< Zaburi 73 >

1 Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale walio na moyo safi.
[Ein Psalm; von Asaph.] Fürwahr, Gott ist Israel gut, denen, die reinen Herzens sind.
2 Lakini kwangu mimi, kidogo tu miguu yangu iteleze; miguu yangu karibu iteleze kutoka kwangu
Ich aber-wenig fehlte, so wären meine Füße abgewichen, um nichts wären ausgeglitten meine Schritte.
3 kwa sababu niliwaonea wivu wenye kiburi nilipoona mafanikio ya waovu.
Denn ich beneidete die Übermütigen, als ich sah die Wohlfahrt der Gesetzlosen.
4 Kwa maana hawana maumivu hadi kufa kwao, lakini wana nguvu na wameshiba.
Denn keine Qualen haben sie bei ihrem Tode, und [Wahrsch. ist zu lesen: Denn keine Qualen haben sie, vollkräftig usw.] wohlgenährt ist ihr Leib.
5 Wako huru dhidi ya mizigo ya watu wengine; nao hawateswi kama watu wengine.
Nicht sind sie im Ungemach der Sterblichen, und mit den Menschen werden sie nicht geplagt.
6 Kiburi kinawapamba kama mkufu kwenye shingo zao; jeuri huwavika kama vazi.
Deshalb umgibt sie der Hochmut wie ein Halsgeschmeide, Gewalttat umhüllt sie wie ein Gewand.
7 Katika upofu wa jinsi hii dhambi huja; mawazo maovu hupita mioyoni mwao.
Es tritt aus dem Fett hervor ihr Auge; sie wallen über in den Einbildungen des Herzens.
8 Wao hudhihaki na kuongea kwa namna ya uovu; kwa kiburi chao hutishia mateso.
Sie höhnen und reden in Bosheit von Bedrückung; von oben herab reden sie.
9 Wameweka vinywa vyao dhidi ya mbingu, na ndimi zao hutanga tanga duniani.
Sie setzen in den Himmel ihren Mund, und ihre Zunge wandelt auf der Erde.
10 Kwa hiyo watu wake huwageukia na maji yaliyojaa hukaushwa.
Deshalb wendet sich hierher sein Volk, und Wasser in Fülle wird von ihnen geschlürft. [O. für sie ausgepreßt]
11 Nao husema, “Mungu anajuaje? Yako maarifa kwake yeye aliye juu?”
Und sie sprechen: Wie wüßte es Gott, [El] und wie sollte Wissen sein bei dem Höchsten?
12 Fahamu: watu hawa ni waovu; mara zote hawajali, wakifanyika matajiri na matajiri.
Siehe, diese sind Gesetzlose, und, immerdar sorglos, [O. sicher ruhig] erwerben sie sich Vermögen.
13 Hakika nimeutunza moyo wangu bure na nimenawa mikono yangu pasipo kukosa.
Fürwahr, vergebens habe ich mein Herz gereinigt, und in Unschuld gewaschen meine Hände.
14 Maana mchana kutwa nimeteswa na kuadhibiwa kila asubuhi.
Da ich ja geplagt ward den ganzen Tag, und alle Morgen meine Züchtigung da war.
15 Kama ningesema, “Ningesema mambo haya,” kumbe nigewasaliti kizazi hiki cha watoto wenu.
Wenn ich gesagt hätte: Ich will ebenso reden, siehe, so wäre ich treulos gewesen dem Geschlecht deiner Söhne.
16 Ingawa nilijaribu kuyaelewa mambo haya, yalikuwa ni magumu sana kwangu.
Da dachte ich nach, um dieses zu begreifen: eine mühevolle Arbeit war es in meinen Augen;
17 Ndipo nilipoingia patakatifu pa Mungu na kuelewa hatma yao.
bis ich hineinging in die Heiligtümer Gottes [El] und jener Ende gewahrte.
18 Hakika wewe huwaweka penye utelezi; huwaangusha mpaka palipoharibika.
Fürwahr, auf schlüpfrige Örter setzest du sie, stürzest sie hin zu Trümmern.
19 Jinsi gani wamekuwa ukiwa kwa muda mfupi! Wamefika mwisho nao wamemaliza kwa utisho.
Wie sind sie so plötzlich verwüstet, haben ein Ende genommen, sind umgekommen durch Schrecknisse!
20 Wao ni kama ndoto wakati wa mtu kuamka; Bwana, utakapo inuka, utazidharau ndoto zao.
Wie einen Traum nach dem Erwachen wirst du, Herr, beim Aufwachen ihr Bild verachten.
21 Maana moyo wangu ulipata uchungu, nami nilijeruhiwa sana.
Als mein Herz sich erbitterte und es mich in meinen Nieren stach,
22 Nilikuwa mjinga na sijui neno; nilikuwa kama mnyama tu mbele yako.
Da war ich dumm und wußte nichts; ein Tier [Eig. Vieh] war ich bei dir.
23 Lakini mimi nipo pamoja nawe daima; umenishika mkono wa kuume.
Doch ich bin stets bei dir: du hast mich erfaßt bei meiner rechten Hand;
24 Utaniongoza kwa shauri lako na baadaye utanipokea katika utukufu.
durch deinen Rat wirst du mich leiten, und nach der Herrlichkeit [O. und nachher, in Herrlichkeit] wirst du mich aufnehmen.
25 Ni nani niliye naye mbinguni isipokuwa wewe? Hakuna nimtamaniye duniani isipokuwa wewe.
Wen habe ich im Himmel? und neben dir habe ich an nichts Lust auf der Erde.
26 Mwili wangu na moyo wangu huwa dhaifu, bali Mungu ndiye nguvu ya moyo wangu daima.
Vergeht mein Fleisch und mein Herz-meines Herzens Fels und mein Teil ist Gott auf ewig.
27 Wale walio mbali nawe wataangamia; utawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
Denn siehe, es werden umkommen, die dir ferne sind; du vertilgst alle, die buhlerisch von dir abweichen.
28 Lakini mimi, linipasalo kufanya ni kumkaribia Mungu. Nimemfanya Bwana Yahwe kimbilio langu. Nami nitayatangaza matendo yako yote.
Ich aber, Gott zu nahen ist mir gut; ich habe meine Zuversicht auf den Herrn, Jehova, gesetzt, um zu erzählen alle deine Taten.

< Zaburi 73 >