< Zaburi 31 >

1 Kwa kiongozi wa muziki. Zaburi ya Daudi. In wewe, Yahwe, nakimbilia usalama; usiniache niaibishwe. Katika haki yako uniokoe.
Au maître de chant. Psaume de David. Yahweh, en toi j’ai placé mon refuge: que jamais je ne sois confondu! Dans ta justice sauve-moi!
2 Unisikie; uniokoe haraka; uwe mwamba wangu wa usalama, ngome ya kuniokoa.
Incline vers moi ton oreille, hâte-toi de me délivrer! Sois pour moi un rocher protecteur, une forteresse où je trouve mon salut!
3 Kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu; kwa hiyo kwa ajili ya jina lako, uniongoze na unielekeze.
Car tu es mon rocher, ma forteresse, et à cause de ton nom tu me conduiras et me dirigeras.
4 Unitoe katika mtego ambao wameuficha kwa ajili yangu, kwa kuwa wewe ni usalama wangu.
Tu me tireras du filet qu’ils m’ont tendu, car tu es ma défense.
5 Mikononi mwako naikabidhi roho yangu; nawe utaniokoa, Yahwe, mwenye kuaminika.
Entre tes mains je remets mon esprit; tu me délivreras, Yahweh, Dieu de vérité!
6 Ninawachukia wale wanaotumikia miungu isiyo na maana, bali ninaamini katika Yahwe.
Je hais ceux qui révèrent de vaines idoles: pour moi, c’est en Yahweh que je me confie.
7 Nitafurahi na kushangilia katika uaminifu wa agano lako, kwa kuwa uliyaona mateso yangu; wewe uliijua dhiki ya moyo wangu.
Je tressaillirai de joie et d’allégresse à cause de ta bonté, car tu as regardé ma misère, tu as vu les angoisses de mon âme,
8 Wewe haujaniweka kwenye mkono wa maadui zangu. Nawe umeiweka miguu yangu mahali pa wazi papana.
et tu ne m’as pas livré aux mains de l’ennemi; tu donnes à mes pieds un libre espace.
9 Uniurumie, Yahwe, kwa maana niko katika dhiki; macho yangu yanafifia kwa huzuni pamoja na moyo wangu na mwili wangu.
Aie pitié de moi, Yahweh, car je suis dans la détresse; mon œil est usé par le chagrin, ainsi que mon âme et mes entrailles.
10 Kwa kuwa maisha yangu yamechoshwa kwa huzuni na miaka yangu kwa kuugua kwangu. Nimekuwa dhaifu kwa sababu ya dhambi zangu, na mifupa yangu inachakaa.
Ma vie se consume dans la douleur, et mes années dans les gémissements; ma force est épuisée à cause de mon iniquité, et mes os dépérissent.
11 Kwa sababu ya maadui zangu wote, watu wananibeza; majirani zangu wanaishangaa hali yangu, na wale wanao nifahamu wanashtuka. Wale wanionao mitaani hunikimbia.
Tous mes adversaires m’ont rendu un objet d’opprobre; un fardeau pour mes voisins, un objet d’effroi pour mes amis.
12 Nimesahaulika kama mtu aliye kufa ambaye hakuna mtu anaye mfikiria. Niko kama chungu kilicho pasuka.
Je suis en oubli, comme un mort, loin des cœurs; je suis comme un vase brisé.
13 Kwa maana nimesikia minong'ono ya wengi, habari za kutisha kutoka pande zote kwa pamoja wamepanga njama kinyume na mimi. Wao wanapanga njama ya kuniua.
Car j’ai appris les mauvais propos de la foule, l’épouvante qui règne à l’entour, pendant qu’ils tiennent conseil contre moi: ils ourdissent des complots pour m’ôter la vie.
14 Bali mimi ninakuamini wewe, Yahwe; Ninasema, “Wewe ni Mungu wangu.”
Et moi, je me confie en toi, Yahweh; je dis: « Tu es mon Dieu! »
15 Hatima yangu iko mikononi mwako. Uniokoe mikononi mwa maadui zangu na wale wanao nifukuzia.
Mes destinées sont dans ta main; délivre-moi de la main de mes ennemis et de mes persécuteurs!
16 Nuru ya uso wako imuangazie mtumishi wako; uniokoe katika uaminifu wa agano lako.
Fais luire ta face sur ton serviteur, sauve-moi par ta grâce!
17 Usiniache niaibishwe, Yahwe; kwa maana ninakuita wewe! Waovu waaibishwe! Na wanyamaze kimya kuzimuni. (Sheol h7585)
Yahweh, que je ne sois pas confondu quand je t’invoque! Que la confusion soit pour les méchants! Qu’ils descendent en silence au schéol! (Sheol h7585)
18 Na inyamazishwe midomo midanganyifu ambayo husema maneno mabaya kuhusu watu wenye haki huku wakiwa na kiburi na dharau.
Qu’elles deviennent muettes les lèvres menteuses, qui parlent avec arrogance contre le juste, avec orgueil et mépris.
19 Uzuri wako ni wa namna gani nao umeuhifadhii kwa ajili ya wale wanao kuheshimu sana, ambao wewe huufanya kwa ajili ya wale ambao hukimbilia kwako kwa ajili ya usalama mbele ya watoto wote wa wanadamu!
Qu’elle est grande ta bonté, que tu tiens en réserve pour ceux qui te craignent, que tu témoignes à ceux qui mettent en toi leur refuge, à la vue des enfants des hommes!
20 Katika makao ya uwepo wako, wewe huwaficha mbali na njama za watu. Wewe huwaficha mahali salama na ndimi zenye vurugu.
Tu les mets à couvert, dans l’asile de ta face, contre les machinations des hommes; tu les caches dans ta tente, à l’abri des langues qui les attaquent.
21 Atukuzwe Yahwe, kwa maana yeye alinionesha maajabu ya uaminifu wa agano lake mahali nilipoishi.
Béni soit Yahweh! Car il a signalé sa grâce envers moi, en me mettant dans une ville forte.
22 Ingawa kwa haraka zangu nilisema, “Nimeondolewa machoni pako,” bali wewe ulisikia kusihi kwangu nilipokulilia wewe.
Je disais dans mon trouble: « Je suis rejeté loin de ton regard! » Mais tu as entendu la voix de mes supplications, quand j’ai crié vers toi.
23 Enyi wafuasi waaminifu, mpendeni Yahwe, Yahwe huwalinda waaminifu, lakini huwalipa wakaidi ipasavyo.
Aimez Yahweh, vous tous qui êtes pieux envers lui. Yahweh garde les fidèles, et il punit sévèrement les orgueilleux.
24 Iweni imara na jasiri, ninyi nyote mnao mwamini Mungu kuwasaidia.
Ayez courage, et que votre cœur s’affermisse, vous tous qui espérez en Yahweh!

< Zaburi 31 >