< Yaratiliş 23 >
1 Sara yüz yirmi yedi yıl yaşadı. Ömrü bu kadardı.
Sara aliishi akawa na umri wa miaka mia na ishirini na saba.
2 Kenan ülkesinde, bugün Hevron denilen Kiryat-Arba'da öldü. İbrahim yas tutmak, ağlamak için Sara'nın ölüsünün başına gitti.
Sara akafa huko Kiriath-Arba (yaani Hebroni) katika nchi ya Kanaani, Abrahamu akamwombolezea na kumlilia Sara.
3 Sonra karısının ölüsünün başından kalkıp Hititler'e,
Ndipo Abrahamu akainuka kutoka pale penye maiti ya mke wake. Akazungumza na Wahiti, akasema,
4 “Ben aranızda konuk ve yabancıyım” dedi, “Bana mezar yapabileceğim bir toprak satın. Ölümü kaldırıp gömeyim.”
“Mimi ni mpitaji na mgeni miongoni mwenu. Niuzieni sehemu ya ardhi yenu ili niweze kumzika maiti wangu.”
5 Hititler, “Efendim, bizi dinle” diye yanıtladılar, “Sen aramızda önemli bir beysin. Ölünü mezarlarımızın en iyisine göm. Ölünü gömmen için kimse senden mezarını esirgemez.”
Wahiti wakamjibu Abrahamu,
“Bwana, tusikilize. Wewe ni mtawala mkuu sana miongoni mwetu. Zika maiti wako katika kaburi unalolipenda kati ya makaburi yetu. Hakuna mtu wa kwetu atakayekuzuia kaburi lake ili kuzika maiti wako.”
7 İbrahim, ülke halkı olan Hititler'in önünde eğilerek,
Abrahamu akainuka na akasujudu mbele ya wenyeji wa nchi, yaani Wahiti.
8 “Eğer ölümü gömmemi istiyorsanız, benim için Sohar oğlu Efron'a ricada bulunun” dedi,
Akawaambia, “Kama mnaniruhusu kumzika maiti wangu, basi nisikilizeni mkamsihi Efroni mwana wa Sohari kwa niaba yangu
9 “Tarlasının dibindeki Makpela Mağarası'nı bana satsın. Fiyatı neyse huzurunuzda eksiksiz ödeyip orayı mezarlık yapacağım.”
ili aniuzie pango la Makpela, lililo mali yake, nalo liko mwisho wa shamba lake. Mwambieni aniuzie kwa bei kamili atakayosema ili liwe mahali pangu pa kuzikia miongoni mwenu.”
10 Hititli Efron halkının arasında oturuyordu. Kent kapısında toplanan herkesin duyacağı biçimde,
Efroni Mhiti alikuwa ameketi miongoni mwa watu wake, akamjibu Abrahamu mbele ya Wahiti wote waliokuwepo katika lango la mji.
11 “Hayır, efendim!” diye karşılık verdi, “Beni dinle, mağarayla birlikte tarlayı da sana veriyorum. Halkımın huzurunda onu sana veriyorum. Ölünü göm.”
“La hasha, bwana wangu, nisikilize, nakupa shamba, pia nakupa pango lililomo ndani yake. Nakupa mbele ya watu wangu. Uzike maiti wako.”
12 İbrahim ülke halkının önünde eğildi.
Abrahamu akasujudu tena, mbele ya wenyeji wa nchi,
13 Herkesin duyacağı biçimde Efron'a, “Lütfen beni dinle” dedi, “Tarlanın parasını ödeyeyim. Parayı kabul et ki, ölümü oraya gömeyim.”
akamwambia Efroni wale watu wakiwa wanasikia, “Tafadhali nisikilize. Nitakulipa fedha za hilo shamba. Kubali kuzipokea ili niweze kumzika maiti wangu.”
14 Efron, “Efendim, beni dinle” diye karşılık verdi, “Aramızda dört yüz şekel gümüşün sözü mü olur? Ölünü göm.”
Efroni akamjibu Abrahamu,
“Nisikilize, bwana wangu, thamani ya ardhi hiyo ni shekeli 400 za fedha, lakini hiyo ni nini kati yako na mimi? Mzike maiti wako.”
16 İbrahim Efron'un önerisini kabul etti. Efron'un Hititler'in önünde sözünü ettiği dört yüz şekel gümüşü tüccarların ağırlık ölçülerine göre tarttı.
Abrahamu akakubali masharti ya Efroni, akampimia ile fedha aliyotaja masikioni mwa Wahiti: Shekeli 400 za fedha kulingana na viwango vya uzito vilivyokuwa vikitumika wakati huo na wafanyabiashara.
17 Böylece Efron'un Mamre yakınında Makpela'daki tarlası, çevresindeki bütün ağaçlarla ve içindeki mağarayla birlikte, kent kapısında toplanan Hititler'in huzurunda İbrahim'in mülkü kabul edildi.
Hivyo shamba la Efroni huko Makpela karibu na Mamre, yaani shamba pamoja na pango lililokuwamo, nayo miti yote iliyokuwamo ndani ya mipaka ya shamba hilo, vilikabidhiwa,
kwa Abrahamu kuwa mali yake mbele ya Wahiti wote waliokuwa wamekuja kwenye lango la mji.
19 İbrahim karısı Sara'yı Kenan ülkesinde Mamre'ye –Hevron'a– yakın Makpela Tarlası'ndaki mağaraya gömdü.
Baada ya hayo Abrahamu akamzika Sara mkewe kwenye pango ndani ya shamba la Makpela karibu na Mamre (huko Hebroni) katika nchi ya Kanaani.
20 Hititler tarlayı içindeki mağarayla birlikte İbrahim'in mezarlık yeri olarak onayladılar.
Hivyo Wahiti wakamkabidhi Abrahamu shamba pamoja na pango lililokuwa humo kuwa mahali pa kuzikia.