< Zaburi 44 >

1 Mungu, tumesikia kwa masikio yetu, baba zetu wametuambia kazi uliyofanya katika siku zao, siku za kale.
伶長にうたはしめたるコラの子のをしへの歌 ああ神よむかしわれらの列組の日になんぢがなしたまひし事迹をわれら耳にきけり 列組われらに語れり
2 Uliwafukuza mataifa kwa mkono wako, lakini ukawafanya watu wetu kuishi humo; wewe uliwataabisha mataifa, lakini ukawaeneza watu wetu katika nchi.
なんぢ手をもてもろもろの國人をおひしりぞけ われらの列組をうゑ並もろもろの民をなやましてわれらの列組をはびこらせたまひき
3 Kwa maana hawakupata umiliki wa nchi kwa upanga wao, wala mkono wao wenyewe haukuwaokoa; bali mkono wako wakuume, mkono wako, na nuru ya uso wako, na kwa sababu uliwaridhia.
かれらはおのが劍によりて國をえしにあらず おのが臂によりて勝をえしにあらず 只なんぢの右の手なんぢの臂なんぢの面のひかりによれり 汝かれらを恵みたまひたればなり
4 Mungu, wewe ni Mfalme wangu, amuru ushindi kwa ajili ya Yakobo.
神よなんぢはわが王なり ねがはくはヤコブのために救をほどこしたまへ
5 Kwa uweza wako tutawaangusha chini maadui zetu; kwa jina lako tutatembea juu yao, wale wanao inuka dhidi yetu.
われらは汝によりて敵をたふし また我儕にさからひて起りたつものをなんぢの名によりて踐壓ふべし
6 Kwa maana sitauamini upinde wangu, wala upanga wangu hautaniokoa.
そはわれわが弓によりたのまず わが劍もまた我をすくふことあたはざれぱなり
7 Bali wewe ndeye uliyetuokoa na adui zetu, na umewaaibisha wale watuchukiao.
なんぢわれらを敵よりすくひ またわれらを惡むものを辱かしめたまへり
8 Katika Mungu tumefanywa kujivuna siku zote, nasi tutalishukuru jina lako milele. (Selah)
われらはひねもす神によりてほこり われらは永遠になんぢの名に感謝せん (セラ)
9 Lakini sasa umetutupa na kutufedhehesha, na hauendi na majeshi yetu.
しかるに今はわれらをすてて恥をおはせたまへり われらの軍人とともに出ゆきたまはず
10 Umetufanya kuwakimbia maadui zetu; na wale watuchukiao huchukua vitu vyetu vya thamani kwa ajili yao wenyewe.
われらを敵のまへより退かしめたまへり われらを惡むものその任意にわれらを掠めうばへり
11 Umetufanya kama kondoo aliyeandaliwa kwa ajili ya chakula na umetutawanya kati ya mataifa.
なんぢわれらを食にそなへらるる羊のごとくにあたへ斯てわれらをもろもろの國人のなかにちらし
12 Wewe unawauza watu wako bure; kwa kufanya hivyo haukupata faida.
得るところなくしてなんぢの民をうり その價によりてなんぢの富をましたまはざりき
13 Wewe umetufanya kukemewa na majirani zetu, kuchekwa, na kudhihakiwa na wale wanao tuzunguka.
汝われらを隣人にそしらしめ われらを環るものにあなどらしめ 嘲けらしめたまへり
14 Umetufaya kituko kati ya mataifa, .......................................................
又もろもろの國のなかにわれらを談柄となし もろもろの民のなかにわれらを頭ふらるる者となしたまへり
15 Siku zote fedheha yangu iko mbele yangu, na aibu ya uso wangu imenifunika
わが凌辱ひねもす我がまへにあり わがかほの恥われをおほへり
16 kwa sababu ya sauti yake iliyo kemea na kutukana, kwa sababu ya adui na kisasi.
こは我をそしり我をののしるものの聲により我にあだし我にうらみを報るものの故によるなり
17 Yote haya yametupata sisi; bado hatukukusahau wewe wala kulikosea agano lako.
これらのこと皆われらに臨みきつれどわれらなほ汝をわすれず なんぢの契約をいつはりまもらざりき
18 Mioyo yetu haikukengeuka; hatua zetu hazikuiacha njia yako.
われらの心しりぞかずわれらの歩履なんぢの道をはなれず
19 Bali wewe umetuadhibu vikali katika mahali pa mbweha na kutufunika na uvuli wa mauti.
然どなんぢは野犬のすみかにてわれらをきずつけ死蔭をもてわれらをおほひ給へり
20 Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kueneza mikono yetu kwa Mungu mgeni,
われらもしおのれの神の名をわすれ或はわれらの手を異神にのべしことあらんには
21 Mungu asingeligundua hili? Kwa maana yeye anazijua siri za moyo.
神はこれを糺したまはざらんや 神はこころの隠れたることをも知たまふ
22 Hakika, kwa ajili ya jina lako tutauawa siku zote; tunahesabiwa kuwa kondoo kwa ajili ya kuchinjwa.
われらは終日なんぢのために死にわたされ屠られんとする羊の如くせられたり
23 Bwana, amka, kwa nini unalala? Inuka, usitutupe moja kwa moja.
主よさめたまへ何なればねぶりたまふや起たまへ われらをとこしへに棄たまふなかれ
24 Kwa nini unaficha uso wako na kusahau mateso yetu na kukandamizwa kwetu?
いかなれば聖顔をかくしてわれらがうくる苦難と虐待とをわすれたまふや
25 Kwa maana tumeyeyushwa kwenye mavumbi; miili yetu imeshikamana na ardhi.
われらのたましひはかがみて塵にふし われらの腹は土につきたり
26 Inuka utusaidie na utuokoe kwa ajili ya uaminifu wa agano lako.
ねがはくは起てわれらをたすけたまへ なんぢの仁慈のゆゑをもてわれらを贖ひたまへ

< Zaburi 44 >