< Ufunuo 19 >
1 Baada ya mambo haya nilisikia sauti kama ya mlio mkubwa wa kundi kubwa la watu mbinguni ikisema, “Haleluya. Wokovu, utukufu, na nguvu ni vya Mungu wetu.
After these things I heard as it were the really loud voice of a great multitude in heaven saying: “Hallelujah! The salvation and power and glory of our God!
2 Hukumu zake ni kweli na za haki, kwa kuwa amemhukumu kahaba mkuu aliyeiharibu nchi kwa uzinzi wake. Amefanya kisasi kwa damu ya watumishi wake, ambayo aliimwaga yeye mwenyewe.”
Because His judgments are true and just, because He has judged the great whore who corrupted the earth with her fornication, and has avenged the blood of His slaves by her hand.”
3 Kwa mara ya pili walisema, “Haleluya! Moshi hutoka kwake milele na milele.” (aiōn )
And a second voice said, “Hallelujah! Her smoke goes up for ever and ever!” (aiōn )
4 Wale wazee ishirini na wanne na viumbe hai wanne wakasujudu na kumwabudu Mungu akaaye kwenye kiti cha enzi. Walikuwa wakisema, “Amina. Haleluya!”
And the twenty-four elders and the four living beings fell down and worshiped God, who sits on the throne, saying, “Amen, Hallelujah!”
5 Ndipo sauti ilitoka kwenye kiti cha enzi, ikisema, “Msifuni Mungu wetu, enyi watumishi wake wote, ninyi mnaomcha yeye, wote wasio na umuhimu na wenye nguvu.”
And a voice came from the Throne saying, “Praise our God, all you His slaves and those who fear Him, small and great!”
6 Ndipo nilisikia sauti kama sauti ya kundi kubwa la watu, kama sauti ya ngurumo ya maji mengi, na kama ngurumo ya radi, ikisema, “Haleluya! Bwana ni Mungu wetu, mtawala juu ya wote, hutawala.
And I heard as it were the voice of a great multitude like the sound of many waters and like the sound of mighty thunderings saying: “Hallelujah! Because the Lord our God reigns, the Almighty!
7 Na tushangilie na kufurahi na kumpa utukufu kwa sababu harusi na sherehe ya Mwana Kondoo imekuja, na bibi harusi yuko tayari.”
Let us rejoice and exult and give Him the glory, because the wedding of the Lamb has come, and His wife has prepared herself.”
8 Aliruhusiwa kuvalishwa kitani safi na yenye kung'aa (kitani safi ni matendo ya haki ya waumini).
And it was granted to her to be dressed in fine linen, bright and pure, for the fine linen is the righteous deeds of the saints.
9 Malaika akasema nami, “Yaandike haya: Wamebarikiwa walioalikwa kwenye sherehe ya harusi ya Mwana kondoo.” Vilevile akaniambia, “Haya ni maneno ya kweli ya Mungu.”
And he says to me, “Write: ‘Blessed are those who are invited to the wedding banquet of the Lamb.’” And he says to me, “These are the true words of God.”
10 Nilisujudu mbele ya miguu yake nikamwabudu, lakini akaniambia, “Usifanye hivi! Mimi ni mtumishi mwenzako na wa ndugu zako mwenye kuushika ushuhuda wa Yesu. Mwabudu Mungu, kwa kuwa ushuhuda wa Yesu ni roho ya unabii.”
And I fell at his feet to worship him, but he says to me: “Don't! I am your fellow slave and among your brothers who hold the testimony of Jesus. Worship God! For the testimony of Jesus is the spirit of prophecy.”
11 Kisha niliona mbingu zimefunguka, na tazama kulikuwa na farasi mweupe! Na yule aliyekuwa amempanda anaitwa Mwaminifu na wa Kweli. Huhukumu kwa haki na kufanya vita.
I saw the heaven opened, and wow, a white horse! And the One who sits on it, called Faithful and True, both judges and makes war with righteousness.
12 Macho yake ni kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake ana taji nyingi. Ana jina lililoandikwa juu yake asilolifahamu mtu yeyote isipokuwa yeye mwenyewe.
Now His eyes were a flame of fire and on His head were many diadems, having names written, besides a written name that no one knows except Himself;
13 Amevaa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aliitwa Neno la Mungu.
and He was clothed with a robe that had been dipped in blood, and His name is called The Word of God.
14 Majeshi ya mbinguni yalikuwa yakimfuata juu ya farasi weupe, walivalishwa kitani nzuri, nyeupe na safi.
And the armies in heaven, clothed in fine linen, white, clean, followed Him on white horses.
15 Kinywani mwake hutoka upanga mkali ambao huyaangamiza mataifa, naye atawatawala kwa fimbo ya chuma. Naye hukanyaga vyombo vya mvinyo kwa hasira kali ya Mungu, hutawala juu ya wote.
And out of His mouth goes a sharp, two-edged sword, so that with it He may strike the nations. And He Himself will shepherd them with a rod of iron. And He Himself treads the winepress of the fury of the wrath of God, the Almighty.
16 Naye ameandikwa juu ya vazi lake na katika paja lake jina, MFALME WA WAFALME NA BWANA WA MABWANA.
And He has a name written on His robe and on His thigh, King of kings and Lord of lords!
17 Niliona malaika amesimama katika jua. Aliwaita kwa sauti kuu ndege wote warukao juu, “Njoni, kusanyikeni pamoja kwenye chakula kikuu cha Mungu.
And I saw an angel standing in the sun; and he cried out with a loud voice, saying to all the birds that fly in midheaven, “Come, gather together to the great dinner of God,
18 Njoni mle nyama ya wafalme, nyama ya majemedari, nyama ya watu wakubwa, nyama ya farasi na wapanda farasi, na nyama ya watu wote, walio huru na watumwa, wasio na umuhimu na wenye nguvu.”
so that you may eat flesh of kings and flesh of commanders and flesh of the mighty and flesh of horses along with their riders, even the flesh of all, both free and slave, both small and great.”
19 Nilimwona mnyama na wafalme wa nchi pamoja na majeshi yao. Walikuwa wamejipanga kwa ajili ya kufanya vita na mmoja aliyepanda farasi na jeshi lake.
And I saw the Beast and the kings of the earth and their armies gathered together to make war against the One riding the horse and against His army.
20 Mnyama alikamatwa na nabii wake wa uongo aliyezifanya ishara katika uwepo wake. Kwa ishara hizi aliwadanganya wale walioipokea chapa ya mnyama na walioisujudia sanamu yake. Wote wawili walitupwa wangali hai katika ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti. (Limnē Pyr )
So the Beast was captured, and with him the False prophet, the one who performed signs in his presence (by which he had deceived those who had received the mark of the Beast and those who worshiped his image). The two were thrown alive into the Lake of Fire that burns with brimstone. (Limnē Pyr )
21 Wale waliobaki waliuawa kwa upanga uliotoka kinywani mwa mmoja aliyepanda juu ya farasi. Ndege wote walikula mizoga ya miili yao.
And the rest were killed by the sword that proceeds from the mouth of the One riding the horse. And all the birds were filled with their flesh.