< Zaburi 45 >
1 Moyo wangu unafurika kwa neno zuri; nitasoma kwa sauti maneno niliyo yaandika kuhusu mfalme; ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi mwenye ustadi.
Pour le chef musicien. Réglé sur « The Lilies ». Une contemplation par les fils de Korah. Un chant de mariage. Mon cœur déborde d'un thème noble. Je récite mes vers pour le roi. Ma langue est comme la plume d'un habile écrivain.
2 Wewe u mzuri sana kuliko mwanadamu yeyote; neema imemiminwa midomoni mwako; Kwa hiyo tunajua ya kuwa Mungu amekubariki milele.
Tu es le plus excellent des fils de l'homme. La grâce a oint vos lèvres, donc Dieu vous a béni pour toujours.
3 Weka upanga wako upande wako, wewe uliye mwenye nguvu, katika utukufu wako na enzi yako.
Attache ton épée à ta cuisse, ô puissant, dans ta splendeur et ta majesté.
4 Katika enzi yako enenda katika ushindi kwa sababu ya uaminifu, upole, na haki; mkono wako wa kuume utakufundisha mambo ya kutisha.
Dans ta majesté, monte victorieusement au nom de la vérité, de l'humilité et de la droiture. Laissez votre main droite afficher des actions impressionnantes.
5 Mishale yako ni mkali; watu huanguka chini yako; mishale yako imo ndani ya mioyo ya adui za mfalme.
Tes flèches sont acérées. Les nations tombent sous toi, avec des flèches dans le cœur des ennemis du roi.
6 Kiti chako cha enzi, Mungu ni cha milele na milele; na fimbo ya haki ni fimbo ya utawala wako.
Ton trône, Dieu, est éternel et permanent. Un sceptre d'équité est le sceptre de votre royaume.
7 Umeipenda haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekupaka mafuta ya furaha kuliko wenzako.
Tu as aimé la justice, et tu as haï la méchanceté. C'est pourquoi Dieu, ton Dieu, t'a oint d'une huile d'allégresse au-dessus de tes semblables.
8 Mavazi yako yote hunukia manemane, udi, na mdalasini; kukoka katika majumba ya pembe vyombo vya muziki wa nyuzi vimekufurahisha.
Tous tes vêtements sentent la myrrhe, l'aloès et la casse. Des palais d'ivoire, des instruments à cordes vous ont réjoui.
9 Binti za wafalme ni kati ya wake zako waheshimiwa; na mkono wako wa kuume amesimama malikia aliye vaa mavazi ya dhahabu ya Ofiri.
Les filles des rois sont parmi vos femmes d'honneur. A votre droite, la reine se tient en or d'Ophir.
10 Sikiliza, mwanangu, tafakari na utege sikio lako; uwasahahu watu wako na watu wa nyumba ya baba yako.
Écoute, ma fille, réfléchis, et prête l'oreille. Oublie ton propre peuple, et aussi la maison de ton père.
11 Hivyo mfalme atautamani uzuri wako; yeye ni Bwana wako; umstahi.
Ainsi le roi désirera ta beauté, honorez-le, car il est votre seigneur.
12 Binti wa Tiro atakuwepo akiwa na zawadi; matajiri kati wa watu watajipendekeza kwako.
La fille de Tyr vient avec un présent. Les riches parmi le peuple implorent votre faveur.
13 Binti mfalme katika jumba la kifahari ana utukufu wote; mavazi yake yametengenezwa kwa dhahabu.
La princesse à l'intérieur est toute glorieuse. Ses vêtements sont tissés d'or.
14 Naye ataongozwa kwa mfalme akiwa katika mavazi ya dhahabu; mabikra, wenzake wanoumfuata, wataletwa kwako mafalme.
Elle sera conduite au roi dans un ouvrage brodé. Les vierges, ses compagnes qui la suivent, te seront amenées.
15 Wao wataongozwa kwa furaha na shangwe; wataingia mahali pa mfalme.
Ils seront conduits avec joie et allégresse. Ils entreront dans le palais du roi.
16 Katika mahali pa baba zako watoto wako watakuwepo, ambao wewe utawafanya kuwa wakuu katika nchi yote.
Vos fils prendront la place de vos pères. Tu en feras des princes sur toute la terre.
17 Nami nitalifanya jina lako kukumbukwa katika uzao wote; kwa hiyo watu watakushukuru milele na milele.
Je ferai en sorte qu'on se souvienne de ton nom dans toutes les générations. C'est pourquoi les peuples te rendront grâce pour toujours et à jamais.