< Tito 1 >

1 Paulo, mtumishi wa Mungu na mtume wa Yesu Kristo, kwa imani ya wateule wa Mungu na maarifa ya kweli iletayo utauwa.
PAUL, a servant of God, and an apostle of Jesus Christ, according to the faith of the elect of God, and the knowledge of truth which leads to godliness;
2 Wapo katika tumaini la uzima wa milele ambao Mungu asiyeweza kusema uongo aliuahidi tangu milele. (aiōnios g166)
in hope of life eternal, which God, who cannot lie, hath promised before time had a being; (aiōnios g166)
3 Kwa wakati muafaka, alilifunua neno lake katika ujumbe alionipa mimi kuhubiri. Ilinipasa kufanya hivi kwa amri ya Mungu mwokozi wetu.
but hath manifested in his own appointed season his word by the preaching, with which I have been entrusted, according to the command of our Saviour God;
4 Kwa Tito, mwana wa kweli katika imani yetu. Neema, huruma na amani kutoka kwa Mungu Baba na Yesu Kristo mwokozi wetu.
to Titus, my genuine son after the common faith, be grace, mercy, peace, from God the Father and our Lord Jesus Christ our Saviour.
5 Kwa sababu hii nalikuacha Krete, kwamba uyatengeneze mambo yote yaliyokuwa hayajakamilika na kuweka wazee wa kanisa kwa kila mji kama nilivyokuagiza.
For this purpose I left thee behind me at Crete, that thou mightest direct the regulations which remained to be executed, and that thou shouldest appoint presbyters in every city, as I charged thee to do:
6 Mzee wa kanisa lazima asiwe na lawama, mme wa mke mmoja, aliye na watoto waaminifu wasioshuhudiwa mabaya au wasio na nidhamu.
if there be a man blameless, the husband of one wife, having children who believe, not under an accusation or debauchery, or disorderly conduct.
7 Ni muhimu kwa mwangalizi, kama msimamizi wa nyumba ya Mungu, asiwe na lawama. Asiwe mtu wa kelele au asiye jizuia. Lazima asiwe mwepesi wa hasira, asiwe mlevi, asiwe mtu wa kusababisha ugomvi, na asiwe mwenye tamaa.
For a bishop ought to be irreproachable, as the steward of God; not self-willed, not irritable, not addicted to wine, not quarrelsome, not greedy of filthy lucre;
8 Badala yake: awe mtu mkaribishaji, apendaye wema. Lazima awe mtu mwenye akili timamu, mwenye haki, mcha Mungu, anayejitawala mwenyewe.
but the stranger’s host, the good man’s friend, grave, just, holy, temperate;
9 Awezaye kusimamia mafundisho ya kweli yaliyofundishwa, ili aweze kuwatia moyo kwa mafundisho mazuri na awezaye kuwarekebisha wote wanaompinga.
firmly attached to the faithful word, according to the doctrine delivered, that he may be able to exhort with sound instruction and to confute the opposers.
10 Kwa kuwa kuna waasi wengi, hasa wale wa tohara. Maneno yao ni ya upuuzi. Wanadanganya na kuwaongoza watu katika upotovu.
For there are many disorderly persons vainly talkative, and under a spirit of delusion, especially some of the circumcised;
11 Ni lazima kuwazuia watu kama hao. Wanafundisha yale wasiyopaswa kwa faida za aibu na kuharibu familia zote.
whose mouths ought to be muzzled, who pervert whole families, teaching things which they ought not, for the sake of base gain.
12 Mmoja wao, mtu mwenye busara, alisema, “Wakrete wana uongo usio na mwisho, wabaya na wanyama wa hatari, wavivu na walafi.”
One of them, a poet of their own nation, hath said, The Cretans are always liars, wicked beasts, slothful gluttons.
13 Haya maelezo ni ya kweli, kwa hiyo uwazuie kwa nguvu ili kwamba waweze kusema kweli katika imani.
This testimony is true. For which cause rebuke them with severity, that they may be sound in the faith;
14 Wewe usijihusishe na hadithi zisizo za kweli za Kiyahudi au amri za watu, ambao hurudisha nyuma ukweli.
not attending to Jewish fables, and injunctions of men, who have turned away from the truth.
15 Kwa wote walio safi, vitu vyote ni visafi. Lakini kwa wote walio wachafu na wasioamini, hakuna kilicho kisafi. Kwa kuwa mawazo yao na dhamira zao zimechafuliwa.
All things indeed are clean to the clean: but to the defiled and to the unbelievers there is nothing clean; but their very mind and conscience are defiled.
16 Wanakiri kumjua Mungu, lakini kwa matendo yao wanamkana. Wao ni waovu na wasiotii. Hawakuthibitishwa kwa tendo lolote jema.
They profess to know God; but in works deny him, being abominable and disobedient, and unto every good work reprobate.

< Tito 1 >