< Zaburi 63 >

1 Mungu, wewe ni Mungu wangu! Ninakutafuta wewe kwa bidii, moyo wangu unakiu yako, mwili wangu unakutamani sana wewe, katika ukame na nchi iliyochoka mahali ambapo hakuna maji.
A Psalme of David. When he was in the wildernesse of Judah. O God, thou art my God, earely will I seeke thee: my soule thirsteth for thee: my flesh longeth greatly after thee in a barren and drye land without water.
2 Hivyo nimekutafuta wewe katika watu watakatifu kuona nguvu zako na utukufu wako.
Thus I beholde thee as in the Sanctuarie, when I beholde thy power and thy glorie.
3 Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakusifu wewe.
For thy louing kindnesse is better then life: therefore my lippes shall prayse thee.
4 Hivyo nitakutukuza wewe niwapo hai; kwa jina lako nitainua mikono yangu juu.
Thus will I magnifie thee all my life, and lift vp mine hands in thy name.
5 Itakuwa kana kwamba nilikula mlo wa mafuta na wenye kunona, kwa midomo ya furaha kinywa changu kitakusifu wewe,
My soule shalbe satisfied, as with marowe and fatnesse, and my mouth shall praise thee with ioyfull lippes,
6 nikufikiripo kitandani mwangu na kukutafakari wewe wakati wa saa za usiku.
When I remember thee on my bedde, and when I thinke vpon thee in the night watches.
7 Kwa maana umekuwa msaada wangu, na katika uvuli wa mbawa zako ninafurahia.
Because thou hast bene mine helper, therefore vnder the shadow of thy wings wil I reioyce.
8 Ninashikamana nawe; mkono wako wa kuume unanisaidia.
My soule cleaueth vnto thee: for thy right hand vpholdeth me.
9 Lakini wale watafutao kuuharibu uhai wangu wataenda chini kwenye sehemu ya chini kabisa ya nchi;
Therefore they that seeke my soule to destroy it, they shall goe into the lowest partes of the earth.
10 watakabidhiwa kwa wale ambao mikono yao hutumia upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
They shall cast him downe with the edge of the sword, and they shall be a portion for foxes.
11 Bali mfalme atashangilia katika Mungu; yeyote anaye apa kupitia yeye atajivunia yeye, lakini vinywa ya wale wasemao uongo watanyamazishwa.
But the King shall reioyce in God, and all that sweare by him shall reioyce in him: for the mouth of them that speake lyes, shall be stopped.

< Zaburi 63 >