< Zaburi 73 >

1 Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale walio na moyo safi.
Surely God is good to Israel [God prevails], to those who are pure in heart.
2 Lakini kwangu mimi, kidogo tu miguu yangu iteleze; miguu yangu karibu iteleze kutoka kwangu
But as for me, my feet were almost gone. My steps had nearly slipped.
3 kwa sababu niliwaonea wivu wenye kiburi nilipoona mafanikio ya waovu.
For I was envious of the arrogant, when I saw the prosperity of the wicked.
4 Kwa maana hawana maumivu hadi kufa kwao, lakini wana nguvu na wameshiba.
For there are no struggles in their death, but their strength is firm.
5 Wako huru dhidi ya mizigo ya watu wengine; nao hawateswi kama watu wengine.
They are free from burdens of men, neither are they plagued like other men.
6 Kiburi kinawapamba kama mkufu kwenye shingo zao; jeuri huwavika kama vazi.
Therefore pride is like a chain around their neck. Violence covers them like a garment.
7 Katika upofu wa jinsi hii dhambi huja; mawazo maovu hupita mioyoni mwao.
Their eyes bulge with fat. Their minds pass the limits of conceit.
8 Wao hudhihaki na kuongea kwa namna ya uovu; kwa kiburi chao hutishia mateso.
They scoff and speak with malice. In arrogance, they threaten oppression.
9 Wameweka vinywa vyao dhidi ya mbingu, na ndimi zao hutanga tanga duniani.
They have set their mouth in the heavens. Their tongue walks through the earth.
10 Kwa hiyo watu wake huwageukia na maji yaliyojaa hukaushwa.
Therefore their people teshuvah ·completely return· to them, and they drink up waters of abundance.
11 Nao husema, “Mungu anajuaje? Yako maarifa kwake yeye aliye juu?”
They say, “How does God know? Is there knowledge in haElyon [the Most High]?”
12 Fahamu: watu hawa ni waovu; mara zote hawajali, wakifanyika matajiri na matajiri.
Behold, these are the wicked. Being always at ease, they increase in riches.
13 Hakika nimeutunza moyo wangu bure na nimenawa mikono yangu pasipo kukosa.
Surely in vain I have cleansed my heart, and washed my hands in innocence,
14 Maana mchana kutwa nimeteswa na kuadhibiwa kila asubuhi.
For all day long have I been plagued, and punished every morning.
15 Kama ningesema, “Ningesema mambo haya,” kumbe nigewasaliti kizazi hiki cha watoto wenu.
If I had said, “I will speak thus;” behold, I would have betrayed the generation of your children.
16 Ingawa nilijaribu kuyaelewa mambo haya, yalikuwa ni magumu sana kwangu.
When I tried to understand this, it was too painful for me;
17 Ndipo nilipoingia patakatifu pa Mungu na kuelewa hatma yao.
Until I entered God’s sanctuary, and considered their latter end.
18 Hakika wewe huwaweka penye utelezi; huwaangusha mpaka palipoharibika.
Surely you set them in slippery places. You throw them down to destruction.
19 Jinsi gani wamekuwa ukiwa kwa muda mfupi! Wamefika mwisho nao wamemaliza kwa utisho.
How they are suddenly destroyed! They are completely swept away with terrors.
20 Wao ni kama ndoto wakati wa mtu kuamka; Bwana, utakapo inuka, utazidharau ndoto zao.
As a dream when one wakes up, so, Lord, when you awake, you will despise their fantasies.
21 Maana moyo wangu ulipata uchungu, nami nilijeruhiwa sana.
For my soul was grieved. I was embittered in my heart.
22 Nilikuwa mjinga na sijui neno; nilikuwa kama mnyama tu mbele yako.
I was so senseless and ignorant. I was a brute beast before you.
23 Lakini mimi nipo pamoja nawe daima; umenishika mkono wa kuume.
Nevertheless, I am continually with you. You have held my right hand.
24 Utaniongoza kwa shauri lako na baadaye utanipokea katika utukufu.
You will guide me with your counsel, and afterward receive me to kavod ·weighty glory·.
25 Ni nani niliye naye mbinguni isipokuwa wewe? Hakuna nimtamaniye duniani isipokuwa wewe.
Whom do I have in heaven? There is no one on earth whom I desire besides you.
26 Mwili wangu na moyo wangu huwa dhaifu, bali Mungu ndiye nguvu ya moyo wangu daima.
My flesh and my heart fails, but God is the strength of my heart and my portion forever.
27 Wale walio mbali nawe wataangamia; utawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
For, behold, those who are far from you shall perish. You have destroyed all those who are unfaithful to you.
28 Lakini mimi, linipasalo kufanya ni kumkaribia Mungu. Nimemfanya Bwana Yahwe kimbilio langu. Nami nitayatangaza matendo yako yote.
But it is good for me to come close to God. I have made the Lord Adonai my refuge, that I may tell of all your works.

< Zaburi 73 >