< Zaburi 135 >

1 Msifuni Yahwe. Lisifuni jina la Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe,
Pujilah TUHAN! Pujilah nama TUHAN, hai kamu hamba-hamba-Nya
2 ninyi msimamao katika nyumba ya Yahwe, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
yang berbakti di Rumah TUHAN di kediaman Allah kita.
3 Msifuni Yahwe, kwa kuwa ni mwema; liimbieni sifa jina lake, maana ni vizuri kufanya hivyo.
Pujilah TUHAN, sebab Ia baik, pujilah nama-Nya, sebab Ia murah hati.
4 Kwa kuwa Yahwe amemchagua Yakobo kwa ajili yake mwenyewe, Israeli kama urithi wake.
Ia memilih Yakub bagi diri-Nya, umat Israel dijadikan milik-Nya.
5 Najua ya kuwa Yahwe ni mkuu, na kwamba Bwana wetu yuko juu ya miungu yote.
Sebab aku tahu TUHAN sungguh besar, Ia agung melebihi segala dewa.
6 Chochote Yahwe apendacho, hufanya mbinguni, duniani, katika bahari na katika vilindi vyote.
Ia melakukan apa yang dikehendaki-Nya, di langit dan di bumi, di laut dan di samudra yang dalam.
7 Hushusha mawingu kutoka mbali, akifanya mianga ya radi kuongozana na mvua na kuleta upepo toka katika ghala yake.
Dari ujung bumi Ia mendatangkan awan, dibuat-Nya kilat untuk hujan. Lalu Ia memerintahkan angin supaya keluar dari tempat penyimpanan-Nya.
8 Aliua mzaliwa wa kwanza wa Misri, wote wanadamu na wanyama.
Di Mesir Ia membunuh semua anak sulung dari manusia maupun binatang.
9 Alituma ishara na maajabu kati yako Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
Di sana dibuat-Nya banyak keajaiban dan tanda untuk menghukum raja dan semua pegawainya.
10 Aliwashambulia mataifa mengi na aliua wafalme wenye nguvu,
Ia membinasakan banyak bangsa, dan membunuh raja-raja perkasa:
11 Sihoni mfalme wa Waamori na Ogu mfalme wa Bashani na falme zote za Kanaani.
Sihon raja Amori dan Og raja Basan, serta semua raja di Kanaan.
12 Alitupatia sisi nchi yao kama urithi, urithi wa Israeli watu wake.
Lalu negeri mereka diserahkan-Nya menjadi milik Israel, umat-Nya.
13 Jina lako, Yahwe, inadumu milele; Yahwe, kumbukumbu lako vizazi hata vizazi.
Ya TUHAN, Engkau akan tetap diwartakan, dan nama-Mu diingat oleh semua keturunan,
14 Kwa kuwa Bwana huwatetea watu wake na anahuruma juu ya watumishi wake.
sebab Engkau memberi keadilan kepada umat-Mu, dan mengasihani hamba-hamba-Mu.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
Berhala mereka dari emas dan perak, buatan tangan manusia.
16 Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
Mereka mempunyai mulut, tetapi tak dapat berbicara, mempunyai mata, tetapi tak dapat melihat.
17 zina masikio, lakini hazisikii, wala vinywani mwao hamna pumzi.
Mereka mempunyai telinga, tetapi tak dapat mendengar, dari mulutnya tidak keluar napas.
18 Wale wazitengenezao wanafanana nazo, vilevile kila anaye zitumainia.
Semoga begitulah nasib orang-orang yang membuatnya, dan yang percaya kepadanya.
19 Enyi kizazi cha Israeli, mtukuzeni Yahwe; kizazi cha Haruni, mtukuzeni Yahwe.
Pujilah TUHAN, hai umat Israel, pujilah Dia, hai imam-imam Allah!
20 Kizazi cha Lawi, mtukuzeni Yahwe.
Pujilah TUHAN, hai orang-orang Lewi, pujilah Dia, kamu semua yang takwa.
21 Atukuzwe Yahwe katika Sayuni, yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Yahwe.
Pujilah TUHAN di Sion, di Yerusalem tempat kediaman-Nya. Pujilah TUHAN!

< Zaburi 135 >