< Zaburi 78 >
1 Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
Intelligence d’Asaph.
2 Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
J’ouvrirai ma bouche en paraboles: je dirai des choses cachées dès le commencement;
3 Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
Combien de grandes choses nous avons entendu et connues, et que nos pères nous ont racontées.
4 Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
Elles n’ont pas été cachées à leurs fils dans une autre génération. Ils ont raconté les louanges du Seigneur, ses œuvres puissantes, et ses merveilles qu’il a faites;
5 Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
Et a suscité un témoignage dans Jacob; et a établi une loi dans Israël: Combien de grandes choses il a commandé à nos pères de faire connaître à leurs fils,
6 Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
Afin qu’une autre génération les connaisse. Les fils qui naîtront et s’élèveront après eux les raconteront à leurs fils,
7 Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
Afin qu’ils mettent en Dieu leur espérance, qu’ils n’oublient pas ses œuvres, et qu’ils recherchent ses commandements.
8 Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
De peur qu’ils ne deviennent comme leurs pères une génération perverse et exaspérant Dieu; Une génération qui n’a point dirigé son cœur, et dont l’esprit ne s’est point confié en Dieu.
9 Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
Les fils d’Ephraïm, habiles à tendre l’arc et à en tirer, ont tourné le dos au jour du combat.
10 Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
Ils n’ont pas gardé l’alliance de Dieu, et ils n’ont pas voulu marcher dans sa loi.
11 Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
Ils ont oublié ses bienfaits et les merveilles qu’il leur a montrées.
12 Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
Devant leurs pères il a fait des merveilles, dans la terre d’Égypte, dans la plaine de Tanis.
13 Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
Il divisa la mer, et il les fit passer: et il fixa les eaux comme dans une outre.
14 Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
Il les conduisit, le jour, au moyen d’une nuée, et toute la nuit à la clarté d’un feu.
15 Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
Il fendit une pierre dans le désert, et les fit boire comme à un abîme abondant.
16 Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
Car il fit sortir de l’eau de la pierre, et il en fit sortir des eaux comme des fleuves.
17 Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
Mais ils péchèrent encore de nouveau contre lui, ils excitèrent à la colère le Très-Haut dans un lieu sans eau.
18 Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
Et ils tentèrent Dieu dans leurs cœurs, au point qu’ils demandèrent une nourriture pour leurs âmes.
19 Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
Et ils parlèrent mal de Dieu, ils dirent: Est-ce que Dieu pourra préparer une table dans le désert?
20 Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
Parce qu’il a frappé une pierre, et que des eaux ont coulé; et que des torrents ont débordé. Est-ce qu’il pourra aussi donner du pain et préparer une table pour son peuple?
21 Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
C’est pour cela que le Seigneur entendit et différa; mais un feu s’alluma contre Jacob, et sa colère monta contre Israël;
22 kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
Parce qu’ils ne crurent pas en Dieu, et qu’ils n’espérèrent pas en son salut;
23 Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
Et il commanda aux nuées d’en haut, et il ouvrit les portes du ciel.
24 Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
Et il leur fit pleuvoir de la manne pour manger, et il leur donna du pain du ciel.
25 Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
L’homme mangea le pain des anges, Dieu leur envoya une nourriture en abondance.
26 Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
Il fit disparaître du ciel le vent du midi, et il amena par sa puissance le vent d’Afrique.
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
Il fit pleuvoir sur eux des viandes comme la poussière, et des oiseaux comme le sable de la mer.
28 Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
Et ils tombèrent au milieu de leur camp, autour de leurs tabernacles.
29 Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
Ils mangèrent et ils furent rassasiés à l’excès, et Dieu leur accorda selon leur désir;
30 Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
Ils ne furent point frustrés dans leur désir. Leurs viandes étaient encore dans leur bouche,
31 Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
Quand la colère de Dieu tomba sur eux. Et il tua les gras d’entre eux, et rejeta l’élite d’Israël.
32 Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
Au milieu de tous ces prodiges ils péchèrent encore, et ne crurent pas à ses merveilles.
33 Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
Et leurs jours se terminèrent vainement, et leurs années avec rapidité.
34 Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
Lorsqu’il les tuait, ils le cherchaient, et ils revenaient, et, dès le point du jour, ils venaient à lui.
35 Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
Et ils se souvinrent que Dieu était leur aide, et que le Dieu très haut était leur rédempteur.
