< Zaburi 118 >
1 Mshukuruni Yahwe, kwa kuwa ni mwema, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
你们要称谢耶和华,因他本为善; 他的慈爱永远长存!
2 Israeli na aseme, “Uaminifu wa agano lake wadumu milele.”
愿以色列说: 他的慈爱永远长存!
3 Nyumba ya Haruni na iseme, “Uaminifu wa agano lake wadumu milele.”
愿亚伦的家说: 他的慈爱永远长存!
4 Wafuasi waaminifu wa Yahwe na waseme, “Uaminifu wa agano lake wadumu milele.”
愿敬畏耶和华的说: 他的慈爱永远长存!
5 Katika dhiki yangu nilimuita Yahwe; Yahwe alinijibu na kuniweka huru.
我在急难中求告耶和华,他就应允我, 把我安置在宽阔之地。
6 Yahwe yuko pamoja nami; sitaogopa; mwanadamu atanifanya nini? Yahwe yuko upande wangu kama msaidizi;
有耶和华帮助我,我必不惧怕, 人能把我怎么样呢?
7 nitawatazama kwa ushindi wale walio nichukia.
在那帮助我的人中,有耶和华帮助我, 所以我要看见那恨我的人遭报。
8 Ni bora kuwa na makazi katika Yahwe kuliko kumtumainia mwanadamu.
投靠耶和华,强似倚赖人;
9 Ni bora kukimbilia katika Yahwe kuliko kuamini katika wakuu.
投靠耶和华,强似倚赖王子。
10 Mataifa yote walinizunguka; kwa jina la Yahwe niliwakatilia mbali.
万民围绕我, 我靠耶和华的名必剿灭他们。
11 Walinizunguka; naam, walinizunguka; kwa jina la Yahwe niliwakatilia mbali.
他们环绕我,围困我, 我靠耶和华的名必剿灭他们。
12 Walinizunguka kama nyuki; walitoweka haraka kama moto kati ya miiba; kwa jina la Yahwe niliwakatilia mbali.
他们如同蜂子围绕我, 好像烧荆棘的火,必被熄灭; 我靠耶和华的名,必剿灭他们。
13 Walinishambulia ili waniangushe, lakini Yahwe alinisaidia.
你推我,要叫我跌倒, 但耶和华帮助了我。
14 Yahwe ni nguvu yangu na furaha yangu, na ndiye anaye niokoa.
耶和华是我的力量,是我的诗歌; 他也成了我的拯救。
15 Kelele za ushindi zimesikika katika maskani ya wenye haki; mkono wa kuume wa Mungu umeshinda.
在义人的帐棚里,有欢呼拯救的声音; 耶和华的右手施展大能。
16 Mkono wa kuume wa Mungu umetukuka; mkono wa kuume wa Yahwe umeshinda.
耶和华的右手高举; 耶和华的右手施展大能。
17 Sitakufa, bali nitaishi na kuyatangaza matendo ya Yahwe.
我必不致死,仍要存活, 并要传扬耶和华的作为。
18 Yahwe ameniadhibu vikali; lakini hajaruhusu nife.
耶和华虽严严地惩治我, 却未曾将我交于死亡。
19 Unifungulie milango ya haki; nitaingia na nitamshukuru Yahwe.
给我敞开义门; 我要进去称谢耶和华!
20 Hili ni lango la Yahwe; wenye haki hupitia kwalo.
这是耶和华的门; 义人要进去!
21 Nitakushukuru wewe, kwa kuwa ulinijibu, na umekuwa wokovu wangu.
我要称谢你,因为你已经应允我, 又成了我的拯救!
22 Jiwe ambalo wajenzi walilikataa wajenzi limekuwa msingi.
匠人所弃的石头 已成了房角的头块石头。
23 Yahwe ndiye afanyaye hili; ni la ajabu machoni petu.
这是耶和华所做的, 在我们眼中看为希奇。
24 Hii ni siku ambayo Yahwe ametenda; tutaifurahia na kuishangilia.
这是耶和华所定的日子, 我们在其中要高兴欢喜!
25 Tafadhali, Yahwe, utupe ushindi! Tafadhali, Yahwe, utupe mafanikio!
耶和华啊,求你拯救! 耶和华啊,求你使我们亨通!
26 Amebarikiwa yule ajaye katika jina la Yahwe; tunakubariki kutoka katika nyumba ya Yahwe.
奉耶和华名来的是应当称颂的! 我们从耶和华的殿中为你们祝福!
27 Yahwe ni Mungu, na ametupa sisi nuru; ifungeni dhabihu kwa kamba pembeni mwa madhabahu.
耶和华是 神; 他光照了我们。 理当用绳索把祭牲拴住, 牵到坛角那里。
28 Wewe ni Mungu wangu, nami nitakushukuru; wewe ni Mungu wangu; nitakutukuza wewe.
你是我的 神,我要称谢你! 你是我的 神,我要尊崇你!
29 Oh, mshukuruni Yahwe; kwa kuwa ni mwema; kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
你们要称谢耶和华,因他本为善; 他的慈爱永远长存!