< Zaburi 48 >

1 Yahwe ndiye aliye mkuu na mwenyekusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu kwenye mlima wake mtakatifu.
En sång, en psalm av Koras söner. Stor är HERREN och högt lovad, i vår Guds stad, på sitt heliga berg.
2 Ni mzuri katika mwinuko wake, furaha ya nchi yote, ni mlima Sayuni, kwenye upande wa kaskazini, mji wa Mfalme mkuu.
Skönt höjer det sig, hela jordens fröjd, berget Sion längst uppe i norr, den store konungens stad.
3 Mungu amejifunua mwenyewe katika jumba lake la kifahari kama kimbilio la usalama.
Gud har i dess palatser gjort sig känd såsom ett värn.
4 Maana, tazama, wafalme walikusanyika wenyewe; wote pamoja walipita.
Ty se, konungarna församlade sig, tillhopa drogo de fram.
5 Nao waliuona, wakashangaa; walifadhaika, na wakaharakisha kuondoka.
De sågo det, då häpnade de; de förskräcktes, de flydde.
6 Pale pale tetemeko liliwashikilia, maumivu makali kama mwanamke anaye zaa.
Bävan grep dem där, ångest lik en barnaföderskas.
7 Kwa upepo wa mashariki wewe huivunja meli ya Tarshishi.
Så krossar du Tarsis-skepp med östanvinden.
8 Kama tulivyo sikia, vivyo hivyo tumeona katika mji wa Yahwe wa majeshi, katika mji wa Mungu wetu; Mungu atautunza milele. (Selah)
Såsom vi hade hört, så fingo vi se det, i HERREN Sebaots stad, i vår Guds stad; Gud håller den vid makt till evig tid. (Sela)
9 Tumeutafakari uaminifu wa agano lako, Mungu, katikati ya hekalu lako.
Vi tänka, o Gud, på din nåd, när vi stå i ditt tempel.
10 Kama lilivyo jina lako, Mungu, hivyo ndivyo zilivyo sifa zako mpaka miisho ya dunia; mkono wako wa kuume umejaa haki.
Såsom ditt namn, o Gud, så når ock ditt lov intill jordens ändar; din högra hand är full av rättfärdighet.
11 Milma Sayuni na ufurahi, nao wana wa Yuda washangilie kwa sababu ya amri ya haki yako.
Sions berg glädje sig, Juda döttrar fröjde sig, för dina domars skull.
12 Tembeeni katika Mlima Sayuni, muuzungukie mji,
Gån omkring Sion och vandren runt därom, räknen dess torn;
13 mzitazame kwa makini nguzo zake, na mtazame majumba yake ya kifahari ili kwamba muweze kuwasimulia kizazi kijacho.
given akt på dess murar, skriden genom dess palatser, så att I kunnen förtälja därom för ett kommande släkte.
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; naye atakuwa kiongozi wetu mpaka kufa.
Ty sådan är Gud, vår Gud, alltid och evinnerligen; intill döden skall han ledsaga oss.

< Zaburi 48 >