< Zaburi 121 >
1 Nitayainua macho yangu nitazame milimani. Msaada wangu utatoka wapi?
Canción de las gradas. Alzaré mis ojos a los montes, de donde vendrá mi socorro.
2 Msaada wangu unatoka kwa Yahwe, aliyezifanya mbingu na nchi.
Mi socorro viene de parte del SEÑOR, que hizo los cielos y la tierra.
3 Hatauacha mguu wako uteleze; yeye akulindaye hatasinzia.
No dará tu pie al resbaladero; ni se dormirá el que te guarda.
4 Tazama, mlinzi wa Israeli hatasinzia wala hatalala usingizi kamwe.
He aquí, no se adormecerá ni dormirá el que guarda a Israel.
5 Yahwe ni mlinzi wako; Yahwe ni uvuli mkono wako wa kuume.
El SEÑOR será tu guardador; el SEÑOR será tu sombra a tu mano derecha.
6 Jua halitakudhuru wakati wa mchana, wala mwezi wakati wa usiku.
El sol no te fatigará de día, ni la luna de noche.
7 Yahwe atakulinda na madhara yote, na ataulinda uhai wako.
El SEÑOR te guardará de todo mal; el guardará tu alma.
8 Yahwe atakulinda katika yote ufanyayo sasa na hata milele.
El SEÑOR guardará tu salida y tu entrada, desde ahora y para siempre.