< Zaburi 2 >
1 Kwa nini mataifa wanafanya dhoruba, kwa nini watu wanafanya njama ambazo zitafeli?
Pourquoi les nations s'agitent-elles? Pourquoi les peuples forment-ils de vains projets?
2 Wafalme wa nchi kwa pamoja hushikilia misimamo yao na watawala kwa pamoja hufanya njama kinyume na Yahwe na kinyume na Masihi, wakisema,
Les rois de la terre se sont soulevés, Et les princes conspirent ensemble Contre l'Éternel et contre son Oint.
3 “Ngoja tuzikate pingu walizo tufingia sisi na kuzitupa pingu zao.”
— Rompons leurs liens, disent-ils. Et jetons loin de nous leurs chaînes!
4 Yeye aketie katika mbingu atacheka kwa dharau mbele yao; Bwana atawadhihaki wao.
— Celui qui habite dans les deux en rira; Le Seigneur se moquera d'eux.
5 Kisha ataongea nao katika hasira yake na kuwaogofya kwa gadhabu yake, akisema,
Alors il leur parlera dans sa colère; Il les épouvantera par son courroux.
6 “Mimi mwenyewe nilimpaka mafuta mfalme wa Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
— Et moi, dira-t-il, j'ai sacré mon roi Sur Sion, ma montagne sainte.
7 Nami nitatangaza amri ya Yahwe. Yeye aliniambia, “wewe ni mwanangu! Leo hii nimekuwa baba yako.
— Je publierai le décret. L'Éternel m'a dit: «Tu es mon Fils; Aujourd'hui je t'ai engendré.
8 Uniombe, nami nitakupa wewe taifa kwa ajili ya urithi na mikoa ya nchi iliyo bora kwa ajili ya umiliki wako.
Demande-moi, et je te donnerai pour héritage les nations. Pour possession les extrémités de la terre.
9 Wewe utawavunja wao kwa fimbo ya chuma; kama vile mtungi wa mfinyanzi, wewe utawavunja wao vipande vipande.”
Tu les briseras avec un sceptre de fer; Tu les mettras en pièces comme un vase de potier.»
10 Hivyo sasa, ninyi wafalme; mchukue tahadhari; mjirekebishe.
Maintenant donc, ô rois, ayez de l'intelligence; Laissez-vous instruire, juges de la terre!
11 Mwabuduni Yahwe kwa hofu na mfurahi mkitetemeka.
Servez l'Éternel avec crainte. Et réjouissez-vous avec tremblement.
12 Mumbusu mwana vinginevyo atawakasirikia, na mtakufa pale pale hasira yake ikiwaka. Ni jinsi gani wamebarikiwa wale wote watafutao usalama ndani yake.
Rendez hommage au Fils, de peur qu'il ne s'irrite, Et que vous ne périssiez dans la voie que vous suivez; Car sa colère est prompte à s'enflammer. Heureux tous ceux qui cherchent leur refuge en lui!