< Zekaria 13 >
1 Katika siku hiyo kijito kitafunguliwa kwa ajili ya nyumba ya Daudi na wenyeji wa Yerusalemu, kwa ajili ya dhambi na uchafu wao.
En ce temps-là il y aura une source ouverte en faveur de la maison de David, et des habitants de Jérusalem, pour le péché, et pour la souillure.
2 Katika siku hiyo - asema Yahwe wa majeshi - kwamba nitaondoa majina ya sanamu katika nchi ili kwamba yasikumbukwe tena. Nitawaondoa pia katika nchi manabii wa uongo na roho wao mchafu
Il arrivera aussi en ce temps-là, dit l'Eternel des armées, que je retrancherai du pays les noms des faux dieux; et on n'en fera plus mention; j'ôterai aussi du pays les [faux] prophètes, et l'esprit d'impureté.
3 Ikiwa mtu yeyote ataendelea kutoa unabii, baba yake na mama yake waliomzaa watamwambia, 'Hautaishi, kwa kuwa umenena uongo kwa jina la Yahwe! Ndipo baba na mama waliomzaa watakapomchoma wakati akitabiri.
Et il arrivera que quand quelqu'un prophétisera dorénavant, son père et sa mère qui l'auront engendré, lui diront: Tu ne vivras plus; car tu as prononcé des mensonges au Nom de l'Eternel; et son père et sa mère qui l'auront engendré, le transperceront quand il prophétisera.
4 Katika siku hiyo kila nabii ataonea aibu maono yake aelekeapo kutoa unabii. Manabii hawa hawatavaa tena vazi la singa, ili kuwadanganya watu.
Et il arrivera en ce temps-là que ces prophètes seront confus chacun de sa vision, quand il aura prophétisé; et ils ne seront plus vêtus de manteau de poil, pour mentir.
5 Kwa maana kila mmoja atasema, 'Mimi siyo nabii! mimi ni mkulima, kwa maana ardhi ndiyo kazi yangu tangu ujana wangu!
Et il dira: Je ne suis point prophète, [mais] je suis un laboureur; car on m'a appris à gouverner du bétail dès ma jeunesse.
6 Lakini mtu mwingine atamwambia, 'Majeraha haya kati ya mikono yako ni ya nini?' naye atajibu, nilijeruhiwa na waliokuwa katika nyumba ya rafiki zangu.”
Et on lui dira: Que veulent donc dire ces blessures en tes mains? Et il répondra: Ce sont celles qui m'ont été faites dans la maison de mes amis.
7 Upanga! inuka mwenyewe dhidi ya mchungaji wangu, mtu asimamaye karibu nami - hivi ndivyo asemavyo Yahwe wa majeshi. Mpige mchungaji, na kondoo watatawanyika! Kwa maana nitageuza mkono wangu dhidi ya wadogo.
Epée, réveille-toi sur mon Pasteur, et sur l'homme qui est mon compagnon, dit l'Eternel des armées; frappe le Pasteur, et les brebis seront dispersées, et je tournerai ma main sur les petits.
8 Kisha itakuwa kwamba katika nchi yote - hivi ndivyo asemavyo Yahwe - kwamba theluthi mbili yake itaondolewa! Watu hao wataangamia; theluthi moja tu ndiyo itakayosalia.
Et il arrivera dans toute la terre, dit l'Eternel, que deux parties seront retranchées en elle, et défaudront, mais la troisième y demeurera de reste.
9 Nitaipitisha hiyo ya tatu motoni na kuwasafisha kama fedha isafishwavyo; nitawajaribu kama dhahabu ijaribiwavyo. Wataliitia jina langu nami nitawajibu na kusema, 'Hawa ni watu wangu!' nao watasema, Yahwe ndiye Mungu wangu!”
Et j'amènerai la troisième partie au feu, je les affinerai comme on affine l'argent, et je les éprouverai comme on éprouve l'or, chacun d'eux invoquera mon Nom, et je l'exaucerai; je dirai: C'est [ici] mon peuple; et il dira: L'Eternel est mon Dieu.