwa vitu vya thamani na vya kupendeza.
5 Bilgelik güçten, Bilgi kaba kuvvetten üstündür.
Mtu mwenye hekima ana uwezo mkubwa, naye mtu mwenye maarifa huongeza nguvu,
6 Savaşmak için yöntem, Zafer kazanmak için birçok danışman gerekli.
kwa kufanya vita unahitaji uongozi na kwa ushindi washauri wengi.
7 Ahmak için bilgelik ulaşılamayacak kadar yüksektir, Kent kurulunda ağzını açamaz.
Hekima i juu mno kwa mpumbavu, katika kusanyiko langoni hana lolote la kusema.
8 Kötülük tasarlayan kişi Düzenbaz olarak bilinecektir.
Yeye apangaye mabaya atajulikana kama mtu wa hila.
9 Ahmakça tasarılar günahtır, Alaycı kişiden herkes iğrenir.
Mipango ya upumbavu ni dhambi, watu huchukizwa na mwenye dhihaka.
10 Sıkıntılı günde cesaretini yitirirsen, Gücün kıt demektir.
Ukikata tamaa wakati wa taabu, jinsi gani nguvu zako ni kidogo!
11 Ölüm tehlikesi içinde olanları kurtar, Ölmek üzere olanları esirge.
Okoa wale wanaoongozwa kwenye kifo; wazuie wote wanaojikokota kuelekea machinjoni.
12 “İşte bunu bilmiyordum” desen de, İnsanın yüreğindekini bilen sezmez mi? Senin canını koruyan anlamaz mı? Ödetmez mi herkese yaptığını?
Kama mkisema, “Lakini hatukujua lolote kuhusu hili,” je, yule apimaye mioyo halitambui hili? Je, yule awalindaye maisha yenu halijui hili? Je, hatamlipa kila mtu kulingana na aliyotenda?
13 Oğlum, bal ye, çünkü iyidir, Süzme bal damağa tatlı gelir.
Ule asali mwanangu, kwa kuwa ni nzuri; asali kutoka kwenye sega ni tamu kwa kuonja.
14 Bilgelik de canın için öyledir, bilmiş ol. Bilgeliği bulursan bir geleceğin olur Ve umudun boşa çıkmaz.
Ujue pia kwamba hekima ni tamu kwa nafsi yako, kama ukiipata, kuna matumaini kwako ya siku zijazo, nalo tumaini lako halitakatiliwa mbali.
15 Ey kötü adam, doğru kişinin evine karşı pusuya yatma, Konutunu yıkmaya kalkma.
Usivizie kama haramia afanyavyo ili kuyashambulia makao ya mwenye haki, wala usiyavamie makazi yake,
16 Çünkü doğru kişi yedi kez düşse yine kalkar, Ama kötüler felakette yıkılır.
Kwa maana ingawa mtu mwenye haki huanguka mara saba, huinuka tena, lakini waovu huangushwa chini na maafa.
17 Düşmanın düşüşüne keyiflenme, Sendelemesine sevinme.
Usitazame kwa kufurahia adui yako aangukapo; wakati ajikwaapo, usiruhusu moyo wako ushangilie.
18 Yoksa RAB görür ve hoşnut kalmaz Ve düşmanına duyduğu öfke yatışır.
Bwana asije akaona na kuchukia akaiondoa ghadhabu yake mbali naye.
19 Kötülük edenlere kızıp üzülme, Onlara özenme.
Usikasirike kwa sababu ya watu wabaya wala usiwaonee wivu waovu,
20 Çünkü kötülerin geleceği yok, Çırası sönecek onların.
kwa maana mtu mbaya hana tumaini la siku zijazo, nayo taa ya waovu itazimwa.
21 Oğlum, RAB'be ve krala saygı göster, Onlara başkaldıranlarla arkadaşlık etme.
Mwanangu, mche Bwana na mfalme, wala usijiunge na waasi,
22 Çünkü onlar ansızın felakete uğrar, İnsanın başına ne belalar getireceklerini kim bilir?
kwa maana hao wawili watatuma maangamizi ya ghafula juu yao, naye ni nani ajuaye maafa wawezayo kuleta?
23 Şunlar da bilgelerin sözleridir: Yargılarken yan tutmak iyi değildir.
Hii pia ni misemo ya wenye hekima: Kuonyesha upendeleo katika hukumu si vyema:
24 Kötüye, “Suçsuzsun” diyen yargıcı Halklar lanetler, uluslar kınar.
Yeyote amwambiaye mwenye hatia, “Wewe huna hatia,” Kabila zitamlaani na mataifa yatamkana.
25 Ne mutlu suçluyu mahkûm edene! Herkes onu candan kutlar.
Bali itakuwa vyema kwa wale watakaowatia hatiani wenye hatia, nazo baraka tele zitawajilia juu yao.
26 Dürüst yanıt Gerçek dostluğun işaretidir.
Jawabu la uaminifu ni kama busu la midomoni.
27 İlkin dışardaki işini bitirip tarlanı hazırla, Ondan sonra evini yap.
Maliza kazi zako za nje, nawe uweke mashamba yako tayari, baada ya hayo, jenga nyumba yako.
28 Başkalarına karşı nedensiz tanıklık etme Ve dudaklarınla aldatma.
Usishuhudie dhidi ya jirani yako bila sababu, au kutumia midomo yako kudanganya.
29 “Bana yaptığını ben de ona yapacağım, Ödeteceğim bana yaptığını” deme.
Usiseme, “Nitamtenda kama alivyonitenda mimi; nitamlipiza mtu yule kwa kile alichonitendea.”
30 Tembelin tarlasından, Sağduyudan yoksun kişinin bağından geçtiğimde
Nilipita karibu na shamba la mvivu, karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili,
31 Her yanı dikenlerin, otların Kapladığını gördüm; Taş duvar da yıkılmıştı.
miiba ilikuwa imeota kila mahali, ardhi ilikuwa imefunikwa na magugu, na ukuta wa mawe ulikuwa umebomoka.
32 Gördüklerimi derin derin düşündüm, Seyrettiklerimden ibret aldım.
Nikatafakari moyoni mwangu lile nililoliona, nami nikajifunza somo kutokana na niliyoyaona:
33 “Biraz kestireyim, biraz uyuklayayım, Ellerimi kavuşturup şöyle bir uyuyayım” demeye kalmadan,
Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
34 Yokluk bir haydut gibi, Yoksulluk bir akıncı gibi gelir üzerine.
hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.

< Süleyman'In Özdeyişleri 24 >