< Zaburi 8 >

1 Yahweh Bwana wetu, ni jinsi gani jina lako ni tukufu katika dunia yote, wewe ufunuaye utukufu wako juu mbinguni.
Au maître-chantre. — Sur la Guittith. — Psaume de David. Éternel, notre Seigneur, Que ton nom est magnifique sur toute la terre! Ta majesté s'élève au-dessus des cieux.
2 Kutoka katika midomo ya watoto na vichanga umeumba sifa kwa sababu ya utukufu wako, ili kuwanyamazisha maadui wote na walipa kisasi wote.
De la bouche des petits enfants, Même de ceux qu'on allaite, Tu tires ta louange pour confondre tes adversaires, Pour réduire au silence l'ennemi et le rebelle.
3 Ninapozitazama mbingu, ambazo vidole vyako vimeumba, mwezi na nyota, ambazo umeziweka kila mmoja katika nafasi yake,
Quand je contemple les cieux, oeuvre de tes mains, La lune et les étoiles que tu y as placées,
4 Binadamu ni nani hata umtazame, na watu hata uwajali wao?
Je dis: Qu'est-ce que l'homme, pour que tu te souviennes de lui? Et le fils de l'homme, pour que tu prennes garde à lui?
5 Umewaumba chini kidogo kuliko viumbe vya mbinguni na umewazunguka na utukufu na heshima.
Tu l'as créé à peine inférieur à un dieu! Tu l'as couronné de gloire et de magnificence.
6 Umemfanya binadamu kutawala kazi ya mikono yako; umeviweka vitu vyote chini ya miguu yake:
Tu lui as donné l'empire sur les oeuvres de tes mains; Tu as mis toutes choses sous ses pieds:
7 kondoo na ng'ombe wote, na hata wanyama wa porini,
Les brebis comme les boeufs, Et même les bêtes sauvages,
8 ndege wa angani, na samaki wa baharini, na vyote vipitavyo katika mikondo ya bahari.
Les oiseaux du ciel et les poissons de l'océan, Tout ce qui parcourt les sentiers des mers.
9 Yahweh Bwana wetu, ni jinsi gani jina lako ni tukufu katika dunia yote!
Éternel, notre Seigneur, Que ton nom est magnifique sur toute la terre!

< Zaburi 8 >