< Zaburi 146 >

1 Msifu Yahwe. Msifu Yahwe, ee nafsi yangu.
הללו-יה הללי נפשי את-יהוה
2 Ninamsifu Mungu maisha yangu yote; nitamuimbia sifa Mungu wangu ni ngali ni hai.
אהללה יהוה בחיי אזמרה לאלהי בעודי
3 Msiweke imani katika wakuu au wanadamu, ambaye katika yeye hamna wokovu.
אל-תבטחו בנדיבים-- בבן-אדם שאין לו תשועה
4 Wakati uhai wa pumzi ya mtu unapokoma, hurudi aridhini; siku hiyo mipango yake hufikia mwisho.
תצא רוחו ישב לאדמתו ביום ההוא אבדו עשתנתיו
5 Amebarikiwa yule ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake liko katika Yahwe Mungu wake.
אשרי--שאל יעקב בעזרו שברו על-יהוה אלהיו
6 Yahwe aliumba mbingu na nchi, bahari, na vyote vilivyomo; huitazama kweli milele.
עשה שמים וארץ-- את-הים ואת-כל-אשר-בם השמר אמת לעולם
7 Yeye hutekeleza hukumu kwa ajili ya walioonewa na huwapa chakula wenye njaa. Yahwe huwafungua waliofungwa;
עשה משפט לעשוקים--נתן לחם לרעבים יהוה מתיר אסורים
8 Yahwe huyafungua macho ya kipofu; Yahwe huwainua walioinama; Yahwe huwapenda watu wenye haki.
יהוה פקח עורים--יהוה זקף כפופים יהוה אהב צדיקים
9 Yahwe huwalinda wageni katika nchi; huwainua yatima na wajane, bali huipinga njia ya wasio haki.
יהוה שמר את-גרים--יתום ואלמנה יעודד ודרך רשעים יעות
10 Yahwe atatawala milele, Mungu wako, Sayuni, kwa vizazi vyote. Msifuni Yahwe.
ימלך יהוה לעולם-- אלהיך ציון לדר ודר הללו-יה

< Zaburi 146 >