< Zaburi 78 >
1 Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
Ein Lehrgedicht, von Asaph. - Mein Volk! Hab acht auf meine Lehre! Zu meines Mundes Reden neiget euer Ohr!
2 Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
Ich öffne meinen Mund zu einem Spruch. Ich künd Gesänge aus der Vorzeit Tagen,
3 Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
die wir vernommen und jetzt wissen, die unsre Väter uns erzählt.
4 Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
Wir, ihre Kinder, wollen über sie nicht schweigen. Wir wollen künftigem Geschlecht des Herren Ruhmestaten künden und seine Macht und Wunder, die er tat.
5 Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
Zum Brauch hat er's in Jakob eingesetzt, zur heiligen Pflicht in Israel gemacht. Denn unsern Vätern hat er anbefohlen, sie ihren Kindern kundzutun,
6 Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
auf daß ein späteres Geschlecht sie kenne, die Enkel, die geboren würden, sie ihren Kindern wiederum verkünden.
7 Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
Sie sollten Gott vertrauen und nicht vergessen Gottes Taten und seine Vorschriften befolgen
8 Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
und nicht, wie ihre Väter, werden ein widerspenstig, trotziges Geschlecht, solch ein Geschlecht von wankendem Gemüt und ungetreuem Herzen gegen Gott.
9 Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
Ganz unvernünftige Söhne, voller Trug, das Leben werfen sie hinweg und wenden sich am Trübsalstage ab;
10 Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
sie halten Gottes Bündnis nicht und wollen nicht nach seiner Lehre wandeln.
11 Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
Und sie vergessen seine Werke gänzlich und seine Wunder, die er ihnen zeigt.
12 Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
Vor ihren Vätern tat er Unvergleichliches, im Land Ägypten, im Gefild von Tanis.
13 Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
Er spaltete das Meer und führte sie hindurch und ließ das Wasser dammgleich stehen.
14 Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
Er leitete bei Tag sie mit der Wolke, die ganze Nacht mit Feuerschein,
15 Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
und ließ die Felsen in der Wüste sprudeln und tränkte sie in Fülle wie mit Fluten.
16 Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
Aus Steinen ließ er Bäche quellen, wie Ströme Wasser sprudeln.
17 Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
Allein sie sündigten noch weiter gegen ihn und widersetzten sich dem Höchsten in der Wüste.
18 Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
Und sie versuchten Gott in ihrem Herzen, für ihre Gelüste Speise heischend.
19 Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
Sie sprachen gegen Gott und fragten: "Vermag es Gott, selbst in der Wüste einen Tisch zu decken?
20 Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
Den Felsen schlug er zwar; das Wasser floß, die Bäche strömten. Vermag er aber Brot zu geben und seinem Volke Fleisch zu spenden?"
21 Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
Der Herr vernahm's und wurde zornig; ein Feuer loderte in Jakob auf; ein Zorn erhob sich gegen Israel,
22 kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
weil sie an Gott nicht glaubten und nicht auf seine Hilfe bauten.
23 Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
Doch er gebot den Wolken oben und tat des Himmels Pforten auf,
24 Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
hernieder ließ er Manna auf sie regnen, um sie zu speisen, schenkte ihnen Himmelsbrot.
25 Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
Das Brot der Engel konnte jeder essen; er sandte ihnen Kost in Fülle.
26 Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
Er ließ den Morgenwind am Himmel wehen; den Südwind führte er durch seine Macht herbei.
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
Dann ließ er Fleisch wie Staub auf sie herniederregnen, wie Meeressand Geflügel.
28 Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
Er ließ es in ihr Lager fallen, um seine Wohnstatt ringsumher.
29 Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
Sie aßen, wurden übersatt; was sie gewünscht, verlieh er ihnen.
30 Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
Noch war nicht ihre Lust gestillt, noch war die Kost in ihrem Munde,
31 Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
als Gottes Zorn sich gegen sie erhob, die Feisten unter ihnen würgte, die junge Mannschaft Israels zu Boden streckte.
32 Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
Bei all dem sündigten sie weiter und glaubten nicht an seine Wunderkräfte.
33 Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
Da ließ er ihre Tage zwecklos schwinden und ihre Jahre in Enttäuschung.
34 Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
Zwar fragten sie nach ihm, wenn er sie würgte, verlangten wiederum nach Gott,
35 Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
wohl eingedenk, daß Gott ihr Hort, der höchste Gott ihr Retter sei.
