< Zaburi 92 >

1 Ni jambo jema kumshukuru Yahwe na kuliimbia sifa jina lako, Uliye Juu,
Ein Psalmlied auf den Sabbattag. Das ist ein köstlich Ding, dem HERRN danken, und lobsingen deinem Namen, du Höchster,
2 kutangaza uaminifu wa agano lako wakati wa asubuhi na uaminifu wako kila usiku,
des Morgens deine Gnade und des Nachts deine Wahrheit verkündigen
3 kwa kinubi cha nyuzi kumi na kwa tuni ya kinubi.
auf den zehn Saiten und Psalter, mit Spielen auf der Harfe.
4 Kwa kuwa wewe, Yahwe, matendo yako yamenifurahisha. Nitaimba kwa furaha kwa sababu ya matendo ya mikono yako.
Denn, HERR, du lässest mich fröhlich singen von deinen Werken, und ich rühme die Geschäfte deiner Hände.
5 Ni jinsi gani matendo yako ni makuu, Yahwe! mawazo yako ni ya kina.
HERR, wie sind deine Werke so groß! Deine Gedanken sind so sehr tief.
6 Mtu mpumbavu hawezi kuyajua, wala mjinga kuyaelewa haya:
Ein Törichter glaubt das nicht, und ein Narr achtet solches nicht.
7 Wasio haki watakapochipuka kama nyasi, na hata watendao uovu watakapo stawi, bado wataangamizwa kwenye uharibifu wa milele.
Die Gottlosen grünen wie das Gras, und die Übeltäter blühen alle, bis sie vertilgt werden immer und ewiglich.
8 Lakini wewe, Yahwe, utatawala milele.
Aber du, HERR, bist der Höchste und bleibst ewiglich.
9 Hakika, watazame adui zako, Yahwe! Hakika, watazame adui zako. Wataangamia! Wale wote watendao maovu watatawanywa.
Denn siehe, deine Feinde, HERR, deine Feinde werden umkommen; und alle Übeltäter müssen zerstreut werden.
10 Wewe umeyainua mapembe yangu kama mapembe ya Nyati wa porini; nimepakwa mafuta safi.
Aber mein Horn wird erhöht werden wie eines Einhorns, und ich werde gesalbt mit frischem Öl.
11 Macho yangu yameona kuanguka kwa adui zangu; masikio yangu yamesikia maangamizi ya maadui zangu waovu.
Und mein Auge wird seine Lust sehen an meinen Feinden; und mein Ohr wird seine Lust hören an den Boshaften, die sich wider mich setzen.
12 Wenye haki watastawi kama mtende; watakua kama mwerezi wa Lebanoni.
Der Gerechte wird grünen wie ein Palmbaum; er wird wachsen wie eine Zeder auf dem Libanon.
13 Wamepandwa katika nyumba ya Yahwe; wakistawi katika nyua za Mungu wetu.
Die gepflanzt sind in dem Hause des HERRN, werden in den Vorhöfen unsers Gottes grünen.
14 Wao huzaa matunda hata uzeeni; hukaa safi na wenye afya,
Und wenn sie gleich alt werden, werden sie dennoch blühen, fruchtbar und frisch sein,
15 kutangaza kuwa Yahwe ni wa haki. Yeye ni mwamba wangu, na hakuna udhalimu ndani yake.
daß sie verkündigen, daß der HERR so fromm ist, mein Hort, und ist kein Unrecht an ihm.

< Zaburi 92 >