< Zaburi 44 >

1 Mungu, tumesikia kwa masikio yetu, baba zetu wametuambia kazi uliyofanya katika siku zao, siku za kale.
Kwa mwimbishaji. Utenzi wa wana wa Kora. Ee Mungu, tumesikia kwa masikio yetu, baba zetu wametueleza yale uliyotenda katika siku zao, siku za kale.
2 Uliwafukuza mataifa kwa mkono wako, lakini ukawafanya watu wetu kuishi humo; wewe uliwataabisha mataifa, lakini ukawaeneza watu wetu katika nchi.
Kwa mkono wako uliwafukuza mataifa na ukawapanda baba zetu, uliangamiza mataifa na kuwastawisha baba zetu.
3 Kwa maana hawakupata umiliki wa nchi kwa upanga wao, wala mkono wao wenyewe haukuwaokoa; bali mkono wako wakuume, mkono wako, na nuru ya uso wako, na kwa sababu uliwaridhia.
Sio kwa upanga wao waliipata nchi, wala si mkono wao uliwapatia ushindi; ilikuwa ni kitanga cha mkono wako wa kuume, na nuru ya uso wako, kwa kuwa uliwapenda.
4 Mungu, wewe ni Mfalme wangu, amuru ushindi kwa ajili ya Yakobo.
Wewe ni mfalme wangu na Mungu wangu, unayeamuru ushindi kwa Yakobo.
5 Kwa uweza wako tutawaangusha chini maadui zetu; kwa jina lako tutatembea juu yao, wale wanao inuka dhidi yetu.
Kwa uwezo wako tunawasukuma nyuma watesi wetu; kwa jina lako tunawakanyaga adui zetu.
6 Kwa maana sitauamini upinde wangu, wala upanga wangu hautaniokoa.
Siutumaini upinde wangu, upanga wangu hauniletei ushindi;
7 Bali wewe ndeye uliyetuokoa na adui zetu, na umewaaibisha wale watuchukiao.
bali wewe unatupa ushindi juu ya adui zetu, unawaaibisha watesi wetu.
8 Katika Mungu tumefanywa kujivuna siku zote, nasi tutalishukuru jina lako milele. (Selah)
Katika Mungu wetu tunajivuna mchana kutwa, nasi tutalisifu jina lako milele.
9 Lakini sasa umetutupa na kutufedhehesha, na hauendi na majeshi yetu.
Lakini sasa umetukataa na kutudhili, wala huendi tena na jeshi letu.
10 Umetufanya kuwakimbia maadui zetu; na wale watuchukiao huchukua vitu vyetu vya thamani kwa ajili yao wenyewe.
Umetufanya turudi nyuma mbele ya adui, nao watesi wetu wametuteka nyara.
11 Umetufanya kama kondoo aliyeandaliwa kwa ajili ya chakula na umetutawanya kati ya mataifa.
Umetuacha tutafunwe kama kondoo na umetutawanya katika mataifa.
12 Wewe unawauza watu wako bure; kwa kufanya hivyo haukupata faida.
Umewauza watu wako kwa fedha kidogo, wala hukupata faida yoyote kwa mauzo yao.
13 Wewe umetufanya kukemewa na majirani zetu, kuchekwa, na kudhihakiwa na wale wanao tuzunguka.
Umetufanya lawama kwa jirani zetu, dharau na dhihaka kwa wale wanaotuzunguka.
14 Umetufaya kituko kati ya mataifa, .......................................................
Umetufanya kuwa mithali miongoni mwa mataifa, mataifa hutikisa vichwa vyao.
15 Siku zote fedheha yangu iko mbele yangu, na aibu ya uso wangu imenifunika
Fedheha yangu iko mbele yangu mchana kutwa, na uso wangu umejaa aibu tele,
16 kwa sababu ya sauti yake iliyo kemea na kutukana, kwa sababu ya adui na kisasi.
kwa ajili ya dhihaka ya wale wanaonilaumu na kunitukana, kwa sababu ya adui, ambaye anatamani kulipiza kisasi.
17 Yote haya yametupata sisi; bado hatukukusahau wewe wala kulikosea agano lako.
Hayo yote yametutokea, ingawa tulikuwa hatujakusahau wala hatujaenda kinyume na agano lako.
18 Mioyo yetu haikukengeuka; hatua zetu hazikuiacha njia yako.
Mioyo yetu ilikuwa haijarudi nyuma; nyayo zetu zilikuwa hazijaiacha njia yako.
19 Bali wewe umetuadhibu vikali katika mahali pa mbweha na kutufunika na uvuli wa mauti.
Lakini ulituponda na kutufanya makao ya mbweha, na ukatufunika kwa giza nene.
20 Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kueneza mikono yetu kwa Mungu mgeni,
Kama tungalikuwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kunyooshea mikono yetu kwa mungu mgeni,
21 Mungu asingeligundua hili? Kwa maana yeye anazijua siri za moyo.
je, Mungu hangaligundua hili, kwa kuwa anazijua siri za moyo?
22 Hakika, kwa ajili ya jina lako tutauawa siku zote; tunahesabiwa kuwa kondoo kwa ajili ya kuchinjwa.
Hata hivyo kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa; tumehesabiwa kama kondoo wa kuchinjwa.
23 Bwana, amka, kwa nini unalala? Inuka, usitutupe moja kwa moja.
Amka, Ee Bwana! Kwa nini unalala? Zinduka! Usitukatae milele.
24 Kwa nini unaficha uso wako na kusahau mateso yetu na kukandamizwa kwetu?
Kwa nini unauficha uso wako na kusahau taabu na mateso yetu?
25 Kwa maana tumeyeyushwa kwenye mavumbi; miili yetu imeshikamana na ardhi.
Tumeshushwa hadi mavumbini, miili yetu imegandamana na ardhi.
26 Inuka utusaidie na utuokoe kwa ajili ya uaminifu wa agano lako.
Inuka na utusaidie, utukomboe kwa sababu ya upendo wako usio na mwisho.

< Zaburi 44 >