36 Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
Mais ils l’aimèrent de bouche seulement, et ils lui mentirent par leur langue;
37 Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
Car leur cœur n’était pas droit avec lui, et ils ne furent pas trouvés fidèles à son alliance.
38 Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
Mais lui est miséricordieux, il pardonnera leurs péchés, et ne les perdra pas entièrement. Et souvent il détourna sa colère, et il n’alluma pas toute sa colère.
39 Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
Il se rappela qu’ils étaient chair, un souffle qui va et qui ne revient pas.
40 Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
Combien de fois l’ont-ils irrité dans le désert, et l’ont-ils excité à la colère dans un lieu sans eau?
41 Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
Et de nouveau ils tentèrent Dieu, et ils ont aigri le saint d’Israël.
42 Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
Ils ne se sont pas rappelé sa main, au jour où il les retira de la main d’un oppresseur,
43 alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
Comment il fit en Égypte ses miracles, et ses prodiges dans la plaine de Tanis.
44 Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
Et il changea en sang leurs fleuves et leurs pluies, pour qu’ils ne bussent point.
45 Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
Il envoya contre eux une multitude de mouches qui les dévorèrent, et la grenouille qui les ravagea.
46 Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
Et il donna à la rouille leurs fruits, et leurs travaux à la sauterelle.
47 Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
Et il fit périr par la grêle leurs vignes, et leurs mûriers par la gelée.
48 Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
Et il livra à la grêle leurs bêtes, et leurs possessions au feu.
49 Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
Il envoya contre eux la colère de son indignation: l’indignation, et la colère, et la tribulation envoyées par des anges mauvais.
50 Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
Il fit une voie au sentier de sa colère, et il n’épargna pas la mort à leurs âmes; et leurs bêtes, il les renferma dans la mort.
51 Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
Et il frappa tout premier-né d’Égypte, les prémices de tout travail dans les tabernacles de Cham.
52 Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
Et il en retira, comme des brebis, son peuple; et il les conduisit comme un troupeau dans le désert.
53 Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
Et il les fit sortir pleins d’espérance, et ils ne craignirent point; quant à leurs ennemis, la mer les couvrit.
54 Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
Et il les amena sur la montagne de sa sanctification; montagne qu’a acquise sa droite. Et il chassa de leur face des nations; et il leur divisa au sort une terre avec un cordeau de partage.
55 Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
Et il fit habiter dans leurs tabernacles les tribus d’Israël.
56 Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
Mais ils tentèrent et aigrirent le Dieu très haut; et ne gardèrent pas ses témoignages.
57 Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
Et ils se détournèrent de lui et n’observèrent pas l’alliance; de la même manière que leurs pères, ils devinrent comme un arc qui porte à faux.
58 Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
Ils l’ont excité à la colère sur leurs collines; et par leurs images taillées au ciseau, ils l’ont provoqué à la jalousie.
59 Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
Dieu entendit, et il méprisa, et il réduisit entièrement au néant Israël.
60 Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
Et il repoussa le tabernacle de Silo, son tabernacle où il avait habité parmi les hommes.
61 Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
Il livra à la captivité l’arche, leur force; et leur beauté entre les mains de l’ennemi.
62 Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
Il renferma son peuple entre les glaives; et son héritage, il le méprisa.
63 Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
Un feu dévora leurs jeunes hommes; et leurs vierges ne furent pas pleurées.
64 Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
Leurs prêtres tombèrent sous le glaive, et on ne pleurait pas leurs veuves.
65 Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
Mais le Seigneur se réveilla comme un homme endormi, comme un héros qui a été ivre de vin.
66 Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
Il frappa ses ennemis par derrière; il leur infligea un opprobre éternel.
67 Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
Et il repoussa le tabernacle de Joseph, et ne choisit point la tribu d’Éphraïm;
68 Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
Mais il choisit la tribu de Juda, la montagne de Sion qu’il a aimée.
69 Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
Et il bâtit comme une corne de licornes son sanctuaire, dans la terre qu’il a fondée pour les siècles.
70 Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
Il choisit David son serviteur, et il le tira du milieu des troupeaux de brebis: il le prit à la suite de celles qui étaient pleines,
71 Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
Pour être le pasteur de Jacob son serviteur, et d’Israël son héritage.
72 Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.
Et David les fit paître dans l’innocence de son cœur, et avec ses mains habiles, il les conduisit.