36 Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
Allein sie täuschten ihn mit ihrem Munde, belogen ihn mit ihrer Zunge.
37 Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
Ihr Herz war unaufrichtig gegen ihn; mit seinem Bunde meinten sie's nicht ehrlich.
38 Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
Doch er, erbarmungsvoll, vergab die Schuld, vertilgte nicht; oft hielt er seinen Zorn zurück und ließ nicht seinen Grimm austoben,
39 Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
wohl eingedenk, daß sie nur Fleisch, ein Windhauch, der verschwindet ohne Wiederkehr.
40 Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
Wie oft erzürnten sie ihn in der Wüste und reizten ihn im Steppenland,
41 Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
versuchten immer wieder Gott, erbitterten die Heiligen Israels,
42 Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
gedachten nimmer seiner Macht, des Tages, da er vor dem Feinde sie gerettet,
43 alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
wie er vor den Ägyptern seine Zeichen tat, an dem Gefild von Tanis seine Wunder:
44 Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
In Blut verwandelte er ihre Ströme; untrinkbar ward ihr fließend Wasser.
45 Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
Er sandte Ungeziefer unter sie, das sie verzehrte, und Frösche ihnen zum Verderben.
46 Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
Der Raupe gab er ihre Früchte preis und ihre Arbeit der Heuschrecke.
47 Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
Er schlug mit Hagel ihren Weinstock und ihren Maulbeerbaum durch Reif.
48 Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
Er gab ihr Vieh dem Hagel preis, den Blitzen ihre Herden.
49 Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
Er ließ die Hitze seines Zornes auf sie los, nur Grimm und Wut und Angst, von Unglücksboten eine Schar.
50 Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
So ließ er seinem Zorne freien Lauf, verschonte ihre Seele mit dem Tode nicht. Er gab der Pest ihr Leben preis,
51 Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
und in Ägypten schlug er alle Erstgeburt, die Jugendblüte in den Zelten Chams.
52 Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
Er führte, Schäflein gleich, sein Volk heraus und lenkte sie wie in der Steppe eine Herde.
53 Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
Er leitete sie sicher, daß sie nichts zu fürchten hatten; das Meer bedeckte ihre Feinde.
54 Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
Er brachte sie zu seinem heiligen Gebiete, zu jenem Berg, den seine Rechte sich erworben,
55 Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
vertrieb vor ihnen weg die Heiden, verloste sie als erblichen Besitz und ließ die Stämme Israels in ihren Zelten wohnen.
56 Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
Und doch versuchten sie und reizten Gott, den Höchsten, und hielten nimmer seine Satzungen.
57 Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
Wie ihre Väter wichen sie und fielen ab; sie wurden wie ein schlaffer Bogen.
58 Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
Sie reizten ihn zum Zorn durch ihre Höhen, zur Eifersucht durch ihre Götzenbilder.
59 Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
Gott hörte dies und wurde zornig, und Israel verwarf er völlig,
60 Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
verließ zu Silo seinen Sitz, das Zelt, in dein er unter Menschen wohnte;
61 Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
gab seine Ehre in Gefangenschaft und seine Zier in Feindeshand
62 Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
und gab sein Volk dem Schwerte preis, entrüstet über dies sein Eigentum.
63 Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
Die jungen Männer fraß das Feuer, und seine Jungfraun durften keine Totenklage halten.
64 Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
Hinfielen seine Priester durch das Schwert, und seine Witwen weinten nicht dazu.
65 Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
Doch wie vom Schlaf erwachte da der Herr, gleichwie ein Held vom Weine jauchzend.
66 Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
Im Rücken schlug er seine Feinde, belegte sie mit ewigem Schimpf.
67 Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
Doch er verschmähte Josephs Zelt; den Stamm von Ephraim erkor er nicht.
68 Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
Vielmehr erkor er Judas Stamm, den Sionsberg, der ihm so lieb.
69 Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
Er baute Himmelshöhen gleich sein Heiligtum und gleich der Erde, die er ewig gründete.
70 Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
Und er erkor sich David, seinen Knecht, entriß ihn seiner Herde Hürden.
71 Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
Vom Milchvieh nahm er ihn hinweg, sein Volk zu weiden in Jakob, in Israel die ewig Seinen.
72 Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.
Mit frommem Sinne weidete er sie und führte sie mit kluger Hand.